Kuna njia nzuri tunayoweza kuifanya,ili kwa pamoja tufanikiwe, hasa kwa wanaotaka kulima (large scale), nina maana kuanzia eka 100 na kwenda mbele, tuunganishe nguvu ili tupate eneo moja kubwa bure kisha tuligawane kwa kilimo, tukifaulu hapo tutakuwa tuko mahali pazuri pa kuibana serikali yetu itusaidie,sisemi tuunde kikundi hapana. Wengi wanashindwa kupata ardhi kubwa kwa sababu wanaogopa kuanzisha mashamba makubwa porini.
Mwaka huu nilipata fursa ya kutembelea mapori fulani huko Moro, yako barabarani/reli,yana maji na ardhi ina rutuba sana haina mwenyewe. Bado natafuta zaidi ili nikipata pori la ndoto zangu nitajichimbia huko nichape kazi kwa kulima na kufuga.