Kilichomponza Mwanakwerekwe, ni dada yake Halima kukata mauno mbele ya wakwe zake!

TUKANA UONE

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2018
Posts
2,345
Reaction score
6,970
Jamaa walitoa tahadhari mapema wakasema,mikong'oto heavy ni Kwa ajili ya Vibaka na Walanguzi walioshindikana hapa Barani Afrika,yeyote atakaye ingia kati wakati mikong'oto hiyo ikiendelea, atajikuta anapokea kichapo kisichokuwa na huruma kama Paka shume aliyekunya kwenye debe la Unga wa uwele!

Hiki ndicho kilichomkuta Leo Mwanakwerekwe,wakati mdogo wake aitwaye Halima Maturunganya alipoamua kusaula nguo zake akabaki na mfuniko wa mboga huku akinengua na kuserebuka mbele ya Wakwe zake!

Kilichofuata baada ya hapo hatokuja tena kurudia maana kipigo alichopokea kimemfanya awe kibogoyo maisha yake yote!

Kibaya zaidi wakwe zake wameyachukua yale meno na kuondoka nayo huku wakisema siku atakapoenda kuwaomba radhi,basi watamrudishia meno yake akayatunze kwenye mkoba wake akiwa anayaangalia anabaki kutabasamu!


The teh teh teh teh teh teh chezea wakwe weyeeeeeeee!
 
Muafrika bhana..kwa akili yote yanga ni kubwa kuliko Simba sc?πŸ˜€πŸ˜€...Simba sc ni imeshakuwa timu kubwa na bora na 5 barani Afrika,sasa hivi ni ya 6..yanga tokea iyanzishwe haijawahi kuingia top 10,Simba ndio timu ya kwanza kuchukua kombe la ligii kuu Tanzania mwaka 1965 na 1966,Simba sc ndio timu ya kwanza kufika nusu final club bingwa 1974,imecheza robo final club bingwa mara 5 mfululuzo,yanga ndio kacheza juzi moja,Simba ndio timu ya kwanza Tanzania kufika final shirikisho mwaka 1993,rais Samia aliwaambia mlipi nyie wenzenu walishapita miaka 30 iliyopita,Simba ndio timu ya kwanza Tanzania kucheza Super league,league ya timu 8 kubwa na bora barani Afrika,hiyo yanga yako bado haijawahi kucheza,Simba ndio club iliyochaguliwa na FIFA kuwania kushiriki kombe la dunia la vilabu kwa mwaka 2025 hiyo yanga ipo wap...utasema ndio ya kwanza kuanzisha ndio akili yenu ilipoishia,sasa ipo hivi ukubwa na ubora wa timu katika bara lake ni ukubwa na ubora aliyonayo katika bara lake na namna inavyojulikana dunia huko...uanzishaji ingekuwa kigezo basi Pamba iliyopanda daraja juzi ingekuwa ndio timu kubwa kuliko Azam,MAMELODY,Belouizdad n.k kwasababu pamba ni ya muda mrefu.
 
Bado hujasema, mpaaaka useme
 
Povu grade one,
na bado, mtani endelea kuporomosha takwimu ila kichapo kiko pale kila mkijaa kwenye 18 za uto!! Subiri October kazi inaendelea tulipoishia nane nane!! Hao FIFA na CAF ndio waliokataa goli la Aziz Ki, nao kuna siku watasema imetosha tuipe Yanga maua yake!!
 
Zilipendwa hizo. Walipata ukubwa wakati wa korona walipokuwa wanawafanyia uhuni timu pinzani na kuwabambikiza korona wachezaji wote wazuri wa wapinzani.

We bi. debora utakuwa na matatizo ya akili.
 
Hizi ni hadithi hata kwenye kanga zipo!
 
Simba ndogo sana kwa Yanga, haya mko namba sita Africa kwa kombe lipo. Nyie mnaizidi Yanga uchawi tu. Hii Yanga imechukua makombe mengi ya ndani kuliko Simba. FA Yanga mengi, Ligi kuu Yanga mengi hadi ngao ya jamii Yanga mengi kuliko Simba. Mnapiga kelele tu kwa sifa za kijinga.
 
Kila siku ni kutoa historia tu..,fanyeni kweli acheni ngojera!
 
YANGA BINGWA [emoji2957]
 
Bado hamjasema mpaka mseme.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…