Kimei aishukuru klabu ya Rotary Mwika kushiriki maendeleo vunjo

SautiYaMnyonge

JF-Expert Member
Joined
May 13, 2018
Posts
439
Reaction score
742
Na Mwandishi Wetu
Vunjo.

Mbunge wa jimbo la Vunjo Mhe Dkt Charles Stephen Kimei ameishukuru klabu ya Rotary ya Mwika kwa kujenga kivuko cha Koongo-Saghai kinachounganisha kata za Mwika Kusini na Mwika Kaskazini.

Ujenzi wa kivuko hicho umegharimu shilingi milioni 10.5 fedha zilizotolewa na klabu hiyo ya Rotary ambayo Mhe Mbunge ni mwanachama.

"Vunjo tunayoitamani itajengwa na kila mmoja wetu aliyopo ndani na nje ya Vunjo. Hivyo nawakaribisha wanavunjo wote wenye nia na dhamira njema ya kutaka kuweka alama katika maendeleo ya jimbo letu katika sekta za afya, elimu, barabara, michezo nk waje tushirikiane kuijenga Vunjo yetu. Hii ndiyo Vunjo Mpya!" Alisema Dkt Kimei

#PamojaTunaweza

Picha ya 1: Kilichokuwa kivuko cha Koongo-Saghai

Picha 2: Kinavyoonekana sasa kivuko hicho cha Koongo-Saghai baada ya ujenzi kukamilika.

KIMEI MITANO TENA

 



Mbunge wa jimbo la Vunjo Mhe Dkt Charles Kimei ameishukuru klabu ya Rotary ya Mwika kwa kujenga kivuko kinachounganisha kata za Mwika Kusini na Mwika Kaskazini.

Ujenzi umegharimu shilingi milioni 10.5 fedha zilizotolewa na klabu hiyo ya Rotary ambayo Mbunge ni mwanachama.
 
million 10 hiko kidaraja? seriously come on ?

no offence ni jambo jema kwa wananchi wa mwika but they can do better
 
Mwendazake alivyokuwa anapenda kick angekuwa hai angeenda kuzindua yeye hicho kidaraja uchwara cha 10ml
 
Mwendazake alivyokuwa anapenda kick angekuwa hai angeenda kuzindua yeye hicho kidaraja uchwara cha 10ml
Lazima angeenda kwanza hakuna ambaye angefanya uzinduzi maana anayefanya uzinduzi ni yeye pekee. Lilikuwa linapenda sofa sana za kijinga. Pathetic
 
Jambo jema, asiyeshukuru kidogo hashukuru kikubwa.

Rotary Club ni moja ya matawi ya freemasons
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…