Kinana, hala hala msijelikoroga juu ya rasimu ya Katiba Mpya!

Kinana, hala hala msijelikoroga juu ya rasimu ya Katiba Mpya!

masopakyindi

Platinum Member
Joined
Jul 5, 2011
Posts
18,207
Reaction score
13,839
Nimemwona katika luninga, ITV , na kumsoma vizuri Katibu Mkuu wa CCM, juu ya rasimu mpya ya katiba na msimamo wake kichama.

Naona Kinana anajaribu kutembea katika mto wenye mawe ya utelezi, asipoangalia ataanguka yeye pamoja na chama-CCM.

Nafikiri CCM bado haijajijua kuwa iko katika awamu ya mpito kisiasa, na suala la uendeshaji wa serikali zilzomo hauwezi kuwa na muono wa miaka 50 iliyopita.

Kilichonipa wasiwasi, na mimi ni mwana CCM, ni hii nukuu ya gazeti la Nipashe, kama ilivyo katika magazeti mengi
Noashe leo 7/6/2013 uk4;

"Chama cha Mapinduzi (CCM) kimesema hakiungi mkono rasimu ya katiba mpya iliyozinduliwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jumatatu wiki hii kwa asili mia mia moja.

Chama hicho kimesema wiki ijayo kitatoa msimamo wake kuhusu rasimu hiyo iliyoandaliwa na tume hiyo iliyoongozwa na Jaji Joseph Warioba.

Kauli hiyo ya chama tawala ilitolewa jana jijini Dar es salaam na Katibu Mkuu wake, bdulrahman Kinana, baada ya kuulizwa na waandishi wa habari kuhusu msimamo wa chamachake juu ya rasimu mpya"


Sasa hapo ndio naona Chama kinataka kuingiza doubt juu ya kazi nzuri iliyofanywa na Kamati ile ya kisomi ya Jaji Warioba.
Kamatti ile ilikuwa na wasomi wengi na hata makada wa vyama tofauti, na nilipendezwa na msimao wao wa utaifa kwanza.
Kinana naona ana fanya attempt ya kuingiza siasa za kichama katika maoni yaliyokusanywa nchi nzima na yanayoelekea kuwa yamewakuna wengi.

Kama CCM itafanya mabadiliko makubwa katika rasimu hiyo, basi wengi tutajiuliza ni kwa manufaa ya nani na kwa ridhaa ya nani.
Hili tutajiuliza maana walioulizwa kutoa maoni yao wakati wa utayarishaji wa rasimu hiyo ni watanzania wote bila kujali itikadi za kichama.

Na dio maana nasema, hala hala Kinana, usijelikoroga, mawe hayo anayaojaribu kutembea juu yake yana utelezi mwingi.
Na asijekuta chama na yeye mwenyewe wanabebwa na maji yanayokwenda kasi ya mabadiliko ya kihistoria
 
Nimemwona katika luninga, Itv , na kumsoma vizuri Katibu Mkuu wa CCM, juu ya rasimu mpya ya katiba na msimamo wake kichama.

Naona Kinana anajaribu kutembea katika mto wenye mawe ya utelezi, asipoangalia ataanguka yeye pamoja na chama-CCM.

Nafikiri CCM bado haijajijua kuwa iko katika awamu ya mpito kisiasa, na suala la uendeshaji wa serikali zilzomo hauwezi kuwa na muono wa miaka 50 iliyopita.

Kilichonipa wasiwasi, na mimi ni mwana CCM, ni hii nukuu ya gazeti lla Majira , kama ilivyo katika magazeti mengi
Majira leo 7/6/2013;

"Chama cha Mapinduzi (CCM) kimesema hakiungi mkono rasimu ya katiba mpya iliyozinduliwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba Jumatatu wiki hii kwa asili mia mia moja.

Chama hicho kimesema wiki ijayo kitatoa msimamo wake kuhusu rasimu hiyo iliyoandaliwa na tume hiyo iliyoongozwa na Jaji Joseph Warioba.

