Kilichofanya wazazi wako wasiwe Matajiri miaka hiyo ndicho kinafanya wewe usiwe tajiri miaka ya leo. Acha lawama!

Kilichofanya wazazi wako wasiwe Matajiri miaka hiyo ndicho kinafanya wewe usiwe tajiri miaka ya leo. Acha lawama!

TUKANA UONE

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2018
Posts
2,345
Reaction score
6,970
Kumekuwa na mitazamo ambayo inaambatana na lawama kutoka kwa watu tofauti tofauti wakiendelea kuwalaumu ndugu zao au wazazi wao eti kwanini wamekuja mjini hasa Dar es Salaam miaka ya nyuma ambayo kila kitu kilikuwa cheap (rahisi) na hawana maeneo, nyumba Wala ukwasi ambao wanadai Kwa miaka hiyo ilikuwa rahisi kupata!

Unakuta huyo mtu anayelaumu, amekuja Dar es Salaam huu ni mwaka wa 20 na zaidi hana chochote cha maana!

Ok yeye alishindwa kuwa tajiri, wewe kimekushinda nini kuwa tajiri leo, kilichokushinda kununua uwanja na maeneo makubwa hadi sasa ni nini?

Vijana acheni lawama, mambo si rahisi kama mnavyodhani! Tena mbaya zaidi unakuta ukoo wenu au familia yenu haina mkondo huo wa pesa ndiyo utapata taabu sana!

Familia nyingi zilizoendelea miaka hiyo na zinazoendelea miaka hii, ni lazima walikuwa na ka-uwezo tangu mwanzo hivyo walishikana na wanaendelea kushikana mikono!

Ni ngumu mno mtu hakuwa na kitu kabisa akaanza moja hadi kuwa tajiri,kama ambavyo imekuwa ngumu kwako!,vinginevyo uenda ukawe Tapeli au Mwizi!
 
SIO LAZIMA UWE TAJIRI

Cha msingi ufanikiwe kujipatia

FOOD, SHELTER AND Cloth

Hayo mengine ni matokeo ya safari zetu za kutafuta maisha
 
SIO LAZIMA UWE TAJIRI

Cha msingi ufanikiwe kujipatia

FOOD, SHELTER AND Cloth

Hayo mengine ni matokeo ya safari zetu za kutafuta maisha

Sio Lazima , ila ni Jambo la Muhimu kuwa tajiri.

Wote tutakufa, iwe maskin au tajiri ,
Hatujui tunapoenda.

Ni vema tuishi Dunia hii kwa raha na Furaha.

Ukiwa tajiri , shida nying utatatua .hivyo ni Muhim kuwa tajiri
 
Back
Top Bottom