BilioneaPATIGOO
JF-Expert Member
- Jun 23, 2012
- 12,320
- 11,327
Kim Kardashian yupo kwenye wakati mgumu kiasi cha kuweka kila kitu pembeni na kuwa na jambo moja tu – kumwangalia mumewe Kanye West aliyelazwa kutokana na matatizo ya kiakili tangu wiki iliyopita.
Vyanzo vimeiambia tovuti ya TMZ kuwa Kim amekuwa kwenye wakati mgumu tangu avamiwe na majambazi mjini Paris, Ufaransa lakini tangu Kanye apate matatizo wiki iliyopita kila kitu kwake kimebadilika. Vyanzo hivyo vimesema kuwa Kim amekuwa kama mwokozi wa Kanye na amekuwa macho muda wote akimwangalia mume wake aliyelazwa kwenye hospitali ya UCLA Medical Center kwa wiki sasa.
Vyanzo vimesema amekuwa na mtihani kwake hasa kwakuwa kuna wakati Kanye amekuwa akizungumza kuwa watu walikuwa wanataka kuivunja ndoa yake. Ni moja ya chanzo cha mashaka yake makubwa.
Kim, anatarajiwa kumrudisha Kanye nyumbani Jumatatu hii na lengo lake ni kuhakikisha anarejea kwenye afya yake. Chanzo kimoja kimesema Kim amejitoa haswaa na kwamba Kanye ana bahati kuwa naye.
“She has been an unbelievably devoted spouse. He’s a lucky man.”
Vyanzo vimeiambia tovuti ya TMZ kuwa Kim amekuwa kwenye wakati mgumu tangu avamiwe na majambazi mjini Paris, Ufaransa lakini tangu Kanye apate matatizo wiki iliyopita kila kitu kwake kimebadilika. Vyanzo hivyo vimesema kuwa Kim amekuwa kama mwokozi wa Kanye na amekuwa macho muda wote akimwangalia mume wake aliyelazwa kwenye hospitali ya UCLA Medical Center kwa wiki sasa.
Vyanzo vimesema amekuwa na mtihani kwake hasa kwakuwa kuna wakati Kanye amekuwa akizungumza kuwa watu walikuwa wanataka kuivunja ndoa yake. Ni moja ya chanzo cha mashaka yake makubwa.
Kim, anatarajiwa kumrudisha Kanye nyumbani Jumatatu hii na lengo lake ni kuhakikisha anarejea kwenye afya yake. Chanzo kimoja kimesema Kim amejitoa haswaa na kwamba Kanye ana bahati kuwa naye.
“She has been an unbelievably devoted spouse. He’s a lucky man.”