Kilimo chetu cha kumnyonya mkulima leo kinatutokea puani

Kilimo chetu cha kumnyonya mkulima leo kinatutokea puani

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Kwa miaka sitini ya uhuru mkulima hajawahi pata bei stahiki ya mazao yake. Haya tunayoyaona leo ni matokeo ya kumnyonya. Watu waliacha kulima kahawa na chai sababu ya kunyonywa. Lakini sababu hao si mazao ya chakula hatukuona athari zake.

Lakini ukweli hata kwenye mahindi na mazao mengine ya chakula watu wameacha kulima. Kwanini ulime wakati kununua ni bei rahisi zaidi? Bora bodaboda au ukauze karanga kuliko kulima.

Matokeo yake hakuna anayewekeza kulima mashamba makubwa, kutumia matrekta au kulima kwa umwagiliaji licha ya kuwa na maji tele.

Tunachoona leo ni matokeo ya watu kukimbia na kuacha kuwekeza kwenye kilimo sababu ya bei za unyonyaji. Dhuluma hailipi.
 
Ukweli mtupu umenena

Tubadilishe sera kandamizi
 
Kati ya watu ambao Serikali imekuwa ikiwaumiza sana, ni wakulima.

Mkulima analima kwa nguvu zake, mbolea anatafuta mwenyewe, anapalilia, anavuna, anataka kuuza, Serikali inakuja na matamko ya kipuuzi, 'kutokana na uhaba wa chakula, hairuhusiwi kuuza nje'! Ala! Anampangia kwani ulisaidiana naye kulima? Tangu lini mkulima amepewa jukumu la kuwatumza wananchi wasio wakulima? Hivi Twiga cement, ALAF au Bakhresa, huwa wanapangiwa pa kuuza bidhaa zao?

Wakulima waachwe wawe huru. Serikali ambayo ina wajibu wa kuhakikisha nchi ina akiba ya chakula cha kutosha, oende kwa wakulima ikanunue mazao inayoyahitaji kwa kushindana na wanunuzi wengine.

Mimi siyo mkulima, nipo tayari kununua chakula kwa bei yoyote ya soko. Nitaumia, lakini kamwe siwezi kuunga mkono fikra zozote za kumzuia mkulima kuwa na uhuru wa kuyauza mazao yake anakotaka.

Mkulima wa Tanzania asiyepewa ruzuku kufidia gharama zake, ni halali kwake kutafuta soko lenye kutoa bei nzuri.
 
For the first time tangu kuumba kwa hii dunia mkulima leo hii anauza gunia la mpunga la kg 150 kwa tshs 170k.
Jamani wakulima mwaka wao huu. Kg 1 ya mchele kwa bei ya chini ni shs 2100 hii ni kwa mkulima.
 
For the first time tangu kuumba kwa hii dunia mkulima leo hii anauza gunia la mpunga la kg 150 kwa tshs 170k.
Jamani wakulima mwaka wao huu. Kg 1 ya mchele kwa bei ya chini ni shs 2100 hii ni kwa mkulima.
Ni jambo zuri kwa kilimo chetu. Kufungfunga mipaka ni kuleta njaa.
 
Kati ya watu ambao Serikali imekuwa ikiwaumiza sana, ni wakulima.

Mkulima analima kwa nguvu zake, mbolea anatafuta mwenyewe, anapalilia, anavuna, anataka kuuza, Serikali inakuja na matamko ya kipuuzi, 'kutokana na uhaba wa chakula, hairuhusiwi kuuza nje'! Ala! Anampangia kwani ulisaidiana naye kulima? Tangu lini mkulima amepewa jukumu la kuwatumza wananchi wasio wakulima? Hivi Twiga cement, ALAF au Bakhresa, huwa wanapangiwa pa kuuza bidhaa zao?

Wakulima waachwe wawe huru. Serikali ambayo ina wajibu wa kuhakikisha nchi ina akiba ya chakula cha kutosha, oende kwa wakulima ikanunue mazao inayoyahitaji kwa kushindana na wanunuzi wengine.

Mimi siyo mkulima, nipo tayari kununua chakula kwa bei yoyote ya soko. Nitaumia, lakini kamwe siwezi kuunga mkono fikra zozote za kumzuia mkulima kuwa na uhuru wa kuyauza mazao yake anakotaka.

Mkulima wa Tanzania asiyepewa ruzuku kufidia gharama zake, ni halali kwake kutafuta soko lenye kutoa bei nzuri.
Umeongea Kwa hisia sana naona unaifahamu vizuri siasa ya nchi yetu kama hawa viongozi wangechukua japo nusu ya mawazo yako haya walahi Tanzania ingeziba pengo la upungufu wa mazao ya chakula uliosababishwa na mzozo wa Ukraine na Russia tungepiga hela sana.
 
HAPA WENGI MNAONGEA HAMPO MASHAMBANI MKULIMA AJAWAHI FAIDIKA WANAOFAIDIKA SAIVI NI MADALALI NA WALE WENYE MAGHALA MAKUBWA WAKULIMA WALISHAUZA ZAMANI TENA KWA WENGINE SAIVI WAO NDO WANANUNUA
 
Kwa miaka sitini ya uhuru mkulima hajawahi pata bei stahiki ya mazao yake. Haya tunayoyaona leo ni matokeo ya kumnyonya. Watu waliacha kulima kahawa na chai sababu ya kunyonywa. Lakini sababu hao si mazao ya chakula hatukuona athari zake.

Lakini ukweli hata kwenye mahindi na mazao mengine ya chakula watu wameacha kulima. Kwanini ulime wakati kununua ni bei rahisi zaidi? Bora bodaboda au ukauze karanga kuliko kulima.

Matokeo yake hakuna anayewekeza kulima mashamba makubwa, kutumia matrekta au kulima kwa umwagiliaji licha ya kuwa na maji tele.

Tunachoona leo ni matokeo ya watu kukimbia na kuacha kuwekeza kwenye kilimo sababu ya bei za unyonyaji. Dhuluma hailipi.
Hata mimi niliacha kulima kwa sababu ya bei ndogo ya mazao lkn sasa nawaza kurudi
 
Kwa miaka sitini ya uhuru mkulima hajawahi pata bei stahiki ya mazao yake. Haya tunayoyaona leo ni matokeo ya kumnyonya. Watu waliacha kulima kahawa na chai sababu ya kunyonywa. Lakini sababu hao si mazao ya chakula hatukuona athari zake.

Lakini ukweli hata kwenye mahindi na mazao mengine ya chakula watu wameacha kulima. Kwanini ulime wakati kununua ni bei rahisi zaidi? Bora bodaboda au ukauze karanga kuliko kulima.

Matokeo yake hakuna anayewekeza kulima mashamba makubwa, kutumia matrekta au kulima kwa umwagiliaji licha ya kuwa na maji tele.

Tunachoona leo ni matokeo ya watu kukimbia na kuacha kuwekeza kwenye kilimo sababu ya bei za unyonyaji. Dhuluma hailipi.
Wewe ni miongoni mwa watz wachache wenyekutumia akili zao vizuri.Big up mkuu!Bandiko fupi tamu.

Sent from my SM-G532F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom