Kilimo: Ungependa serikali ya awamu ya tano ifanye nini kwenye hii sekta?

Kilimo: Ungependa serikali ya awamu ya tano ifanye nini kwenye hii sekta?

Red Giant

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2012
Posts
15,657
Reaction score
20,967
Wadau wa kilimo hebu tuseme tunataka nini itufanyie serikali ya awamu ya tano. ni matatizo gani itutatulie na mambo gani ituboreshee? Mimi binafsi nahitaji kilio changu cha kila siku hapa chini kisikilizwe na kufanyiwa kazi.

Vijana na watu wengi hawapendi kulima kwa sababu mbili. Kwanza ni kukosekana kwa masoko ya uhakika wa mazao ya kilimo na bei kuwa ya chini. haya yote yanasababishwa na serikali kuzuia watu kuuza mazao nje ya nchi wakati uzalishaji na potential ya kuzalisha ni kubwa sana.

Ninaweza sema Tanzani kuna deflation ya bei ya chakula. Deflation ina madhara yake, kwanza inapunguza uzalishaji na kusababisha unemployment. Deflation ya chakula inanufaisha wachache na kuumiza wakulima ambao ndiyo wengi. Imekuwa nafuu kununua kuliko kulima. Hii inamaanisha wakulima huzalisha kwa hasara.

Je ni kweli kufungua mipaka kutaleta njaa?. Nchi yetu inazalisha ziada ya msosi pia naamini inaweza kuzalisha hata mara mia ya kiwango cha sasa kwa ardhi na maji tuliyo nayo. Hivyo kufungua mipaka kutaongeza uwekezaji kwenye kilimo, kutaongeza uzalishaji na matokeo yake ajira kuongezeka. Pia vijana wengi wataanza kujiajiri na kilimo maana kitakuwa kinalipa.

Sasa kwanini wanazuia? Kama tunavyojua mabadiliko ya kisiasa huanziaga mijini. Serikali kwa kuona hilo huamua kuwapumbaza watu wa mjini kwa kuhakikisha bei ya chakula ipo chini na njia moja ni kufunga mipaka. Wanafanya hivyo kwa expense ya 80% ya watanzania. Hata hivyo watu wengiwamjini pia hulima au wangependa kuwekeza kwenye kilimo. So hii strategy inatutafuna sote.

Ili kukabiliana na ajira serikali inatakiwa iruhusu uuzaji wa mazao nje, itatengeneza ajira nyingi sana. Na siyo kufungua kinafiki. Kufungua harafu kuweka kodi ya kuexport kubwa ili kudiscourage watu.
 
Serikali inayokuja, isimamie vyema mchakato wa uanzishwaj wa masoko ya bidhaa (commodity exchange) ambao umeshaanza, na Mh rais amesign muswada wake tayar.

Kama kukiwa na usimamiz mzuri, commodity exchange itasaidia wakulima sana kupata masoko ya uhakika ya bidhaa zao na bei za ushindani
 
watendaji kazi wa mashambani kuwa serious kwenye vibarua vyao na kuipenda kazi yao.

mazao ya biashara yanayouzwa nje bei yake kuboreshwa na kusimamiwa na serikali sio kuwaachia matajiri wachache waamue.
 
1. Benki ya kilimo ifanye kazi kwa ufanisi.
2. Bei nzuri ya mazao sokoni
3. Kuondoa madalali sokoni
4. Urahisi na wepesi wa upatikanaji wa pembejeo
5. Viwanda vya usindikaji wa mazao vifufuliwe.
 
Ijenge mabwawa makubwa ili wakulima walime muda wote,irrigation system
 
- Hiyo benki ya wakulima ipewe mtaji mkubwa kukidhi mahitaji yaliyopo
- Hati za ardhi zitolewe bila mizengwe ili sisi wakulima tukopesheke
- Viwanda vidogo vya kusindika sasa vijengwe vijijini, umeme upo
- Somo la kilimo lirudishwe shuleni
- Tuache kuuza mazao ghafi
 
Mada ya kuangaliwa kwa makini sana hii.
Umeongea jambo la msingi mtoa hoja
 
- Hiyo benki ya wakulima ipewe mtaji mkubwa kukidhi mahitaji yaliyopo
- Hati za ardhi zitolewe bila mizengwe ili sisi wakulima tukopesheke
- Viwanda vidogo vya kusindika sasa vijengwe vijijini, umeme upo
- Somo la kilimo lirudishwe shuleni
- Tuache kuuza mazao ghafi

Ikifanya hayo yote itakuwa imecheza km Pelle.
 
