Elections 2010 Kilichonishtua Juu Ya Dr Slaa Pale Mwembetogwa


Hili linapaswa kufanyiwa kazi, hii ilikuwa ni fursa nzuri ya kuwaeleza WanaIringa umuhimu wa wao kumchagua Mchungaji Msigwa badala ya Mama Mbega.
 
Marksman,

Unaandika usichokijua. Sasa hilo ni tatizo lako. Kama unahitaji msaada wa kujuzwa, omba.

Pole Maggid kwa shambulizi la mlenga shabaha Marksman. Nadhani kakushambulia kuhusu JAMII KWANZA kwa kukuonea. Kuna vitu vingi vinahitajika ili gazeti lisimame. Marksman hajui.

Maggid sijaanza leo kusoma makala zako. Ni tangu enzi za Rai ileeeee. Kama sijakosea wewe ni Mwalimu au umewahi kuwa mwalimu. Hata hivyo naona kama kuna ka-bias japo kadogo kanuku-affect towards CCM. Je unadhani ni kitu gani kimefanya mkutano wa CHADEMA uweke rekodi ya mahudhurio (Kama utaweza jaribu kukisia kilicho vichwani mwao)? Kitu gani pia kinafanya watu wajae mkutano wa CHADEMA huku wakiwa hawajui ofisi za CHADEMA? Kitendo cha watu "kujua" ofisi za CCM zilipo ni kutokana na Oganaizeshenii nzuri ya CCM au historia? Je, kwanini Slaa ana nguvu sana sasa ilhali JK ndo yuko "katikati" ya miaka 10 (mazoea anayeanza huwa na nguvu zaidi)? Je, wananchi wanaoshangilia CHADEMA halafu kesho mjumbe/balozi wa nyumba 10 (wa CCM obviously) "akawafuata" wana uwezo gani wa kufikiri? Je, kusambaa huku kwa CCM kutaondolewa na CUF au CHADEMA nayo kusambaa that much?
 

majjid uchambuzi wako uko wazi kabisa na unaeleweka usihangaike kujibishana na hawa watu watakupoTezea muda wako wa kutuletea tathmini zingine, kwani kazi zao ni kungoja wanaume walete hoja huku halafu wao utasikia ooo ccm huyu, cuf huyu, mjahidina huyu, mdini huyu!!! JF KUNA MEMBERS ZAIDI YA 1000 HIVYO HAWA WACHACHE WASIOAMBILIKA WASIKUBABAISHE!!! MBONA WAO WAKIJA NA HOJA HAPA MBONA NI PUMBA TUPU!!!!

Hawa watu utafikiri wanaishi nyakati za stone age!!! Wao wanataka umsifie slaa kuanzia mwanzo mpaka mwisho!!! Sasa dr.slaa anaanza kutukumbusha hotuba za lyatonga mrema za kutoa siku 7!!! Anamtishia afisa wa jeshi kwa kumpa siku 7!!!
Inaonekana yale mabomu yake 20 yameshaisha isha na huku akiendelea kushinikizwa amrudishe mke wa mtu!!!
 
3D,
Ahsante sana.
Hayo ndio maswali ya msingi tunayopaswa kuulizana sasa kwa maslahi ya nchi yetu. Lakini hata hawa wanaokurupuka na kunishambulia mimi kama mtoa hoja nawapenda sana. Ni sehemu ya jamii yetu na kuna sababu za wao kufanya hivyo. Uliyoyauliza ni ya msingi sana. Naweza kuyatolea maelezo marefu, lakini nitafupisha. Ninaposema Iringa ni ngome ya CCM kuna sababu za kihistoria za tangu enzi za TANU. Wengi hawafahamu kuwa ni Iringa ambako Nyerere alikubalika sana na kupata sapoti kubwa wakati akipigania uhuru wetu. Miaka ya hamsini alipotoka kwenye harakati zake Iringa mjini alifika pale kijijini Ilula. Watu walijaa kumsikiliza. Mwisho wa hotuba yake Watanganyika wale wa Ilula walimkabidhi Mwalimu ' Kifyagilo' kwa maana ya kifagio. Walimwambia aende nacho Dar es Salaam akawafagilie mbali wakoloni. Ilikuwa ni jambo la ishara. Na Mwalimu na wenzake katika TANU walitumia ' kifyagilo' kile kama alama katika kadi ya TANU. Mliopata kuziona kadi za TANU mtakumbuka kuona alama ya kifyagilo.

