By @zamaradimketema . . Hata ukinyamanza kimya watu watalazimisha ubrag tu hata kama sio tabia yako, kuanzia kila ulichokiona hakuna nilichochangiwa wala kupewa bure, MSIMCHAFUE SPONSOR WANGU ambayo mimi ni BALOZI WAKE, watu walikula, walikunywa na na narudia tena NI PESA YA MFUKONI MWANGU iliyotokana na MDHAMINI WANGU.. ALINILIPA ZAIDI YA HIYO NA ACOCOVER COST ZOTE, Na naongea hivi pia kuprotect BRAND ya wadhamini wangu sababu uongo unapitiliza sana, nataka niseme hivi KWA KUJIAMINI. Sijawahi kuomba mchango, kuchangisha wala Kuchangiwa na yeyote kwenye 40 ya mwanangu, na zaidi kama kuna mtu angetaka kunichangia NINGEKATAA bado maana sioni sababu kwenye kitu kama cha kujifurahisha mwenyewe, leo natungiwa maneno kila kona ili tu kunishusha, nawahakikishia SITASHUKA KWA HILO, na zaidi yeyote alieleta chochote kutoka popote ni ZAWADI AMBAZO SIKUOMBA ila mapenzi ya watu binafsi, sina shilingi kumi ya mtu niliyokula na HAKUKUWA NA HELA YA KULIWA inayoweza kunisaidia kwenye party wala maisha yangu, nawaruhusu kunichukia ila msilazimishe uongo kuwa kweli, kuna tofauti kubwa kati ya ZAWADI NA MICHANGO hivi mimi nina power gani ya kulazimisha watu wachange na wakachanga kwa kuniogopa, hivi NINAOGOPEWA KIASI HIKO ama NINA NGUVU HIYO!?? Au kuna karama mnayoiona ambayo mimi sijaigundua!?? Kweli jamani!??? Aaaaaah msifanye hivyo, kuna muda kubali yaishe, ZAMU YANGU IMEFIKA.. badala ya kukalia majungu na roho mbaya muombe MUNGU akuone, usiwe busy kushusha watu kwa uongo na uzushi na kuwachafua ama kuwatukanisha HAITAKUPANDISHA WEWE!! Sana sana unajibebea laana za kushindwa kuendelea, hata MBELE ZA MUNGU hafurahii. Nisameheni niliowakwaza, nililazimika kuliweka hili sawa sababu lilitaka kuathiri hadi brand ya wengine ninayoisimamia mimi. MNIWIE RADHI.