Anonymous
Senior Member
- Apr 6, 2006
- 118
- 339
Watu watatu waliokuwa wakimfuatilia mgombea ubunge jimbo la Vunjo kwa tiketi ya NCCR-Mageuzi, Ndg. James Mbatia wakiwa na gari aina ya Toyota Prado namba DFP 788 wamekamatwa na Jeshi la Polisi mjini Moshi jana saa 10 alasiri eneo la KDC baada ya Polisi kufukuzana na gari hilo na kufanikiwa kulidhibiti (block).
Mmoja wao alifanikiwa kukimbia baada ya kuona wamedhibitiwa lakini wawili walidhibitiwa na Jeshi la P
Watu hao waliokuwa wakijitambulisha maeneo mengi kuwa wao ni Usalama wa Taifa na wakati mwingine wakidai wao Askari wa Jeshi la Polisi hatimaye baada ya kukamatwa na kuhojiwa imedaiwa ni watu kutoka kitengo cha ‘Maadili na Usalama’ ndani ya CCM kutoka ofisi ndogo ya CCM Lumumba.
Baada ya kupekuliwa, watu hao walikutwa na nambari za magari tofauti tofauti na silaha mbalimbali zikiwamo koleo zinazodaiwa kutumika kuwatesa makada wa upinzani waliotekwa Vunjo na Moshi Vijijini na kuzua taharuki mkoani Kilimanjaro.
Wanaendelea kushikiliwa Central Police mjini Moshi.
Hawa ndio walioweza kukamatwa
Hizi ni nambari za magari zilizokutwa ndani ya gari lao
Mbatia akiongelea vitendo hivi 👇🏾
Ilivyotokea: Mnamo majira ya saa 10 za jioni kulitoka kurupushani katika ya msafara wa James Mbatia pamoja na watu waliokuwa na gari hilo hali iliyozua taharuki kubwa. Nguvu ya ziada iliongezwa na Jeshi la Polisi kituo kidogo cha Himo na kuanza kulifukuza gari hilo ili kuli-block jambo ambalo pia halikufua dafu kwani almanusura gari hilo liligonge gari la OCS wa Kituo cha Polisi Himo.
Polisi walilazimika kuongeza nguvu zaidi ya magari kutoka Kituo Kikuu cha Polisi Moshi - Kilimanjaro ndipo walipofanikiwa kulizuia gari hilo kwa kuziba barabara zote na kuwakamata watuhumiwa wawili kati ya watatu ambapo mmoja alifanikiwa kutoroka kwa kuruka Dirishani. Baada ya purukushani hizo zilizodumu kwa zaidi ya saa 2 ndipo gari hilo lilikutwa na Mapanga, Marungu, Sime, Mikuki, Jambia na plate number nne za magari tofauti.
Watuhumiwa wamejitetea kwamba wao ni usalama wa Taifa hata hivyo Idara hiyo imewakana haiwafahamu.
=====
Baadhi ya matukio wanayohusishwa nayo:
Septemba 9, 2020:
Watu wasiojulikana wakiwa na gari aina ya Toyota Prado lenye namba za DFP wanadaiwa kuwateka nyara makada wawili wa NCCR-Mageuzi jimbo la Vunjo kisha kuwatesa na mmoja kukatwa sikio lake la kulia.
Taarifa za uhakika zimewataja makada hao kuwa ni Yolanda Lyimo ambaye ni mgombea udiwani viti maalum na Deogratius Mosha ambaye ni kampeni Meneja wa mgombea udiwani kata ya Kilema kati, Gibras Riwa.
Vyanzo vya habari vinadai kuwa tukio hilo lilitokea juzi kati ya saa 12:00 na 1:00 usiku katika kijiji cha Mkyashi huko kata ya Kilema ambapo watu wasiojulikana, wakiwa na bunduki waliwateka makada hao.
Inadaiwa kuwa watu hao waliokuwa na gari aina ya Prado, walijitambulisha kwa makada hao waliokuwa na mazungumzo yao binfasi na watu wengine watatu, kwamba wao ni maofisa wa Jeshi la Polisi.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, waliwachukua Yolanda na Deogratius na kuwaamuru wapakie kwenye gari kuwa wanakwenda kufanya nao mahojiano, lakini badala yake walilazwa kwenye gari hiyo.