Kauli hiyo ya chama tawala ilitolewa jana jijini Dar es salaam na Katibu Mkuu wake, bdulrahman Kinana, baada ya kuulizwa na waandishi wa habari kuhusu msimamo wa chamachake juu ya rasimu mpya"


Sasa hapo ndio naona Chama kinataka kuingiza doubt juu ya kazi nzuri iliyofanywa na Kamati ile ya kisomi ya Jaji Warioba.
Kamatti ile ilikuwa na wasomi wengi na hata makada wa vyama tofauti, na nilipendezwa na msimao wao wa utaifa kwanza.
Kinana naona ana fanya attempt ya kuingiza siasa za kichama katika maoni yaliyokusanywa nchi nzima na yanayoelekea kuwa yamewakuna wengi.

Kama CCM itafanya mabadiliko makubwa katika rasimu hiyo, basi wengi tutajiuliza ni kwa manufaa ya nani na kwa ridhaa ya nani.
Hili tutajiuliza maana walioulizwa kutoa maoni yao wakati wa utayarishaji wa rasimu hiyo ni watanzania wote bila kujali itikadi za kichama.

na dio maana nasema , hala hala Kinana , usijelikoroga, mawe hayo anayaojaribu kutembea juu yake yana utelezi mwingi.
Na asijekuta chama na yeye mwenyewe wanabebwa na maji yanayokwenda kasi ya mabadiliko ya kihistoria

mkuu, unafikiri ccm ni kama chadema? ccm huwa haikurupuki tu kuunga mkono au kukataa. kinana amesema kuwa wao kama chama hawajakutana na kutolea uamuzi juu ya rasimu hiyo wa ama kuunga mkono kwa asilimia mia moja au la. amesema kuwa kamati kuu itakutana wiki ijayo na watajadili na hatimaye kutoa msimamo wa chama.
 
chadema badala ya kutumia muda wenu kuitafakari mnangoja kauli ya ccm ndo na nyie mpate pa kutokea. unajua chama kikiongozwa na mbumbumbu, huwa kinashindwa kujadili mambo mazito kama rasimu ya katiba. wao wanang'ang'ana na mabaraza ya katiba tu
 
mkuu, unafikiri ccm ni kama chadema? ccm huwa haikurupuki tu kuunga mkono au kukataa. kinana amesema kuwa wao kama chama hawajakutana na kutolea uamuzi juu ya rasimu hiyo wa ama kuunga mkono kwa asilimia mia moja au la. amesema kuwa kamati kuu itakutana wiki ijayo na watajadili na hatimaye kutoa msimamo wa chama.
`Hatua hiyo imeshpitwa na wakati na ndio maana hata Mawaziri Wakuu karibu wote walienda pale kutoa maoni yao KABLA ya kutayarishwa rasimu.
Hili la Kinana nasema ni jaribio la kuzuia maoni halali ya walio wengi.
 
halafu hayo magazeti yenu yanayoandika kinyumenyume mtakuja kuumbuka. huwezi kusema kuwa chama cha mapinduzi kimesema hakiungi mkono rasimu ya katiba wakati hawajakaa kama chama kuijadili.
 
Huku ni kupotosha watu nadhani,kinana wala hakumaanisha unacho maanisha mkuu,yeye alibainisha kuwa chama bado hakitatoa tamko la kukubari au kukataa rasimu kwa vile hawajaisoma na kuichambua.
 
mkuu, naona wewe huelewi kabisa mchakato unavyoendelea. baada ya rasimu kutoka, bado kuna mchakato wa mabaraza ya katiba ambayo vyama vina wawakilishi, bunge la katiba ambalo naamini litakuwa na wadau wa vyama vya siasa na referendum. michakato yote hiyo huwezi kuzuia watu kutoa maoni. kumbuka, ile ni rasimu na si katiba kamili. watu wanastahili kutoa maoni yao juu ya vipengele ambavyo wanaona vinastahili kufanyiwa marekebisho
 
halafu hayo magazeti yenu yanayoandika kinyumenyume mtakuja kuumbuka. huwezi kusema kuwa chama cha mapinduzi kimesema hakiungi mkono rasimu ya katiba wakati hawajakaa kama chama kuijadili.
Mkuu mbona hueleweki, wewe ndio Kinana mwenyewe nini?
Mbona nukuu umewekewa pale juu, ni kiasi cha kukanusha kilichoandikwa ili kuondoa kiwingu kinachoanza kukusanyika juu ya kauli ya Kinana.
 