Kama nilivyosema kuna mengi niliyoyaona pale Mwembetogwa ambayo naweza kuyaandkia kurasa kumi za makala. Lakini leo ni Jumapili, niko nyumbani na familia yangu. Ila kwa ufupi tu, nakiona kitu kimoja cha msingi. Kwamba Watanzania waliosoma miaka ishirini iliyopita wamesoma kwa tabu sana. Sisi wengine tulibahatika kusoma bure. Pale Tambaza Sekondari tulisoma bure na tulikula bure. Hata matunda tuliletewa na serikali. Sasa hapa kuna ' nostalgie' fulani. Maana waliosoma miaka ishirini iliyopita wanalijua hilo, lakini wao wamesoma kwa tabu. Na sasa, waliosoma miaka ishirini iliyopita kwa tabu sasa ni wazazi wanaosomesha kwa tabu sana. Na idadi yao inaongezeka. Kwa mwanasiasa makini lazima alibaini kundi hili ambalo CHADEMA na hususan Freeman Mbowe alikuwa hodari sana wa kulibaini na kulipa jina la " Wanaopigika".
Kwa mtazamo wangu, vita kali ya kisiasa ya leo na kesho itakuwa ni kugombania kura za ' wanaopigika'. Kama inataka kuendelea kuongoza , CCM lazima irudi kwenye drawing board. Hata kama chumba umekichoka , unaweza kuanza na kubadilisha mashuka na pazia....
Ngoja nikawaandalie chakula wana wangu. Nikipata nafasi baadae nitaendelea na ninachokifikiri kwa uhuru kabisa.
 
maggid wacha jazba. hata blog yako 95% ni CCM, kama ungekuwa neutral tungeona picha za vyama vyote equally au unapata za CCM zaidi?
Good day
 

Nimekuelewa Maggid, in reality binafsi napendelea mabadiliko. Kwa mazingira ya sasa ningependa kuona mabadiliko katika nchi. Hatimaye moyo wangu umeangukia kwa Dr. Slaa. Hata hivyo bado tunaweza kuzungumza kwa hoja bila kujali tunafanana ama kutofautiana.
 
Makala za Maggid hazina mvuto kama vile za Bagenda, tatizo lake anaandika vitu vilivyo nje ya uwezo wake. Hajui uchambuzi wa kisayansi na kisomi nadhani yeye angefaa zaidi kuwa mpiga picha au angalau ripota lakini sio mchambuzi. Uwezo wake wa kuchanganua mambo sio mkubwa. Hata ukiangalia milinganisho (analogy) yake zake katika makala zake kunakuwa hakuna mlingano. (makala zake huunza na kisa kisha hujaribu kujenga hoja juu ya hicho kisa) lakini ajabu kunakuwa hakuna ulinganifu kabisa.

Jikombe sana kwa CCM , unaweza kuambulia kuziba nafasi ya Nape pale Lumumba
 
Hivi Mjengwa mbona hakutupa tathmini ya Kikwete wakati anawafokea na kuwakashifu wafanyakazi pale Diamond Jubilee? Hata hivyo good job!, Sikujua Dr. Slaa alivuta maelfu Iringa kuliko mtu mwingine yeyote. Hilo limenipa tumaini. Big up!



MJENGWA , toa pia tathimini wa mkutano wa jk, ridhiwani , na mama salima , au umeaidiwa ukuu wa wilaya.
 
Kuna ugonjwa unaitwa "chambio(toilet tissue) la mafisadi" unawaathiri wanasiasa,waandishi na hata viongozi wa dini. Ukisikiliza na kusoma wanachoeleza hawa watu utajua kama wameathirika au la!
 
Negotiator said:
Kuna ugonjwa unaitwa "chambio (toilet tissue) la mafisadi" unawaathiri wanasiasa,waandishi na hata viongozi wa dini. Ukisikiliza na kusoma wanachoeleza hawa watu utajua kama wameathirika au la!

Chambio la Mafisadi???? This is an incredible new terminology in Tanzanian politics. Duuuuh, ya leo kali!!!
 
Jamani Maggid yupo sahihi kwa hili kasema ukweli ambao wengi hatupendi kuusikia. Hivi mnajua kwamba CHADEMA inawagombea wangapi Iringa wa nafasi ya Ubunge? Mnafaham kuwa kuna majimbo CCM inasubiri siku tu ili iyachukue. Hata km CHADEMA itashindi hayawezi kuwa zaidi ya majimbo mawili katika majimbo 9. Je inabaki kuwa ngome ya nani?
 
