Economist Jay
Member
- Feb 18, 2016
- 42
- 51
Maneno bahati mbaya na nzuri yamekuwa yakisikika sana katika vinywa vya watu wengi duniani, mtu akifanikiwa kutoka salama katika ajali watu husema kuwa “yaani imekuwa bahati nzuri ametoka salama” na ikitokea labda wakati akitoka ndani ya gari baada ya ajali lakini akaumia mguu utasikia watu wanasema kuwa ‘wakati akitoka ndani ya gari bahati mbaya mguu wake umeteguka.’ Je, kauli hizi zina maana yoyote katika ulimwengu wa biashara?
Kabla sijajibu swali hilo hapo juu, napenda nirejee katika maana ya neno ‘bahati’. Neno bahati maana yake ni tarajio chanya limtokealo mtu katika maisha yake hapa duniani, kinyume na neno hili huitwa mkosi. Waswahili wengi hupenda kulazimisha maneno “bahati mbaya” kuwa neno “mkosi” kitu ambacho siyo sahihi. Hebu tafakari kauli zifuatazo;
John ana bahati, amepata ajali.
John ana bahati mbaya amepata ajali
John ana mkosi, amepata ajali
Ukiangalia sentensi zote hapo utagundua kuwa sentensi ya 1 na ya 2 siyo sahihi kwa sababu huwezi kuwa na bahati alafu ukapata ajali au ukawa na bahati kisha ikawa mbaya. Sentensi ya 3 iko sahihi kwa sababu mkosi huambatana na mabaya, na bahati huambatana na mazuri.
Kutokana na ukweli huo sasa tunaweza kutumia vizuri maneno hayo katika maongezi yetu katika maisha. Pamoja na kwamba kuna neno hili “bahati”, hii haina maana kuwa neno bahati linaweza kutumika kila mahali. Eneo ambalo neno hili halipaswi kutumika ni katika maswala yote yanayohusisha mipango katika kufikia malengo husika.
Sehemu yoyote ambayo kuna neno mipango, neno bahati halina nafasi kabisa, kutokana na kwamba bahati ni kitu cha kusadikika, hutokea lakini hakihusishi utaratibu fulani wa akili katika kupatikana kwake. Neno bahati hutofautiana na neno mkosi katika kutokea kwake, bahati hufariji kwa maana ya kuleta manufaa fulani lakini mkosi huondoa faraja na huleta huzuni.
Je, Maneno bahati, bahati mbaya, na bahati nzuri yana nafasi katika biashara na wafanyabiashara?
Jibu la swali hili liko wazi kabisa maneno hayo yote hayana nafasi katika biashara na kwa mfanyabiashara mwenyewe, kinywa cha mfanyabiashara hakitakiwi kabisa kutamka maneno hayo.
Biashara ni sayansi, inahusisha akili ya mtu kupanga mipango ya biashara ambayo itakufanya uweze kufikia malengo utakayojiwekea. Biashara hufuata njia zote za kisayansi katika kuanzishwa kwake na mavuno yake. Kutokana na maelezo haya unaweza kujiuliza; kwa nini watu huwa wana mipango mizuri kabisa na wanapokwenda kuitekeleza huwa wanaingia hasara?
Jibu la swahi hili pia liko wazi, ukijinasibu kuwa una mipango mizuri ya biashara lakini ulipokwenda kuitekeleza uliingia hasara, maana yake ni kuwa haukuwa na mipango thabiti, hasara huwa ni matokeo ya mipango mibovu ya biashara aliyokuwa nayo mtu.
kabla hujaanza biashara, unapojiandaa ni lazima uangalie na mambo ambayo huenda yakatokea kwa dharura na kusababisha uingie hasara, hivyo ukijiandaa na haya hapo ndipo unaweza kusema mpango wako wa biashara umeuweka vizuri, lolote litakalotokea ili kukukwamisha utakuwa tayari ulishaliwekea tahadhari, na hii ndiyo tunaita mpango madhubuti wa biashara.
Mfano unaweza ukawa umejiandaa kulima pamba, ukaandaa pesa kwa ajili ya kulimia, parizi, uvunaji lakini ukasahau bajeti ya kununua dawa ya kuulia wadudu watakaoshambulia matunda ya pamba shambani. Sasa hapa ukipata hasara usijekuanza kutuhumu kilimo na wadudu, ni lazima ujitafakari na kukubali kuwa hukuwa na mipango mizuri, ingekuwa ni mipango mizuri usingepata hasara.
Wafanyabiashara wengi husingizia kuwa hawana bahati na biashara, lakini ukweli ni kwamba hawana mipango mizuri ya biashara. huwezi kutegemea bahati kitu ambacho hakihusiki katika vitu vinavyohitaji akili ya mtu kuleta mpangilio mzuri wa kumnufaisha.
Biashara yoyote ile haiendeshwi kwa bahati, bali biashara duniani zinaendeshwa kwa mipango makini. Mfanyabiashara anatakiwa kujitahidi sana katika kupangilia vizuri mambo yake yote yanayohusisha biashara fulani.
