Kilio cha umma juu ya utekaji kinazidi kupamba moto, serikali iwe makini cheche zilichoma msitu!

Kilio cha umma juu ya utekaji kinazidi kupamba moto, serikali iwe makini cheche zilichoma msitu!

Superbug

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2018
Posts
13,864
Reaction score
35,079
Ukiangalia kwa jicho la ndani utaona kuna mawazo kinzani juu ya hili swala la utekaji.

Serikali inasema hilo jambo halipo na watu wanajifanyisha tu maigizo ila utekaji haupo. Rejea kauli ya Rais.

Ukija bungeni spika anazuia jambo hili lisijadiliwe bungeni hata kinafiki tu ili kufunika kombe mwanaharamu apite.

Unazuiaje mjadala muhimu kama huu kujadiliwa wakati ni jambo linalohusu usalama wa wananchi wako? Walipa kodi wako?

Ukija kwa polisi na vyombo vya dola hawa ndio wananyooshewa vidole na wananchi kama wahusika wakuu wa biashara hii haramu ya kutekana.

Jambo la ajabu ni kwamba utekaji upo na watekwaji wapo tena wengine wanawataja wazi kama dola ndio imehusika na madhila waliyoyapata.

Rai yangu kwa serikali isifanye kama mbuni afanyavyo kujificha kichwa kwenye mchanga akidhani haonekani ilhali mwili mzima uko nje. Serikali kuzuia mjadala huu au kuubeza sio sawa.

Tukae tukijua cheche zilichoma msitu mkubwa! Je, bado Tanzania ni kisiwa cha amani kama tunavyojinasibu?
 
Ukiangalia kwa jicho la ndani utaona kuna mawazo kinzani juu ya hili swala la utekaji.
Serikali inasema hilo jambo halipo na watu wanajifanyisha tu maigizo ila utekaji haupo. Rejea kauli ya rais.
Ukija bungeni spika anazuia jambo hili lisijadiliwe bungeni hata kinafiki tu ili kufunika kombe mwanaharamu apite. Unazuiaje mjadala muhimu kama huu kujadiliwa wakati ni jambo linalohusu usalama wa wananchi wako? Walipa kodi wako?
Ukija kwa polisi na vyombo vya dola hawa ndio wananyoshewa vidole na wananchi kama wahusika wakuu wa biashara hii haramu ya kutekana.
Jambo la ajabu ni kwamba utekaji upo na watekwaji wapo tena wengine wanawataja wazi kama dola ndio imehusika na madhila waliyoyapata.
Rai yangu kwa serikali isifanye kama mbuni afanyavyo kujificha kichwa kwenye mchanga akidhani haonekani ilhali mwili mzima uko nje. Serikali kuzuia mjadala huu au kuubeza sio sawa. Tukae tukijua cheche zilichoma msitu mkubwa!
Swali langu je bado Tanzania ni kisiwa cha amani kama tunavyojinasibu?
Mmmh
 
Sheria ya usalama wa taifa kuruhusiwa kuua ndio sasa inafanya kazi kwa haya yanayoendelea. Polisi wanajitahidi kutoa taarifa za vifo kwa waganga wa kienyeji ili kutupoteza maboya, lakini ukweli tunaujua. Spika Tulia ni mmoja wa washiriki wa kutunga sheria hii mbaya ya utekaji na mauaji. Ndio maana anazuia mjadala wa hili jambo, maana yeye anajua fika hii sheria aliyoasisi iko kazini.
 
Sheria ya usalama wa taifa kuruhusiwa kuua ndio sasa inafanya kazi kwa haya yanayoendelea. Polisi wanajitahidi kutoa taarifa za vifo kwa waganga wa kienyeji ili kutupoteza maboya, lakini ukweli tunaujua. Spika Tulia ni mmoja wa washiriki wa kutunga sheria hii mbaya ya utekaji na mauaji. Ndio maana anazuia mjadala wa hili jambo, maana yeye anajua fika hii sheria aliyoasisi iko kazini.
Mara mganga wa Uganda amekutwa na Vichwa😆😆😆
 
Wale wamasai kwa namna walivyoungana na kuandamana bila yeyote kutarajia ni funzo kwa hii serikali kiziwi.
Hivi hakuna namna ya kuiga na kutumia njia hiyo waliyo tumia wamasai au hata njia iliyo badilishwa kidogo kulingana na hali halisi ya swala husika na mahala, ili wananchi sehemu mbali mbali za nchi waweze kufikisha taarifa kwa hawa "viziwi" na ulimwenguni kote?

