Kilio cha wakulima: Madalali wanatunyonya, hawalipi kodi, ni watu wabaya

Kilio cha wakulima: Madalali wanatunyonya, hawalipi kodi, ni watu wabaya

illegal migrant

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2013
Posts
1,277
Reaction score
1,121
Kweli jamani kila mtu anatakiwa atafute riziki kihalali, ila vitu vingine vinaudhi, vinaumiza, niliamua kuwa mkulima kwa lengo la kujiongezea kipato, nikaamua kushirikiana na mzazi wangu aliyeko huko kijijini, tulianza kilimo cha viazi kwa kuanzia nilianza na hekari tano. Baada kulima kwa muda, mazao yakawa tayari kwa ajili ya kuvuna, wakulima wenzetu walituambia kwamba tusipate tabu ya kuvuna kwani kuna madalali huwa wanakuja wanachagua kisha wanaleta wateja ambao huvuna wenyewe.

Nikaona ni Jambo la kheri tuliwasiliana na dalali ambaye alituahidi siku ya kuja na wakulima wote tukawa tunamsubiri, mara nikaona kigari aina ya Paso kinakuja shambani kimeandikwa “wajinga ndio waliwao” akashuka pande la mtu suruali amevalia tumboni, tukatambulishwa kuwa jamaa ndiye dalali wakulima akiwemo mzazi wangu wanamnyenyekea utadhani nini sijui, kumbe yule bwana jukumu lake kukagua mazao shambani kisha anapanga bei, na ukitofautiana naye utapata wakati mgumu kuuza mazao yako kwani atawaeleza madalali wengine pia kwani wana mtandao.

Jamaa alikuja kwenye shamba letu wakati tunasubiri “ofa” jamaa akachukua panga na kuanza kufukua huku akisema “hamna kitu hapa chelema Tupu hizi, hapa labda niwape laki nane” nikamwambia hiyo hailipi akasema kama hailipi, hakuna mtu atatununua labda tukale wenyewe. Nikamuuliza, unataka kununua kwa lazima na kwa bei unayoitaka? Akajibu akasema yeye ndio don kijijini pale tulichukuana upepo, ukizingatia tabu anazopata mkulima halafu jitu levi tu linakuja na kuanza kutoa bei anazotaka na kwa lugha ya kebehi, aliinua mkono kwa lengo la kunipiga kibao nilimpiga Ngumi nyingi mfululizo.

Imebidi ahairishe zoezi la kukebehi na kulangua mazao. Wamesema atakuja tena Jumamosi ijayo nimemwambia mama tuelekee mjini kwani anaweza kuwa amejihami 😁 kilio cha wakulima, madalali wanatunyonya, hawalipi kodi ni wabaya.
 
Niligoma kuuza mazao yangu Stakabadhi ghalani kwa huu uhuni
 
Mazao mazuri ni nafaka. Unaweza kuyaweka ndani hata kwa miaka saba hadi bei itakapokuwa nzuri. Lakini ukilima viazi, nyanya, vitunguu nk, tegemea maumivu. Kulaliwa nje nje!
 
Nikiwa katika harakati zangu kijiji kimoja huko Kahama ... Nilipata wasaa wa kukaa na wazee jioni moja. Wazee hawa wamelima maisha yao yote.. lakini hayuko hata mmoja anayetamani mwanae kuwa mkulima.

Katika maongezi yetu niligundua.. Madalali wasio waaminifu ndio tatizo. Madalali waliojaa Umimi, choyo, ulaghai na waongo ndio tatizo. Na jamii hii ya viumbe hawa (kupe) inamuibia kila mtu hata kupitia kodi.

Mawazo binafsi;
Ushauri niliowapatia wazee ulikuwa, pamoja na njia za kisasa za ukulima, bado walihitaji namna ya kisasa ya kuuza mazao yao, na namna bora kuongeza thamani.

Kinachoweza kufanyika kama jamii za vijijini ikiwa zitaondokana na Tamaa na Ubinafsi. Wanaweza kuanzisha maduka ya ushirika katika maeneo yenye uhitaji mkubwa wa mazao yao. Na kuunda utaratibu wa hisa zitazopatikana kwa kuthaminisha mavuno yao na ubora wake.

Ikiwa watafanikiwa, wataweza kuwaajiri watoto wao katika maeneo ya uzalishaji, matangazo na mauzo, usafirishaji, stoo nk. Na baadae kuajiri katika nyanja nyinginezo kadri vikundi hivi vinavyoendelea kukua na kudiversify uwekezaji wao.

Faida ya mfumo huu ni kuwalinda wazee watakapozeeka, kuongeza ajira..na kusaidia kilimo kukua na kuwa cha kisasa.

Madalali ni kupe. Madalali ni kupe. Ninakubaliana na wewe

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Kwahiyo umepiga doni wa madalali..sasa jiandaeni kula hivyo viazi vyenu wenyewe.

#MaendeleoHayanaChama
 
Kama laki nane hailipi kula mwenyewe chelema hizo, ngoja nikirudi nikukute wikendi ijayo... mbona umekimbia!
Dah jamaa naona unalazimisha tuzoeane...angalia profile yangu vizuri angalia post zangu vizuri kisha uje tena
 
Dah jamaa naona unalazimisha tuzoeane...angalia profile yangu vizuri angalia post zangu vizuri kisha uje tena

Achana na post, wewe umemkwaza doni wa kijiji kisha umekimbilia mjini na mkeo, huo uoga wako umewagharimu wakulima wengi jiandae kulaumiwa tu.
 
Kweli jamani kila mtu anatakiwa atafute riziki kihalali, ila vitu vingine vinaudhi, vinaumiza, niliamua kuwa mkulima kwa lengo la kujiongezea kipato, nikaamua kushirikiana na mzazi wangu aliyeko huko kijijini, tulianza kilimo cha viazi kwa kuanzia nilianza na hekari tano. Baada kulima kwa muda, mazao yakawa tayari kwa ajili ya kuvuna, wakulima wenzetu walituambia kwamba tusipate tabu ya kuvuna kwani kuna madalali huwa wanakuja wanachagua kisha wanaleta wateja ambao huvuna wenyewe.

Nikaona ni Jambo la kheri tuliwasiliana na dalali ambaye alituahidi siku ya kuja na wakulima wote tukawa tunamsubiri, mara nikaona kigari aina ya Paso kinakuja shambani kimeandikwa “wajinga ndio waliwao” akashuka pande la mtu suruali amevalia tumboni, tukatambulishwa kuwa jamaa ndiye dalali wakulima akiwemo mzazi wangu wanamnyenyekea utadhani nini sijui, kumbe yule bwana jukumu lake kukagua mazao shambani kisha anapanga bei, na ukitofautiana naye utapata wakati mgumu kuuza mazao yako kwani atawaeleza madalali wengine pia kwani wana mtandao.

Jamaa alikuja kwenye Shamba Letu wakati tunasubiri “ofa” jamaa akachukua panga na kuanza kufukua huku akisema “hamna kitu hapa chelema Tupu hizi, hapa labda niwape laki nane” nikamwambia hiyo hailipi akasema kama hailipi, hakuna mtu atatununua labda tukale wenyewe. Nikamuuliza, unataka kununua kwa lazima na kwa bei unayoitaka? Akajibu akasema yeye ndio don kijijini pale tulichukuana upepo, ukizingatia tabu anazopata mkulima halafu jitu levi tu linakuja na kuanza kutoa bei anazotaka na kwa lugha ya kebehi, aliinua mkono kwa lengo la kunipiga kibao nilimpiga Ngumi nyingi mfululizo.

Imebidi ahairishe zoezi la kukebehi na kulangua mazao. Wamesema atakuja tena Jumamosi ijayo nimemwambia mama tuelekee mjini kwani anaweza kuwa amejihami [emoji16] kilio ha wakulima, madalali wanatunyonya, hawalipi kodi ni wabaya.
Wengi na makada wa ccm
 
Madarari wengi ni wezi kama wezi wengne ....

Kuna siku niliwai kuwaza hivi kma leo kuna uwezekano wa kumuunganisha mzalishaji wa bidhaa,msambazaji na muuzaji (rejareja/jumla) kupitia simu au system yoyote ya kimawasiliano....kwanini isiwezekane ikaandaliwa system ya kuwaungamisha wakulima,wasambazaji na wanunuzi uku mijini kupitia simu zao wakulima....mfano mkulima akitaka kuangalia Bei sokoni azame tu chapu Kwenye simu ajue...

Au ata mnunuzi akitaka bidhaa kutoka kwa mkulima azame kweny sm yake aangalie Bei then atafute na Bei ya usafiri then anaweka order mzigo unamfikia.

Naamini Hawa madalali wangepotea na tungekuwa mbali na hyo system ingeweza kua accessiwa na nchi adi za nje.

Yaani Hawa madalali wengne hawana tofauti na wale mateja wanaovizia daladala ikisimama ili wapate miamia
 
Dalali ni mtu mvivu anaetegemea kula kutokana na majasho ya wengine.mimi nimelima mpunga wangu mbegu ambayo gunia la debe sita kwa shambani linauzwa elfu themanini.mume wangu akampigia mtu ambae aliahidi kuja kununua akamwambia sogeza mpaka barabarani mwendo mrefu tu Kama nusu saa kwa mguu magunia yakabebwa kila gunia elfu 5 yalikua 20.walisubiri wee mtu hakutokea .huwezi kurudisha shambani na yako barabarani hapo mimi niko hospitali nimejifungua kwa op.Daa akaja siku ya pili akaangalia mpunga kwa dharau akasema huu sio mpunga haya ni madudu hapa labda elfu 30 😆😆😆 mmh mume wangu akasema suizi kwa bei hiyo wakazozana wee wakafika kwenye arobaini.mpunga ambao ulikua 80 ukaenda kwa 40.

Cha Kwanza dalali ili akuwin anakufrustrate anakuonyesha kitu chako hakina thamani.
 
Dalali ni mtu mvivu anaetegemea kula kutokana na majasho ya wengine.mimi nimelima mpunga wangu mbegu ambayo gunia la debe sita kwa shambani linauzwa elfu themanini.mume wangu akampigia mtu ambae aliahidi kuja kununua akamwambia sogeza mpaka barabarani mwendo mrefu tu Kama nusu saa kwa mguu magunia yakabebwa kila gunia elfu 5 yalikua 20.walisubiri wee mtu hakutokea .huwezi kurudisha shambani na yako barabarani hapo mimi niko hospitali nimejifungua kwa op.Daa akaja siku ya pili akaangalia mpunga kwa dharau akasema huu sio mpunga haya ni madudu hapa labda elfu 30 [emoji38][emoji38][emoji38] mmh mume wangu akasema suizi kwa bei hiyo wakazozana wee wakafika kwenye arobaini.mpunga ambao ulikua 80 ukaenda kwa 40.

Cha Kwanza dalali ili akuwin anakufrustrate anakuonyesha kitu chako hakina thamani.
Washenzi kabisa hawa majamaa...hawana tofauti na mabeberu..ila hii yote ni kwa sababu ya ccm.

#MaendeleoHayanaChama
 
Washenzi kabisa hawa majamaa...hawana tofauti na mabeberu..ila hii yote ni kwa sababu ya ccm.

#MaendeleoHayanaChama
Madalali wasajiliwe ili isiwepo janja janja.ila naunga mkono hoja happy juu kuwepo na njia za kuwa eliminate
 
Back
Top Bottom