Baadae katika eneo ambao hawakulitambua, watu hao walianza kuwatesa kwa kuwapiga ambapo Deogratius alikatwa sikio lake la kulia na baadae kutelekezwa kwenye pori lenye miba katika msitu Ghona.
Hata hivyo, waliweza kujikongoja umbali wa kati ya kilometa 3 hadi 4 hadi kijiji cha Ghona ambapo wananchi waliweza kuwapa msaada ikiwamo kupiga simu polisi Himo, ambao walifika na kuwachukua.
Yolanda kwa sasa ni mgombea udiwani viti maalum na katika mchakato wa uchaguzi mkuu 2020, alishiriki kura za maoni CCM kuwania Udiwani kata ya Kilema Kati lakini hakuteuliwa ndipo akajiunga na NCCR-Mageuzi.
Pia ni Diwani aliyemaliza muda wake katika kata hiyo hiyo lakini kupitia chama cha Tanzania Labour Party (TLP) wakati Deogratius yeye ni kampeni Meneja wa mgombea udiwani kata ya Kilema Kati
>>>>>
Tarehe 6 Oktoba 2020:
Vitendo vya kiharamia vya kuteka makada wa vyama, kuwatesa na hata kuwaua vimeanza kutikisa nchi baada ya makada wawili wa CHADEMA Wilaya ya Hai, kutekwa na kufanyiwa mateso makubwa.
Miongoni mwa mateso hayo ni kuingiziwa mti sehemu ya haja kubwa, kuminywa korodani kwa koleo, kujaribu kuwang’oa meno kwa koleo, mmoja kukatwa sikio na wote kuteswa kwa kupigwa na shoti ya umeme.
Makada hao walitekwa kata ya Narumu juzi na watu waliokuwa na magari ya kiraia matatu wakidaiwa kuwa na bunduki mbili na bastola moja, na baada ya mateso hayo, waliwatupa maeneo tofauti wilayani Arumeru.
>>>>>
Matukio wanayohusishwa watu ni mengi, tusubiri kuona mwisho wao utakuwaje
Mmoja wao alifanikiwa kukimbia baada ya kuona wamedhibitiwa lakini wawili walidhibitiwa na Jeshi la P
Watu hao waliokuwa wakijitambulisha maeneo mengi kuwa wao ni Usalama wa Taifa na wakati mwingine wakidai wao Askari wa Jeshi la Polisi hatimaye baada ya kukamatwa na kuhojiwa imedaiwa ni watu kutoka kitengo cha ‘Maadili na Usalama’ ndani ya CCM kutoka ofisi ndogo ya CCM Lumumba.
Baada ya kupekuliwa, watu hao walikutwa na nambari za magari tofauti tofauti na silaha mbalimbali zikiwamo koleo zinazodaiwa kutumika kuwatesa makada wa upinzani waliotekwa Vunjo na Moshi Vijijini na kuzua taharuki mkoani Kilimanjaro.
Wanaendelea kushikiliwa Central Police mjini Moshi.
Hawa ndio walioweza kukamatwa
Hizi ni nambari za magari zilizokutwa ndani ya gari lao
Mbatia akiongelea vitendo hivi 👇🏾
Ilivyotokea: Mnamo majira ya saa 10 za jioni kulitoka kurupushani katika ya msafara wa James Mbatia pamoja na watu waliokuwa na gari hilo hali iliyozua taharuki kubwa. Nguvu ya ziada iliongezwa na Jeshi la Polisi kituo kidogo cha Himo na kuanza kulifukuza gari hilo ili kuli-block jambo ambalo pia halikufua dafu kwani almanusura gari hilo liligonge gari la OCS wa Kituo cha Polisi Himo.