Harasa ni matokeo ya mipango mibovu, bali faida ni kiashiria kuwa unatumia mipango madhubuti katika biashara.
Mafanikio ni haki yako!
Makala haya na nyengine nzuri utazipata kwenye link hii hapa chini
www.mgejwajr.com
0759708499
Kabla sijajibu swali hilo hapo juu, napenda nirejee katika maana ya neno ‘bahati’. Neno bahati maana yake ni tarajio chanya limtokealo mtu katika maisha yake hapa duniani, kinyume na neno hili huitwa mkosi. Waswahili wengi hupenda kulazimisha maneno “bahati mbaya” kuwa neno “mkosi” kitu ambacho siyo sahihi. Hebu tafakari kauli zifuatazo;
John ana bahati, amepata ajali.
John ana bahati mbaya amepata ajali
John ana mkosi, amepata ajali
Ukiangalia sentensi zote hapo utagundua kuwa sentensi ya 1 na ya 2 siyo sahihi kwa sababu huwezi kuwa na bahati alafu ukapata ajali au ukawa na bahati kisha ikawa mbaya. Sentensi ya 3 iko sahihi kwa sababu mkosi huambatana na mabaya, na bahati huambatana na mazuri.
Kutokana na ukweli huo sasa tunaweza kutumia vizuri maneno hayo katika maongezi yetu katika maisha. Pamoja na kwamba kuna neno hili “bahati”, hii haina maana kuwa neno bahati linaweza kutumika kila mahali. Eneo ambalo neno hili halipaswi kutumika ni katika maswala yote yanayohusisha mipango katika kufikia malengo husika.
Sehemu yoyote ambayo kuna neno mipango, neno bahati halina nafasi kabisa, kutokana na kwamba bahati ni kitu cha kusadikika, hutokea lakini hakihusishi utaratibu fulani wa akili katika kupatikana kwake. Neno bahati hutofautiana na neno mkosi katika kutokea kwake, bahati hufariji kwa maana ya kuleta manufaa fulani lakini mkosi huondoa faraja na huleta huzuni.
Je, Maneno bahati, bahati mbaya, na bahati nzuri yana nafasi katika biashara na wafanyabiashara?
Jibu la swali hili liko wazi kabisa maneno hayo yote hayana nafasi katika biashara na kwa mfanyabiashara mwenyewe, kinywa cha mfanyabiashara hakitakiwi kabisa kutamka maneno hayo.
Biashara ni sayansi, inahusisha akili ya mtu kupanga mipango ya biashara ambayo itakufanya uweze kufikia malengo utakayojiwekea. Biashara hufuata njia zote za kisayansi katika kuanzishwa kwake na mavuno yake. Kutokana na maelezo haya unaweza kujiuliza; kwa nini watu huwa wana mipango mizuri kabisa na wanapokwenda kuitekeleza huwa wanaingia hasara?
Jibu la swahi hili pia liko wazi, ukijinasibu kuwa una mipango mizuri ya biashara lakini ulipokwenda kuitekeleza uliingia hasara, maana yake ni kuwa haukuwa na mipango thabiti, hasara huwa ni matokeo ya mipango mibovu ya biashara aliyokuwa nayo mtu.
kabla hujaanza biashara, unapojiandaa ni lazima uangalie na mambo ambayo huenda yakatokea kwa dharura na kusababisha uingie hasara, hivyo ukijiandaa na haya hapo ndipo unaweza kusema mpango wako wa biashara umeuweka vizuri, lolote litakalotokea ili kukukwamisha utakuwa tayari ulishaliwekea tahadhari, na hii ndiyo tunaita mpango madhubuti wa biashara.
Mfano unaweza ukawa umejiandaa kulima pamba, ukaandaa pesa kwa ajili ya kulimia, parizi, uvunaji lakini ukasahau bajeti ya kununua dawa ya kuulia wadudu watakaoshambulia matunda ya pamba shambani. Sasa hapa ukipata hasara usijekuanza kutuhumu kilimo na wadudu, ni lazima ujitafakari na kukubali kuwa hukuwa na mipango mizuri, ingekuwa ni mipango mizuri usingepata hasara.
Wafanyabiashara wengi husingizia kuwa hawana bahati na biashara, lakini ukweli ni kwamba hawana mipango mizuri ya biashara. huwezi kutegemea bahati kitu ambacho hakihusiki katika vitu vinavyohitaji akili ya mtu kuleta mpangilio mzuri wa kumnufaisha.
Biashara yoyote ile haiendeshwi kwa bahati, bali biashara duniani zinaendeshwa kwa mipango makini. Mfanyabiashara anatakiwa kujitahidi sana katika kupangilia vizuri mambo yake yote yanayohusisha biashara fulani.
Harasa ni matokeo ya mipango mibovu, bali faida ni kiashiria kuwa unatumia mipango madhubuti katika biashara.
Mafanikio ni haki yako!
Makala haya na nyengine nzuri utazipata kwenye link hii hapa chini
www.mgejwajr.com
0759708499