NALIA NGWENA
JF-Expert Member
- Oct 6, 2016
- 10,587
- 13,425
Acha kumtupia lawama Ayub Lagreb tuliyemsifu kwenye gemu Wydad Casablanca kwa kufanya saves za kutosha nasema acha kabisa.
Tatizo lipo kwa wachezaji (saikolojia Yao) waliingia na matokeo mfukoni wakiamini KMC atafungwa tu Tena nyingi Kama walivyofanya Yanga na Azam.
Nimetazama mpira mpaka nikajiuliza mbona kila mchezaji anataka kufunga? Papala zinakua Nyingi sana kisaikolojia walishaambiwa kuwa timu ipate magoli mengi na ndiyo maana kila mchezaji anataka kufunga hata Kama ni nafasi ya kupasia anataka afunge tu.
Nilimsikia msemaji wa Simba sc (Ahmedy Ally) akisema "Azam Fc wameifunga KMC goli tano na wapinzani wetu wameifunga goli tano Ila sisi tuna droo kwa kweli hiyo siyo nzuri"
Hapa Ahmedy Ally alizungumza kishabiki na kusahau kuwa Yanga Sc ni Bora na Azam Fc ni bora kuanzia beki, viungo na washambuliaji Azama na Yanga Sc kwa Sasa Wana Vikosi Bora.
Ukipiga hesabu za kihistoria Fulani kamfunga goli tano usipoangalia utashuka daraja maana mpira haupo hivyo na ndicho kilichotokea kwa Simba SC waliamini KMC watamfunga tu maana alishafungwa magoli mengi bila ya kujali kuwa aliyemfunga KMC ni Nani na ana ubora gani??
Maoni Yangu : kwa Sasa ligi ni ngumu kila mechi ni Fainali hakuna Mambo ya kutazama historia na kuingia na matokeo mfukoni.
Tatizo lipo kwa wachezaji (saikolojia Yao) waliingia na matokeo mfukoni wakiamini KMC atafungwa tu Tena nyingi Kama walivyofanya Yanga na Azam.
Nimetazama mpira mpaka nikajiuliza mbona kila mchezaji anataka kufunga? Papala zinakua Nyingi sana kisaikolojia walishaambiwa kuwa timu ipate magoli mengi na ndiyo maana kila mchezaji anataka kufunga hata Kama ni nafasi ya kupasia anataka afunge tu.
Nilimsikia msemaji wa Simba sc (Ahmedy Ally) akisema "Azam Fc wameifunga KMC goli tano na wapinzani wetu wameifunga goli tano Ila sisi tuna droo kwa kweli hiyo siyo nzuri"
Hapa Ahmedy Ally alizungumza kishabiki na kusahau kuwa Yanga Sc ni Bora na Azam Fc ni bora kuanzia beki, viungo na washambuliaji Azama na Yanga Sc kwa Sasa Wana Vikosi Bora.
Ukipiga hesabu za kihistoria Fulani kamfunga goli tano usipoangalia utashuka daraja maana mpira haupo hivyo na ndicho kilichotokea kwa Simba SC waliamini KMC watamfunga tu maana alishafungwa magoli mengi bila ya kujali kuwa aliyemfunga KMC ni Nani na ana ubora gani??
Maoni Yangu : kwa Sasa ligi ni ngumu kila mechi ni Fainali hakuna Mambo ya kutazama historia na kuingia na matokeo mfukoni.