Kiongozi aliyemezwa na tamaa kwa kuwadhulumu mafukara haamini kama kuna siku ya kiama

Kiongozi aliyemezwa na tamaa kwa kuwadhulumu mafukara haamini kama kuna siku ya kiama

Shaadya Salum

Member
Joined
Jan 24, 2024
Posts
13
Reaction score
6
Wewe ni kiongozi. Unaona watu unaowaongoza wanalalamikia uvunjifu wa katiba, kanuni, miongozo, na taratibu ambazo wewe kiongozi kwa viapo vyako na ahadi yako kwa CCM uliahidi kuvilinda, kuvitetea, na kuvihifadhi.

Mheshimiwa Rais anasisitiza haki, lakini wewe husikii; umeweka pamba masikioni. Viongozi wa dini wanahubiri haki, lakini wewe husikii. Viongozi wa kitaifa wanahubiri haki, lakini wewe husikii. Umekuwa nunda.

Ujue wewe, hata ukitamka neno Mwenyezi Mungu, unajitamkisha tu kutuzuga. Wewe ni tapeli. Upo unasubiri kumaliza tu maisha ya kidunia ili uende zako kuishi motoni. Ndiyo maana hujali vilio vya mafukara. Ndiyo maana ukiona mtu anaandika ukweli, roho yako chafu inakereka.

Bado muda unao, Badilika, Acha kujisahaulisha kwa utamu wa fedha za kuwadhulumu mafukara wanazostahili. Kumbuka daima kuwa moto wa jahanam kuni zake ni watu na mawe. Na inavyoonekana, usipobadilika na kuacha kufuru, utakuwa mmoja wa kuni za jahanam.

Kidumu Chama Cha Mapinduzi

IMG_20240408_123618.jpg
Pia soma:
 
Waambie wafanyakazi wa Hazina na wafanyakazi wa PSSSF wanavyokwiba mafao ya wafanyakazi! Wakwanza kupigwa na karma hapa duniani ni katibu mkuu wizara ya fedha na wa pili na Mkurugenzi mkuu PSSSF Dodoma
 
Actually ili nchi iweze kujikomboa ni lazima wananchi nao wapunguze mahaba na dini.

Kwenye ukomunisti wanasema dini ni nyenzo inayotumiwa na watawala kuwahadaa watawaliwa. Wewe masikini unaendele kujipa moyo kuwa utapata fungu jema baada ya kufa huku wao waki enjoy fungu jema wakati huu.

Ukitaka kufurukuta basi watawala wanawatumia viongozi wa dini kukwambia uache papara, mambo mazuri yapo baada ya wewe kufa, au umeichoka hii amani yetu tuliyonayo??? Basi na wewe unanywea kweli.

Ili ujikomboe unapaswa kupambana ili hiyo paradiso unayoiwaza itekelezwa hapahapa ukiwa hai.
 
Back
Top Bottom