Polisi walilazimika kuongeza nguvu zaidi ya magari kutoka Kituo Kikuu cha Polisi Moshi - Kilimanjaro ndipo walipofanikiwa kulizuia gari hilo kwa kuziba barabara zote na kuwakamata watuhumiwa wawili kati ya watatu ambapo mmoja alifanikiwa kutoroka kwa kuruka Dirishani. Baada ya purukushani hizo zilizodumu kwa zaidi ya saa 2 ndipo gari hilo lilikutwa na Mapanga, Marungu, Sime, Mikuki, Jambia na plate number nne za magari tofauti.
Watuhumiwa wamejitetea kwamba wao ni usalama wa Taifa hata hivyo Idara hiyo imewakana haiwafahamu.
=====
Baadhi ya matukio wanayohusishwa nayo:
Septemba 9, 2020:
Watu wasiojulikana wakiwa na gari aina ya Toyota Prado lenye namba za DFP wanadaiwa kuwateka nyara makada wawili wa NCCR-Mageuzi jimbo la Vunjo kisha kuwatesa na mmoja kukatwa sikio lake la kulia.
Taarifa za uhakika zimewataja makada hao kuwa ni Yolanda Lyimo ambaye ni mgombea udiwani viti maalum na Deogratius Mosha ambaye ni kampeni Meneja wa mgombea udiwani kata ya Kilema kati, Gibras Riwa.
Vyanzo vya habari vinadai kuwa tukio hilo lilitokea juzi kati ya saa 12:00 na 1:00 usiku katika kijiji cha Mkyashi huko kata ya Kilema ambapo watu wasiojulikana, wakiwa na bunduki waliwateka makada hao.
Inadaiwa kuwa watu hao waliokuwa na gari aina ya Prado, walijitambulisha kwa makada hao waliokuwa na mazungumzo yao binfasi na watu wengine watatu, kwamba wao ni maofisa wa Jeshi la Polisi.
Kwa mujibu wa taarifa hizo, waliwachukua Yolanda na Deogratius na kuwaamuru wapakie kwenye gari kuwa wanakwenda kufanya nao mahojiano, lakini badala yake walilazwa kwenye gari hiyo.
Baadae katika eneo ambao hawakulitambua, watu hao walianza kuwatesa kwa kuwapiga ambapo Deogratius alikatwa sikio lake la kulia na baadae kutelekezwa kwenye pori lenye miba katika msitu Ghona.
Hata hivyo, waliweza kujikongoja umbali wa kati ya kilometa 3 hadi 4 hadi kijiji cha Ghona ambapo wananchi waliweza kuwapa msaada ikiwamo kupiga simu polisi Himo, ambao walifika na kuwachukua.
Yolanda kwa sasa ni mgombea udiwani viti maalum na katika mchakato wa uchaguzi mkuu 2020, alishiriki kura za maoni CCM kuwania Udiwani kata ya Kilema Kati lakini hakuteuliwa ndipo akajiunga na NCCR-Mageuzi.
Pia ni Diwani aliyemaliza muda wake katika kata hiyo hiyo lakini kupitia chama cha Tanzania Labour Party (TLP) wakati Deogratius yeye ni kampeni Meneja wa mgombea udiwani kata ya Kilema Kati
>>>>>
Tarehe 6 Oktoba 2020:
Vitendo vya kiharamia vya kuteka makada wa vyama, kuwatesa na hata kuwaua vimeanza kutikisa nchi baada ya makada wawili wa CHADEMA Wilaya ya Hai, kutekwa na kufanyiwa mateso makubwa.
Miongoni mwa mateso hayo ni kuingiziwa mti sehemu ya haja kubwa, kuminywa korodani kwa koleo, kujaribu kuwang’oa meno kwa koleo, mmoja kukatwa sikio na wote kuteswa kwa kupigwa na shoti ya umeme.
Makada hao walitekwa kata ya Narumu juzi na watu waliokuwa na magari ya kiraia matatu wakidaiwa kuwa na bunduki mbili na bastola moja, na baada ya mateso hayo, waliwatupa maeneo tofauti wilayani Arumeru.
>>>>>
Matukio wanayohusishwa watu ni mengi, tusubiri kuona mwisho wao utakuwaje