Ktk kilimo kunamengi yakufanya ila Mimi ningependa serekali ikawekawataalamu wakilimo wengi ilikuwakumpatiaa elimu mkulima mdogo
 
Bila kuwa na viongozi wanajua umhimu wa viwango katila masoko hasa ya nje na namna ya kukidhi viwango hivyo, utafutaji wa masoko na ushawishi wa makusudi tutabaki kuwa wasindikizaji tu kwenye Kilimo!?
 
Wadau wa kilimo hebu tuseme tunataka nini itufanyie serikali ya awamu ya tano. ni matatizo gani itutatulie na mambo gani ituboreshee? Mimi binafsi nahitaji kilio changu cha kila siku hapa chini kisikilizwe na kufanyiwa kazi.

Vijana na watu wengi hawapendi kulima kwa sababu mbili. Kwanza ni kukosekana kwa masoko ya uhakika wa mazao ya kilimo na bei kuwa ya chini. haya yote yanasababishwa na serikali kuzuia watu kuuza mazao nje ya nchi wakati uzalishaji na potential ya kuzalisha ni kubwa sana.

Ninaweza sema Tanzani kuna deflation ya bei ya chakula. Deflation ina madhara yake, kwanza inapunguza uzalishaji na kusababisha unemployment. Deflation ya chakula inanufaisha wachache na kuumiza wakulima ambao ndiyo wengi. Imekuwa nafuu kununua kuliko kulima. Hii inamaanisha wakulima huzalisha kwa hasara.

Je ni kweli kufungua mipaka kutaleta njaa?. Nchi yetu inazalisha ziada ya msosi pia naamini inaweza kuzalisha hata mara mia ya kiwango cha sasa kwa ardhi na maji tuliyo nayo. Hivyo kufungua mipaka kutaongeza uwekezaji kwenye kilimo, kutaongeza uzalishaji na matokeo yake ajira kuongezeka. Pia vijana wengi wataanza kujiajiri na kilimo maana kitakuwa kinalipa.

Sasa kwanini wanazuia? Kama tunavyojua mabadiliko ya kisiasa huanziaga mijini. Serikali kwa kuona hilo huamua kuwapumbaza watu wa mjini kwa kuhakikisha bei ya chakula ipo chini na njia moja ni kufunga mipaka. Wanafanya hivyo kwa expense ya 80% ya watanzania. Hata hivyo watu wengiwamjini pia hulima au wangependa kuwekeza kwenye kilimo. So hii strategy inatutafuna sote.

Ili kukabiliana na ajira serikali inatakiwa iruhusu uuzaji wa mazao nje, itatengeneza ajira nyingi sana. Na siyo kufungua kinafiki. Kufungua harafu kuweka kodi ya kuexport kubwa ili kudiscourage watu.

Mkuu Serikali mbona haijazuia kuuza mazao nje.
 
Mkuu Serikali mbona haijazuia kuuza mazao nje.
mkuu iliruhusu baada ya ya kuona haiwezi kununua mazao yote. lakini ukilima unakua hujui kama wataruhususu au laa. hamna mtu anataka kucheza hiyo kamari.
 
watendaji kazi wa mashambani kuwa serious kwenye vibarua vyao na kuipenda kazi yao.

mazao ya biashara yanayouzwa nje bei yake kuboreshwa na kusimamiwa na serikali sio kuwaachia matajiri wachache waamue.
umenena vema mkuu. si matajiri tuu hata bodi za mazao ziangaaliwe, zimekuwa wanyonyajji wakubwa wa wakulima.
 
- Hiyo benki ya wakulima ipewe mtaji mkubwa kukidhi mahitaji yaliyopo
- Hati za ardhi zitolewe bila mizengwe ili sisi wakulima tukopesheke
- Viwanda vidogo vya kusindika sasa vijengwe vijijini, umeme upo
- Somo la kilimo lirudishwe shuleni
- Tuache kuuza mazao ghafi
umemaliza yote mkuu. na sisi wakulima tunataka tukopesheke na hiyo benki ya wakulima iwe ya wote Pasco.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom