Pre GE2025 Kimeumana! mjumbe adakwa akidaiwa kugawa nauli uchaguzi Bavicha

Pre GE2025 Kimeumana! mjumbe adakwa akidaiwa kugawa nauli uchaguzi Bavicha

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Sintofahamu imezuka katika uchaguzi wa viongozi wa Baraza la Vijana la Chadema (Bavicha), baada ya wajumbe kumtilia shaka mmoja wa wagombea aliyekuwa akitoa nauli.

Uchaguzi wa Bavicha unaendelea katika ukumbi wa Ubungo Plaza, jijini Dar es Salaam leo Jumatatu Januari 13, 2025.

Pia, Soma: Mjumbe wa mkutano mkuu BAVICHA alilia posho ya kujikimu, 'tuliambiwa tutalipwa ila hadi sasa bado, kwa hali hii tunaweza kuepuka rushwa?'

Mashaka zaidi, yametokana na mgombea huyo kudaiwa kugawa nauli hizo katika eneo la kificho, wajumbe wakiuliza ana mamlaka gani ya kutoa fedha hizo.

Hali hiyo ilizua tafrani baada ya wajumbe kutoka ukumbini kwenda alikokuwa mgombea huyo, wakihoji yeye ni nani hadi atoe nauli kwa wajumbe.

Baadaye, msimamizi msaidizi wa uchaguzi huo, Salum Mwalimu aliwataka walinzi kuwaondoa watu wote kwenye korido za ukumbi huo.

Kisha, aliwaamrisha wajumbe waingie ndani kusikiliza sera za wagombea wa ujumbe wa baraza kuu waliokuwa wanajinadi.

Soma: Kinachoendelea katika Uchaguzi BAVICHA Taifa
 
Mbowe yupo nyumba ya wakati, kizazi cha sasa sio cha miaka ya 2009 badala ya kuelewa yeye kashupaza shingo

Ilitosha hotuba ya Pambalu imuamshe kutoka usingizini badala yake yeye anajiona pesa ya mama Abdul itawafanya yeye na Wana CCM wenzake waliopo CDM kushinda uongozi
 
Mgawa rushwa nasikia ni Kibibi ambaye ni team Mbowe.

.......Fedheha hii.

Chadema ukiwaona kwenye majukwaa wanavyokemea rushwa kama watu vile kumbe ni Mbwa mwitu.

Aibu kabisa.
 
Mgawa rushwa nasikia ni Kibibi ambaye ni team Mbowe.

.......Fedheha hii.

Chadema ukiwaona kwenye majukwaa wanavyokemea rushwa kama watu vile kumbe ni Mbwa mwitu.

Aibu kabisa.
Rushwa haina chama ni tabia za jamii yoyote iliyopoteza muelekeo.

Madereva wanaotoa rushwa huko barabarani kwa Trafiki ni wote ni CHADEMA?
 
Dah 😂
Kuna wapumbavu wanasema chadema ni baba wa demokrasia 😂

Bora upumbavu wa ccm kuliko ujinga wa chadema
 
Back
Top Bottom