`Hatua hiyo imeshpitwa na wakati na ndio maana hata Mawaziri Wakuu karibu wote walienda pale kutoa maoni yao KABLA ya kutayarishwa rasimu.
Hili la Kinana nasema ni jaribio la kuzuia maoni halali ya walio wengi.
Wewe usifanye watu kama watoto kwamba hawafuatilii taarifa sote tumemsikia alichosema but hili ulilo andika humuni tamko lako labda siyo kinana.
 
mkuu, naona wewe ndo umepitwa na wakati au unajua ila unafanya makusudi
 
Hilo ndio tego ambalo ccm hawakulijua na hapo ndio ujue chadema ni chama makini, Wao walifikiria kuunda katiba mpya mchezo!!! Acha wahangaike nalo .si yetu macho, Mtego huu atimae ccm amenasa kwenye nyavu?
 
Akihojiwa jana na waandishi wa habari kinana alibainisha kwamba kwa sasa si wakati mwafaka wa kuipinga au kuiku bari rasimu hiyo kwa kuwa bado hawajaisoma na kuichambua pindi watakapo isoma wataweza kutoa tamko la chama.
 
`Hatua hiyo imeshpitwa na wakati na ndio maana hata Mawaziri Wakuu karibu wote walienda pale kutoa maoni yao KABLA ya kutayarishwa rasimu.
Hili la Kinana nasema ni jaribio la kuzuia maoni halali ya walio wengi.
Mkuu, inawezekana wewe hujui hata kidogo mchakato wa kupata katiba mpya. Bado kuna hatua ya mabaraza ya katiba, bunge la katiba, referendum kabla ya draft ya mwisho kuchapishwa. Hatua zote hizo huwezi kuzuia wadau kutoa maoni yao. Labda kama unatumia utaratibu wa chadema wa kusubiri maoni ya kiongozi mmoja mmoja badala ya msimamo wa chama
 
chadema badala ya kutumia muda wenu kuitafakari mnangoja kauli ya ccm ndo na nyie mpate pa kutokea. unajua chama kikiongozwa na mbumbumbu, huwa kinashindwa kujadili mambo mazito kama rasimu ya katiba. wao wanang'ang'ana na mabaraza ya katiba tu

kwa hiyo unataka uwasikie na wao wakitoa tamko. mbona unalazomisha mkuu vp? we subiri ya kwenu si tayari? kiherehere cha kuitaja cdm unataka nini?
 
Hilo ndio tego ambalo ccm hawakulijua na hapo ndio ujue chadema ni chama makini, Wao walifikiria kuunda katiba mpya mchezo!!! Acha wahangaike nalo .si yetu macho, Mtego huu atimae ccm amenasa kwenye nyavu?
Mkuu. Inamaana unataka kutuambia kuwa chadema hawatatoa maoni yao juu ya rasimu ya katiba ili baadaye waseme kuwa katiba hiyo ni ya ccm?
 
kwa hiyo unataka uwasikie na wao wakitoa tamko. mbona unalazomisha mkuu vp? we subiri ya kwenu si tayari? kiherehere cha kuitaja cdm unataka nini?
Mkuu, chadema ndo wana utamaduni wa kukurupuka kusema mambo individually badala ya kusubiri msimamo wa chama
 
Mkuu mbona hueleweki, wewe ndio Kinana mwenyewe nini?
Mbona nukuu umewekewa pale juu, ni kiasi cha kukanusha kilichoandikwa ili kuondoa kiwingu kinachoanza kukusanyika juu ya kauli ya Kinana.
Mkuu, mbona kinana kaeleza vizuri kuwa chama hakijatoa msimamo? Hapo ndo maana nambalapala anasema kuwa magazeti haya yanaandika kinyumenyume
 
Ha ha ha.. Uzi umeanzishwa na wenyewe.. Halafu wanalumbana wenyewe.. Japo hoja ya masopakyindi ina mashiko.. Hawa wengine kazi yao ni kubisha tu.. Hata kama hoja imeletwa na gamba mwenzao.. Lol...
 
Last edited by a moderator:
Mkuu. Inamaana unataka kutuambia kuwa chadema hawatatoa maoni yao juu ya rasimu ya katiba ili baadaye waseme kuwa katiba hiyo ni ya ccm?

Tulia uone, Mmekurupuka nakatiba mpya wakati haikuwa agenda yenu, Lazima mtoane macho tu.
 
Back
Top Bottom