Mjengwa nadhani unapoteza muda tu kutaka kutuaminisha kuwa CCM is the best. Watu tulishaamua JK OUT. narudia tena analysis zako sio za kisomi kabisa.
Hizi dharau zinapitiliza. Tuwekee tathmini yako.
 

Ukilinganisha na Ulicho ulizwa, Hizo zote ni PuMBA. Maswali yalikua

  1. Je unadhani ni kitu gani kimefanya mkutano wa CHADEMA uweke rekodi ya mahudhurio (Kama utaweza jaribu kukisia kilicho vichwani mwao)?
  2. Kitu gani pia kinafanya watu wajae mkutano wa CHADEMA huku wakiwa hawajui ofisi za CHADEMA?
  3. Kitendo cha watu "kujua" ofisi za CCM zilipo ni kutokana na Oganaizeshenii nzuri ya CCM au historia?
  4. Je, kwanini Slaa ana nguvu sana sasa ilhali JK ndo yuko "katikati" ya miaka 10 (mazoea anayeanza huwa na nguvu zaidi)?
  5. Je, wananchi wanaoshangilia CHADEMA halafu kesho mjumbe/balozi wa nyumba 10 (wa CCM obviously) "akawafuata" wana uwezo gani wa kufikiri?
  6. Je, kusambaa huku kwa CCM kutaondolewa na CUF au CHADEMA nayo kusambaa that much?​
Jibu Japo maswali Matatu unayoyaweza, na uache Ubabaishaji wako wa makamba (std 7)
 

Nimechoka naona unanipotezea muda wangu na makala yako isiyo na makalio.
 
Hayo hapo juu ni sina haja ya kuyazungumzia kwasababu ukweli ni sawa na mafuta,hata kwenye maji yanajitenga....
Sumaku said:
Udhaifu wake:
- Anaanza hotuba yake kwa kuonyesha ana haraka kidogo. Wanaomsikiza nao wanapata ' stress' ya namna fulani. Watu wanaanza kuangalia saa zao pia. Details hizo zinaweza kumtoa nje msikilizaji.
Huo si udhaifu bali ni srenght.Kwasababu wananchi hao wanakuwa more alert kumsikiliza,wananchi wakijua kuwa wana muda mchache wa kumsikiliza basi wakuwa makini zaidi kwasbabu ya muda...mikutano mirefu ina negative impact kwasababu concentration inakuwa low due to boredom etc....Ni lazima ujiweke kwenye nafasi ya mwananchi wa kawaida na si kuandika feelings zako,conclusion yako ni "butu"

- Wakati mwingine anaonyesha jazba kidogo. Maneno kama ; " Kama Kikwete mwanamme…" Anatakiwa ayaepuke. Yanaweza kutafsiriwa vibaya na katika nchi nyingine wanaharakati wa jinsia wanaweza kumjia juu.
Wakati unaomba kura kwa watanzania unatakiwa uongee na watanzania na si kuwa please hao "nchi nyingine" ama eti wanaharakati wa jinsia,kuna issue ambazo ni local issues na kuna lugha inayotakiwa itumike kama unataka ku appeal to a certain group of citizens...again unaonyesha bias kwasababu sijaona tatizo lolote kwenye lugha hiyo,wananchi siyo wajinga kiasi hicho kama unavyotaka tuamini....Kama uanume ni kusimamia maslahi ya taifa basi sidhani kama hilo ni tatizo kwa wanachi.

- Anatoa maagizo, anatoa siku saba.. hata kabla hajaingia Ikulu. Labda angetamka zaidi " CHADEMA tunataka'. Kuna wapigakura wanaohofia kumwingiza madarakani mwenye silika za udikteta.

Again more bias,kwanza ulitakiwa utuwekee kauli hiyo ya siku saba ndiyo tupime.Wakati huu wa kampeni ni less than a month kabla ya zoezi la upigaji kura halijaanza,so sishangai kama akiweka msisitizo wa muda ie siku tatu,tano,saba nk....Pia unatakiwa uonyeshe ni kivipi kauli hiyo ni ya "Kidikteta" Je kauli za JK za vitisho kwamba ana uwezo wa kumfanyia mtu kitu chochote wakati wa hotuba zake ie ile ya wafanyakazi ni kitu gani?Zipi ni kauli za kidikteta kati ya hizo mbili?

Hilo sasa nalo ni tatizo la Dr Slaa ama chama chake kwa ujumla?Ni kivipi huo ni udhaifu wake?Je hakusema kwamba wataangalia uwezekano wa mchakato wa kupata katiba mpya ndani ya siku mia moja endapo watashinda?Kama ni kweli alishawahi kusema hayo basi umeonyesha tena udhaifu wa kuwa bias kwenye analysis yako....Kwa unafiki sisi wabongo ni namba moja.

Hapo ndiyo umeniacha hoi...Yani una imply kuwa Dr ni dhaifu sana na kwamba umma huo umekuja hapo kumsikiliza kwasababu ccm waliboronga kwenye process ya kumpata mgomba wa ubunge Iringa mjini....Hata hivyo wewe ndiyo umeboronga kabisa kwasababu ya kuandika kinafiki,sababu hiyo haiwezi kuwa sababu pekee ya ku conclude kama ulivyofanya,si sababu ya kuijengea hoja nzito,inawezekana ikawani sababu mojawapo tu,lakini si the only one and the main reason....cheki hapo chini ulivyojichanganya kwasababu hiyo hiyo ya unafiki...Na sometimes kuuma na kupuliza...Unauma kweliekweli (Lol!)Yani unasema wameenda kumsikiliza Dr Slaa kwasababu tu ya kuboronga kwa ccm?sasa unataka waseme nini tena kuhusiana na mgombea "Monica Mbega?"Hilo si tayari limempunguzia Dr Slaa mzigo?Just kama ufisadi ambavyo umesababisha umasikini kukithiri,na hivyo kueplekea kiu ya mabadiliko,kuboronga huko kwenye uchaguzi wa mgombea wao ni mojawapo tu ya injustices za chama tawala,lakini haina maana eti ni "Kura zao za maoni tu" ndizo zimewafanya wajazane kwenye mkutano wa Slaa.Sababu zilizowapelekea wananchi hao kumsikiliza Dr Slaa ni zaidi ya kura hizo za maoni za ccm,tafadhali jali kuhusu inteligence za wenzako,usiongee kama unatoa hadithi za alf lela ulela kwa kwa watoto wa chekechea,njoo na hoja nzito na si haya makapi.

Miongoni mwa waliomsikiliza Dr Slaa jana pale Mwembetogwa ni wanachama na wapenzi wengi wa CCM. Na ajabu kubwa kabisa; Dr Slaa tangu mwanzo hadi mwisho wa hotuba yake hakutamka jina la " Mama Monica Mbega". Mgombea Ubunge wa CCM, Iringa Mjini.
Sasa kama uliona ni "ajabu kubwa kabisa" then ulitakiwa uone pia kuwa makala yako hii nayo ni "ajabu kubwa kabisa",ajabu moja kubwa hupelekea ajabu nyingine kubwa....?Kwamba ulitaka watamke jina la mama Mbega ili baadae uje kusema ni negative campaining ?Kwamba hakukuwa na haja ya kulitaja jina lake tena?Sitaki ku invoke negative prediction,hata hivyo unaelekea kutapa tapa sana ili kuweza kupata sababu ya kujazia hizo dhaifu zako,kwa kifupi una struggle ili kuiwezesha ipate mashiko,tatizo ni kulazimishia na huwezi kutumia tope kujenga juu ya msingi wenye concrete,utachekesha....kwenye baadhi ya situations si lazima kutaja taja jina la mpinzani all the time,rather huo ni wkati wa kupenyeza message...Na kwa hilo nampongeza Dr,ataje jina la nini tena na umeshasema kuwa wako hapo kwasababu hiyo hiyo kuteuliwa kwa mama Mbega?Kama unakiri kuwa umma huo wakiwemo wanachama wa ccm waliojazana kwenye mkutano wa Slaa ili kumsikiliza ulichangiwa na uborongaji wa ccm,then ina maana kuwa tayari wananchi hao wako well informed na suala zima la mama Mbega. Tatizo ni kwamba haujakiri kuhusu ufisadi pia kuonyesha kuwa umewasukuma wananchi waliochoshwa waje hapo,unajidai kuwa umesahau how far wananchi hao wametoka in regard to kusota na umasikini,njaa,magonjwa, ukosefu wa elimu nk......Umsehau kuwa kutokea ile listi ya Mwembe Yanga wananchi wengi walifunguka macho,na kwahiyo Slaa yeye alipata muda wa kusema wao watafanya nini kama mbadala,sioni udhaifu wowote hapo,sijaona udhaifu wowote kwenye uchambuzi wako huu,samahani ndo ukweli huo.

Hata mgombea wa CHADEMA Mchungaji Msigwa alipopewa dakika tatu na Slaa aongee, naye hakutamka jina la " Monica Mbega" na kwanini wana Iringa Mjini wasimchague Monica Mbega.
Hivi mkuu wewe ndiyo mwenye tatizo ama una assume kuwa wananchi hao nao walikuwa na matatizo kama haya ya kwako?Je walikuwa na matatizo ya kufikiri kama haya?Kwamba wanajua sababu ya kwanini hawatamchagua Monica Mbega na ccm yake lakini bado wanataka waende kumsikiliza Dr Slaa akirudia rudia yale yale wanayoyafahamu?Kama ingekuwa hivyo si wangeondoka mkutanoni kama ilivyowatokea ccm ambapo na wewe pia hujaandika kuhusu hayo?mimi kwasasa sina muda na hivyo sijaweza kupitia topics nyingi wala kutembele blogs,however kuna wana jf wengi tu wanadai hawajawahi kuona ukitoa uchambuzi the same way kwa viongozi wengine wanaogombea ie JK

Hayo mengineyo bado ni hizo dhaifu zako za kufikirika?
Hii inaweza kuwa changamoto zaidi badala ya udhaifu...Kwanza nasikitika sana kwasababu unaoneka ku down play mwamko wa watanzania. Kwa wana ccm hao,inawezekana mizengwe ya chaguzi za wagombea ubunge kupitia chama chao ni mojawapo tu ya sababu za kuwakatisha tamaa baadhi ya wanachama hao,lakini haina maana hiyo ndiyo sababu pekee inayotosheleza kutoa conclusion kwamba eti ndiyo maana watu walijaa kwenda kumsikiliza mgmbea wa chadema....Yani ni very shallow kufanya analysis ya ki hivyo na at the same time kudown play resolve ya wananch at large kwa kudai kuwa hawaelewi kwamba ufisadi umechangia umasikini wao,na pia unainsult intelligence ya wengi wetu humu ndani. Unatakiwa uelewe there is a combination of factors as to why many citizens are tired and why the need change...Do not present your feelings as if they are facts and then you went ahead and drew conclusion based on those mischaractirizations, you want us to believe that you have done some reserch or even any efforts to interview some of those who attended the rally before drawing any conclusions....Huwezi kusema wananchi wote walikuwa wan feel the same way you felt,na wakati hukumhoji mtu yoyote wewe utabaki na conclusions zako tu,na ukamalizia kwa kusema eti sijui balozi wa nyumba kumi ndiyo wataenda kuwabadilisha mawazo wananchi hao....Bado tu kuna vielement vya kutuaminisha kuwa change is impossible.
 

Kama una frustrations zako nyingine ziwezi kukusaidia. Maswali nimeyaona na aliyeuliza hakunilazimisha niyajibu. Kuna maelezo ya jumla nimeyatoa kutokana na maswali hayo. Mengine nitajibu nitakapotaka na kama nitaweza kuyajibu yote siwezi kusema sasa. Mimi ni mtu huru na najivunia uhuru wangu. Nina maisha yangu mengine. Yanahitaji muda wangu pia.
 

JMushi,

Kuna mwandishi wa habari alikamatwa na kufikishwa kwa Idi Amin. Aliamini kuwa ungekuwa ni mwisho wake. Idi Amin alitamka na kumwuliza mwandishi yule swali moja tu; " Nyinyi waandishi wa habari mnaandika mambo mengi mbaya kuhusu mimi. Sasa nikuulize kijana, hivi katika yote ninayoongea na ninayoyafanya hakuna hata moja lililo zuri?" Mwandishi yule akajibu; " Yapo mengi Mkuu".

Idi Amin akatamka; " Basi, nenda kaandike moja tu lililo zuri kuhusu mimi!" Tafakari.
 
Na wewe mtani wangu kwani ni lazima ujibu kila kitu?

Wewe kama mwandishi uwe unaandika tu unayoyaona yanafaa kuandika.

Sisi kama Wasomaji tutasoma na kuamua kama kweli wewe ni MWAANDISHI kweli au na wewe ni Chambio la Mafisadi.

Jisikie huru kuandika unachotaka na sisi tuache tuwe HURU kukutafutia kundi unalostahili kuwa.

Acha kuandika na baadaye kuja hapa KUTETEA maelezo yako. Hata uandike kumsifu Slaa, wengine bado watakushambulia.

Nafuatilia sana makala zako. Mwenye akili anakuelewa na asiye na akili basi kazi kwake. Kuna wengine wanataka kutafuniwa kila kitu ila ujumbe wako wa kijibwa cha Manzese, ulisema yote.

Mbona hatukaribishani kwenye Ulanzi sasa? Mie ngoja nisema, karibu basi Sikonge, maembe yataanza hivi karibuni.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…