BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,591
- 8,826
Ndani ya saa 24 baada ya jibu la ombi kuwasilishwa, kiambatanisho kitawasilishwa na kutolewa uamuzi, ambapo upande wa Mawakili wa Rais Mteule William Ruto utakuwa na siku 4 kuwasilisha na kutoa majibu kufuatia ombi hilo. Mkutano wa kabla ya kesi utafanyika ndani ya Mahakama Kuu kwa siku 8 kuanzia tarehe ya kuwasilisha Pingamizi la Uchaguzi wa Rais
Mahakama ya Majaji 7 ikiongozwa na Jaji Mkuu Martha Koome itaamua kesi hiyo ndani ya muda uliowekwa wa siku 14 (Septemba 15, 2022) kuanzia siku ambayo ombi hilo liliwasilishwa. Kesi hiyo itachukua jumla ya siku 3 kabla Mahakama ya Majaji 7 kuandika na kutoa uamuzi wa mwisho
Iwapo Majaji watatoa uamuzi wa kuhesabiwa upya kwa Kura za Urais, Mahakama Kuu itasimamia zoezi la kuhesabu upya kura kisha itamtangaza mshindi na kutoa cheti. Iwapo ushindi wa William Ruto utaidhinishwa, ataapishwa mnamo Novemba 12, 2022 kama Rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya
Kulingana na Sheria ya Uchaguzi ya 2011, Mamlaka ya Mahakama ya Uchaguzi huiamuru Mahakama Kuu kutangaza mshindi iwapo itaagiza kuhesabiwa upya kwa Kura za Urais.
-
Kifungu cha 80 ibara ndogo ya 4 cha Sheria ya Uchaguzi ya 2011 kinasema:
- Mahakama ya Uchaguzi inaweza kwa amri, kuagiza Tume kutoa cheti cha ushindi wa Rais, Mbunge au Mjumbe wa Bunge la Kaunti ikiwa baada ya kuhesabiwa upya kwa kura zilizopigwa, mshindi anaonekana; na mshindi huyo akionekana kuwa hakutenda kosa la uchaguzi.
Kifungu cha 140 (c)
- Ikiwa Mahakama Kuu itaamua kuwa Uchaguzi wa Rais ni batili, uchaguzi mpya utafanywa ndani ya siku 60 baada ya uamuzi.
Mahakama ya Majaji 7 ikiongozwa na Jaji Mkuu Martha Koome itaamua kesi hiyo ndani ya muda uliowekwa wa siku 14 (Septemba 15, 2022) kuanzia siku ambayo ombi hilo liliwasilishwa. Kesi hiyo itachukua jumla ya siku 3 kabla Mahakama ya Majaji 7 kuandika na kutoa uamuzi wa mwisho
Iwapo Majaji watatoa uamuzi wa kuhesabiwa upya kwa Kura za Urais, Mahakama Kuu itasimamia zoezi la kuhesabu upya kura kisha itamtangaza mshindi na kutoa cheti. Iwapo ushindi wa William Ruto utaidhinishwa, ataapishwa mnamo Novemba 12, 2022 kama Rais wa 5 wa Jamhuri ya Kenya
Kulingana na Sheria ya Uchaguzi ya 2011, Mamlaka ya Mahakama ya Uchaguzi huiamuru Mahakama Kuu kutangaza mshindi iwapo itaagiza kuhesabiwa upya kwa Kura za Urais.
-
Kifungu cha 80 ibara ndogo ya 4 cha Sheria ya Uchaguzi ya 2011 kinasema:
- Mahakama ya Uchaguzi inaweza kwa amri, kuagiza Tume kutoa cheti cha ushindi wa Rais, Mbunge au Mjumbe wa Bunge la Kaunti ikiwa baada ya kuhesabiwa upya kwa kura zilizopigwa, mshindi anaonekana; na mshindi huyo akionekana kuwa hakutenda kosa la uchaguzi.
Kifungu cha 140 (c)
- Ikiwa Mahakama Kuu itaamua kuwa Uchaguzi wa Rais ni batili, uchaguzi mpya utafanywa ndani ya siku 60 baada ya uamuzi.