kwisha
JF-Expert Member
- Sep 9, 2021
- 1,779
- 4,982
Mnamo tarehe 7/2/1706, Kimpa Vita aliuawa kwa kuchomwa moto na mishenari wa kikatoliki huko nchini Congo.
Kimpa vita aliuliwa kwa sababu tu ya kuwahubiria watu kuhusu imani ya kijadi ya Kongo na kuwashawishi wakongo kurejea katika imani na mila. Mwana mama huyu, pia aliwataka wakongo wa jamii ya Mbanza kurejea katika aridhi yao baada ya kuikimbia kwa muda mrefu kufuatia kuanguka kwa utawala wa VITA -A- NKANGA katika Vita maarufu ya Mbwila (Ambuila 1665).
Kimpa Vita aliuliwa kwa sababu alikuwa akiwashawishi wakongo kuachana na dini ya kikristo (katoliki) na kuwataka kurejea katika imani zao.
Alipokuwa mdogo, Kimpa Vita alibatizwa kwa jina la Ana Beatriz, lakini punde alipoanza harakati zake za kuwarejesha wenzie Katika imani ya nyumbani kwao, alilikataa jina hilo la kikristo na kubeba jina lake la asili la Kimpa Vita au kimpa Nkya Nvita maana yake 'Mbinu mpya za mapambano' huku akiwa amejikita katika mapambano ya kiimani/kiroho.
Kimpa Vita alichomwa moto na mishenari wa kikatoliki yeye pamoja na mwanaye akiwa amembeba mgongoni.
Kimpa vita aliuliwa kwa sababu tu ya kuwahubiria watu kuhusu imani ya kijadi ya Kongo na kuwashawishi wakongo kurejea katika imani na mila. Mwana mama huyu, pia aliwataka wakongo wa jamii ya Mbanza kurejea katika aridhi yao baada ya kuikimbia kwa muda mrefu kufuatia kuanguka kwa utawala wa VITA -A- NKANGA katika Vita maarufu ya Mbwila (Ambuila 1665).
Kimpa Vita aliuliwa kwa sababu alikuwa akiwashawishi wakongo kuachana na dini ya kikristo (katoliki) na kuwataka kurejea katika imani zao.
Alipokuwa mdogo, Kimpa Vita alibatizwa kwa jina la Ana Beatriz, lakini punde alipoanza harakati zake za kuwarejesha wenzie Katika imani ya nyumbani kwao, alilikataa jina hilo la kikristo na kubeba jina lake la asili la Kimpa Vita au kimpa Nkya Nvita maana yake 'Mbinu mpya za mapambano' huku akiwa amejikita katika mapambano ya kiimani/kiroho.
Kimpa Vita alichomwa moto na mishenari wa kikatoliki yeye pamoja na mwanaye akiwa amembeba mgongoni.