Hali ya namna hiyo ikienea nchi nzima, hawa wakoloni hawawezi kuizima kwa urahisi.

Matatizo yapo kila mahali, siyo kwa wamasai peke yao.
 
Sheria ya usalama wa taifa kuruhusiwa kuua ndio sasa inafanya kazi kwa haya yanayoendelea. Polisi wanajitahidi kutoa taarifa za vifo kwa waganga wa kienyeji ili kutupoteza maboya, lakini ukweli tunaujua. Spika Tulia ni mmoja wa washiriki wa kutunga sheria hii mbaya ya utekaji na mauaji. Ndio maana anazuia mjadala wa hili jambo, maana yeye anajua fika hii sheria aliyoasisi iko kazini.
Huyo tulia asiyetulia alivyo na uroho wa madarka yumkini anaweza hata kushriki kwenye uhayawani huu wa kuondoa roho za watu alimradi ahakikishiwe kuendelea kuwepo kwenye madaraka.

Tuyakatae mashetani mauaji kwa namna zote ambazo tunaweza.
 
Kutokana na Muendelezo wa matukio mbalimbali ya kiharifu na kikatili nchini, na kwasehemu kubwa washukiwa wakuu kwa mujibu wa wanao report ikisemekana ni vyombo vya ulinzi na usalama. Hivyo ni vema uchunguzi wa kina na hatua stahiki kwa wahusika ili kudhibiti matendo haya ya kiharifu, ikiwemo kuanzisha kwa kikosi maalumu kwaajili kufatilia wahusika wakuu wa matendo haya na upelelezi wa kina na mwisho kutolea ufafanuzi kwa jamii.

Wahanga wa matukio haya ni wanajamii hivyo kutokupata ufafanuzi wa kina kuhusu nini hasa kinachopeleka wimbi la matukio haya yakihusisha hata watoto wadogo . yanajenga chuki na hivyo kutakua kizazi katili ambacho kinaweza kuwa tayari kufanya chochote kutokana na machungu ya kupotelewa na wapendwa wao . inaweza fikia yale ya nchi jirani ya kenya.

Alamusiki!
 
Kwa watanzania hawa ambao ukiwapa kanga wanakupa kura, sahau hiyo kitu
 
Kutokana na Muendelezo wa matukio mbalimbali ya kiharifu na kikatili nchini, na kwasehemu kubwa washukiwa wakuu kwa mujibu wa wanao report ikisemekana ni vyombo vya ulinzi na usalama. Hivyo ni vema uchunguzi wa kina na hatua stahiki kwa wahusika ili kudhibiti matendo haya ya kiharifu, ikiwemo kuanzisha kwa kikosi maalumu kwaajili kufatilia wahusika wakuu wa matendo haya na upelelezi wa kina na mwisho kutolea ufafanuzi kwa jamii.

Wahanga wa matukio haya ni wanajamii hivyo kutokupata ufafanuzi wa kina kuhusu nini hasa kinachopeleka wimbi la matukio haya yakihusisha hata watoto wadogo . yanajenga chuki na hivyo kutakua kizazi katili ambacho kinaweza kuwa tayari kufanya chochote kutokana na machungu ya kupotelewa na wapendwa wao . inaweza fikia yale ya nchi jirani ya kenya.

Alamusiki!
True
P
 
Kama Chadema wataacha ujinga nchi hizi kutakuwa na siasa za amani, Samia amejaribu kufanya kila kitu kiwe cha kidemokrasia ila wapuuzi hawa wanaleta ujinga

USSR
 
Ukweli mchungu sana huu, Very soon kuna chama kitaishi kwa mashaka, DHAMBI ni mbaya
 
Yalitokea tukasema na bado yanaendelea kutokea tunaoipenda Tanzania tunaumia sana ukiangalia mbali ni kama tutarithisha wenetu chaotic state.😭😭😭😭
 
Back
Top Bottom