Kilimo cha matikiti maji (watermelon): Ushauri na Masoko

Ukisoma vizuri maoni ya watu inaonesha ni sukari f1, kwa uzoefu wangu ni keshavu kutoka India.

Kwa imani yangu ni kwamba ukitoa huduma vizuri mbegu yeyote ya hybrid inatoa matunda makubwa, mimi huwa natumia sugar queen f1 huwa napata matunda kwa saizi ya ndoo ya Lita kumi mengi tu.

Japokuwa kibiashara matunda makubwa yanavutia wateja lakini hayanunuliwi kwa sababu ya bei, matunda ya saizi ya kawaida yanauzika kirahisi maana hata mwenye 500 anapata tunda kuliko hayo makubwa yanabana wateja kwenye bei.
 
Kuna mbegu inaitwa Princess F1 Ni ya kampuni ya Kibo Seeds, Ina sifa hiyo.
 
Ninaomba mniadd kwenye group la whatsap la kilimo cha tikiti
0762345990
 
Noamba kuuliza - eti ni lazima kumwagia matikiti kila siku?

Je nkimwagia leo alafu baada ya siku mbili ardhi ikawa bado ina unyevu kwa chini nkifukua mchanga, natakiwa lazima nimwagie ili ardhi ilowe?

Mwenye utaalamu please anisaidie ni jinsi gani mmea huu (na mimea mingine) inakunywa maji? Imezoeleka kumwaga maji mengi sana kwenye kilimo cha tikiti, ningependa kujua kitaalamu kama ni kweli mmea wa tikiti unahitaji maji MENGI sana
 
Naomba mni add ktk group la kilimo cha matikiti au matunda

#0746582997
 
Kwangu mimi namwagilia kila siku.
 
Kwa tulioko dar es salaam, na tunaopenda kwenda sokoni wenyewe hivi Kuna soko lingine zuri kwa kuzuia matikiti tofauti na Temeke stereo. ?
 
Je unahitaji kulima mahindi na hauna muda wa kusimamia? Au unataka upate mavuno mengi zaidi? Njoo ofisini kwetu.

Ofisi ya YAD yenye wataalamu wabobezi wa kilimo sasa inakuletea mpango wa kusimamia shughuli zote za shambani. Mkulima utatukabidhi shughuli zako pale shambani kwako sisi tutafanya kila kitu kwa utaalamu zaidi na kukukabidhi mazao yako yakiwa yamekomaa.

Gharama zetu ni nafuu sana na tunakuhakikishia kwa ekari moja kuvuna mahindi zaidi ya gunia 30. Usihangaike sasa, sisi tupo kwa ajili yako, Kwa Wale ambao hawana mashamba tutakuwezesha kupata mashamba ya kukodi kwa elfu 40 tu na mashamba ya kununua kwa elfu 60 tu hata ukihitaji ekari 100 za kununua utazipata kwa bei hiyo hiyo.

Kwa maelezo zaidi fika ofisini kwetu.
Jengo la NSSF SONGEA
Ghorofa ya 3 chumba no. 317
Simu. 0621133117
 
Nini siri ya kutoa ndonga mkuu, daily watering? frequent foliar feeding? Mbolea au?
 
Kwa kawaida, tikiti maji zinahitajika kama matunda. Lakini, tunapaswa kufikiria juu ya bidhaa zingine ambazo zinaweza kuzalishwa kwa kutumia tikiti maji.

Je! Ni bidhaa ipi ya tikiti maji inayohitajika zaidi? Ninafikiria juisi ya tikiti maji. Vipi kuhusu soko?
 
Shukrani kwa uchambuzi huo makini, lakini vipi kilimo hiki kinaweza kufanyika katika maeneo yenye miinuko na baridi kali, maeneo km ya nyanda za juu kusini au na katika safu milima ya usambara?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…