Kingwendu kujikita zaidi kwenye muziki, sasa asaka meneja

Bilionea Asigwa

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2011
Posts
16,515
Reaction score
28,506



Msanii wa vichekesho na muimbaji, Kingwendu amesema angependa kuwa na msimamizi wa shughuli zake katika sanaa ya muziki ili aweze kutoka badala ya kutegemea uchekeshaji peke yake.

Msanii wa vichekesho na muimbaji, Kingwendu amesema angependa kuwa na msimamizi wa shughuli zake katika sanaa ya muziki ili aweze kutoka badala ya kutegemea uchekeshaji peke yake.

Akizungumza na Times Fm, Kingwendu alisema kuwa amekuwa akitoa nyimbo mbalimbali lakini bahati mbaya hazipati nafasi ya kusikilizwa kwenye vituo vya redio kwa ajili ya kumtangaza.

“Nimegundua kuwa sababu kubwa ambayo inanikwamisha kutoka kimuziki ni kukosa meneja wa kusimamia kazi zangu, hivyo najaribu kuangalia uwezekano wa kumpata,” alisema kingwendu.

Msanii huyo alisema kuwa ana uwezo wa kupambana na wasanii wa muziki wa kizazi kipya wanaotamba kwa sasa na kuwabwaga iwapo atapata meneja wa kusimamia kazi zake vizuri.

“Hao wanaotamba sasa ni kwa sababu wana watu wa kusimamia kazi zao na mimi nitafanya hivyo ndipo mtaamini kile ninachokisema kwamba nina uwezo mkubwa wa kuimba ila ninakosa usimamizi tu,” alisema
 

Huyu na Majuto wapiga picha wengi huwa hawapendi kufanya nao Kazi kwakuwa hushindwa kujizuia kutokucheka pindi wanapokuwa wanawashuti. Scenes za Kingwendu na Majuto mpaka zije kukamilika zinaweza hata kuchukua siku nzima au mbili kwani kuna wakati unaweza ukamwambia Kingwendu au Majuto " cut " huku unamshuti tena ukiwa serious lakini kwa kituko ambacho mmoja wapo atakifanya utakuja kujikuta umeangusha Kamera au huna mbavu kwa kucheka. Kingwendu na Majuto kwa UKOMEDI hapa Tanzania ni habari nyingine!
 
Huyu ni mbunge wa Kisarawe 2020
Dah! Uchaguzi wa 2010 uliingia katika historia. Una kumbukumbu nyingi za kuvutia & za kufedhehesha pia.

Kingwendu anaingia kwenye kumbukumbu za kuvutia. Kampeni zake zilinifurahisha sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…