Kinachoendelea Diamond Jubilee ni utafunaji wa Bajeti inayotakiwa kwenda kuboresha huduma za jamii

Kinachoendelea Diamond Jubilee ni utafunaji wa Bajeti inayotakiwa kwenda kuboresha huduma za jamii

Msanii

Platinum Member
Joined
Jul 4, 2007
Posts
25,252
Reaction score
36,513
Muda huu tarehe 10 Machi 2023, ninamuona Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam CPA Amos Makala akiongoza shughuli ya kumpongeza mama Samia kutimiza miaka 2 ya uongozi wake madarakani.

Kumpongeza Rais kwa kutimiza miaka miwili madarakani ni jambo la kumpongeza lakini ni muhimu sana kuzingatia usahihi wa namna ya kupongeza. Shughuli inayofanyika Diamond Jubilee imetumia bajeti ambayo sidhani kama ipo kwenye votes za bajeti iliyopitishwa na Bunge.
Kuna tatizo linalohusu madawati, ubovu wa barabara, tatizo la maji jijini na mambo mengine. Lakini nilidhani pesa hizi zinazotumika kufanya sherehe za kumpongeza mama zingemheshimisha sana endapo mkuu wa Mkoa na wasaidizi wake wangeelekeza nguvu kutatua baadhi ya kero kupitia hela hizo na badala yake zinatumika kufanya sherehe.

kwa namna ninavyofahamu viongozi wengi wa Dar, lazima hapo uchotaji wa fedha za umma kwa kigezo cha shughuli ya kumpongeza mama.

Tungempongeza mama kwa kufanyakazi za kujitolea, kukagua miradi ya serikali na kufanya mikutano ya kusikiliza kero za wananchi na kuzitatua.

Nakupongeza Rais Samia kwa kutimiza miaka 2 madarakani na tunaamini safari inaendelea lakini wasaidizi wako wanaonekana kupwaya na hawakusaidii bali wanafanya uzidi kuwa mbali na wananchi wako.
 
Muda huu tarehe 10 Machi 2023, ninamuona Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam CPA Amos Makala akiongoza shughuli ya kumpongeza mama Samia kutimiza miaka 2 ya uongozi wake madarakani.

Kumpongeza Rais kwa kutimiza miaka miwili madarakani ni jambo la kumpongeza lakini ni muhimu sana kuzingatia usahihi wa namna ya kupongeza. Shughuli inayofanyika Diamond Jubilee imetumia bajeti ambayo sidhani kama ipo kwenye votes za bajeti iliyopitishwa na Bunge.
Kuna tatizo linalohusu madawati, ubovu wa barabara, tatizo la maji jijini na mambo mengine. Lakini nilidhani pesa hizi zinazotumika kufanya sherehe za kumpongeza mama zingemheshimisha sana endapo mkuu wa Mkoa na wasaidizi wake wangeelekeza nguvu kutatua baadhi ya kero kupitia hela hizo na badala yake zinatumika kufanya sherehe.

kwa namna ninavyofahamu viongozi wengi wa Dar, lazima hapo uchotaji wa fedha za umma kwa kigezo cha shughuli ya kumpongeza mama.

Tungempongeza mama kwa kufanyakazi za kujitolea, kukagua miradi ya serikali na kufanya mikutano ya kusikiliza kero za wananchi na kuzitatua.

Nakupongeza Rais Samia kwa kutimiza miaka 2 madarakani na tunaamini safari inaendelea lakini wasaidizi wako wanaonekana kupwaya na hawakusaidii bali wanafanya uzidi kuwa mbali na wananchi wako.
Hakuna mtu mwovu hapa Tanzania kama Kikwete yeye ndio ameleta haya

USSR
 
Naona kama shuguli shuguli zimekuwa nyingi sana
Kila siku mashuguli .....duh

Ova
Kwa sababu mama anaonekana kutokukubalika sana> Wale wazee wa Mwanaaangu Naaape! wameweka mikakati kuwepo na shughuli zinazomtajataja mama kila kona.
Sasa hapo Diamond Jubilee waliopelekwa ni Watendaji wa Kata, Mitaa na wenyeviti wa mitaa pamoja na Madiwani

Waliojaza ukumbi ni vijana wa hamasa
 
Kuna jitu lilikuwa likiimbwa na kuabudiwa kila kukicha lakini mlinyamaza maana mliogopa kuokotwa kwenye viroba sasa mama wa watu amewaacha mlopoke muwezavyo na hana neno na mtu, msemeni tu,mtukaneni kadri mpendavyo hiyo ndiyo demokrasia yeye hajioni ni mungu mtu asiyetaka kukosolewa.
 
Kuna jitu lilikuwa likiimbwa na kuabudiwa kila kukicha lakini mlinyamaza maana mliogopa kuokotwa kwenye viroba sasa mama wa watu amewaacha mlopoke muwezavyo na hana neno na mtu, msemeni tu,mtukaneni kadri mpendavyo hiyo ndiyo demokrasia yeye hajioni ni mungu mtu asiyetaka kukosolewa.
Hii id Ina kazi ngapi?
 
Kama ni kweli, binafsi nalaani matumizi mabaya ya fedha za umma, kama wamechangishana kufanya hiyo party sawa ila kama wametumia fedha za umma....hakika hayo ni matumizi mabaya ya fedha za umma.
 
Back
Top Bottom