Richard
JF-Expert Member
- Oct 23, 2006
- 15,692
- 23,038
Huku waasi wa M23 wakiwa wameuchukua na kuweka chini ya himaya yake mji wa Goma, baadhi ya vikosi vya askari wa kukodiwa walokuwa wakipigana sambamba na majeshi ya serikali ya Congo DRC, imekuwa ni viguu kuamini kuwa ndani ya Congo DRC kuna makundi ya waasi na mamluki yapatayo 120.
Yote makundi haya yapigania sehemu zenye rasilimali khasa Goma na upande wa mashariki mwa Congo DRC, lakini huku mapigano yao yakiacha watu zaidi ya 200,000 bila makazi. Upande wa mashariki ndo ulio katika shida kuwa kwani ndiko vita inakopiganwa huku majeshi ya Congo DRC yakikabiliana na vikosi vya waasi na kufanya vitendo vya kinyama dhidi ya raia wa Congo DRC kama ubakaji, utekaji na mauaji.
Kukiwepo na aina hii ya mgogoro inakuwa shida kuitatua kwa kutokuwa na namna na kutafuta suluhisho hususan namna ya kuvikutanisha vikundi hivi vya waasi. Yasemwa kuwa nchini Congo DRC yapo makundi makubwa zaidi ya 50 ya waasi ambao wengi wapo upande wa mashariki mwa nchi hiyo ambako ndiko kwenye rasilimali nyingi.
Hali hii yaleta ukakasi kuwa ipi ni idadi kamili ya makundi ya waasi iliyopo ndani ya nchi ya Congo DRC.
Taarifa kadhaa za kiuchambuzi na kijasusi zilikusanywa kwa kipndi cha tokea miaka ya 2000 zimebaini kuwepo kwa makundi rasmi yafuatayo ambayo mengi yapo upande wa Kaskazini na Kusini mwa jimbo la Kivu na kaskaizni mashariki.
1. M23
2. ADF. NALU
3. Mai-Mai Group
4. Nyatura Rebels
5. CNDP
6. LRA
7. Raia Mutomboki
8. FRPI
9. FPLC
10. FARDC
11. MILIA
12. FDLR
Sasa leo kiongozi wa makundi yote ta waasi Corneille Nangaa akiongea na waandishi wa habari mjini Goma, amesema m23 kuichukua Goma si suala la utani na kwamba wapo hapo mazima na wataendeleza kampeni yao ambayo itawapeka hadi mji mkuu wa Kinshasa.
Mwaka 2012 M23 ilipouchukua mji wa Goma walikaa hapo kwa mwaka mzima hadi walipofurushwa na majeshi ya Congo DRC na nchi kubwa duniani ziliweka shinikizo kwa Rwanda kusaidia kuwaondoa waasi hao na pia kusitisha misaada.
Safari hii si Marekani, Uingereza, Ufaransa wala UN wanochukua hatua zozote isipokuwa kutoa kauli za hapa na pale.
Kinoonekana kwa jicho la tatu ni kazi kapewa mtu asafishe njia.
Nini Rwanda itaendelea kufanya?
Kwenye majukwa ya kidiplomasia Rwanda itaendelea kuwatumia wanadiplomasia wake kujibu hoja mbalimbali na uwezo huo wanao. Tayari balozi wa Rwanda katika UN azijibu na kipangua hoja mbalimbali na hivyo kufanya kazi ya kuikosoa Rwanda kuwa ngumu kidiplomasia.
Kijeshi Rwanda bila shaka sasa hivi imesogeza ulinzi wake hadi Goma na eneo hilo litakuwa ndo Buffer ne mpya ya kujilinda na aina yoyote ya mashambulizi kutoka Congo DRC.
Je, Raisi Tshisekedi anafikiria nini.?
Raisi Tshisekedi ameamuru kukusanya vijana zaidi ili wajiunge na jeshi la Congo DRC maana wanajeshi hawapo wenye ujuzi na mafunzo ya kutosha. Itachukua miezi mingi kuwapa mafunzo vijana hao wa kuokoteza. Hivyo kusema M23 wakiamua kuingia Kinshasa waweza kufanya hivyo ingawa itakuwa ni vita kamili ambayo itawahusisha nchi zote jirani.
Akiongea juzi kwenye runinga ya taifa raisi Tshisekedi alisema kuwepo katika ardhi ya Congo DRC kwa majeshi ya Rwanda kwapelekea kutokea kwa matukio yasotarajiwa katika eneo lote la Afrika Mashariki.
Nini maoni yako?
Yote makundi haya yapigania sehemu zenye rasilimali khasa Goma na upande wa mashariki mwa Congo DRC, lakini huku mapigano yao yakiacha watu zaidi ya 200,000 bila makazi. Upande wa mashariki ndo ulio katika shida kuwa kwani ndiko vita inakopiganwa huku majeshi ya Congo DRC yakikabiliana na vikosi vya waasi na kufanya vitendo vya kinyama dhidi ya raia wa Congo DRC kama ubakaji, utekaji na mauaji.
Kukiwepo na aina hii ya mgogoro inakuwa shida kuitatua kwa kutokuwa na namna na kutafuta suluhisho hususan namna ya kuvikutanisha vikundi hivi vya waasi. Yasemwa kuwa nchini Congo DRC yapo makundi makubwa zaidi ya 50 ya waasi ambao wengi wapo upande wa mashariki mwa nchi hiyo ambako ndiko kwenye rasilimali nyingi.
Hali hii yaleta ukakasi kuwa ipi ni idadi kamili ya makundi ya waasi iliyopo ndani ya nchi ya Congo DRC.
Taarifa kadhaa za kiuchambuzi na kijasusi zilikusanywa kwa kipndi cha tokea miaka ya 2000 zimebaini kuwepo kwa makundi rasmi yafuatayo ambayo mengi yapo upande wa Kaskazini na Kusini mwa jimbo la Kivu na kaskaizni mashariki.
1. M23
2. ADF. NALU
3. Mai-Mai Group
4. Nyatura Rebels
5. CNDP
6. LRA
7. Raia Mutomboki
8. FRPI
9. FPLC
10. FARDC
11. MILIA
12. FDLR
Sasa leo kiongozi wa makundi yote ta waasi Corneille Nangaa akiongea na waandishi wa habari mjini Goma, amesema m23 kuichukua Goma si suala la utani na kwamba wapo hapo mazima na wataendeleza kampeni yao ambayo itawapeka hadi mji mkuu wa Kinshasa.
Mwaka 2012 M23 ilipouchukua mji wa Goma walikaa hapo kwa mwaka mzima hadi walipofurushwa na majeshi ya Congo DRC na nchi kubwa duniani ziliweka shinikizo kwa Rwanda kusaidia kuwaondoa waasi hao na pia kusitisha misaada.
Safari hii si Marekani, Uingereza, Ufaransa wala UN wanochukua hatua zozote isipokuwa kutoa kauli za hapa na pale.
Kinoonekana kwa jicho la tatu ni kazi kapewa mtu asafishe njia.
Nini Rwanda itaendelea kufanya?
Kwenye majukwa ya kidiplomasia Rwanda itaendelea kuwatumia wanadiplomasia wake kujibu hoja mbalimbali na uwezo huo wanao. Tayari balozi wa Rwanda katika UN azijibu na kipangua hoja mbalimbali na hivyo kufanya kazi ya kuikosoa Rwanda kuwa ngumu kidiplomasia.
Kijeshi Rwanda bila shaka sasa hivi imesogeza ulinzi wake hadi Goma na eneo hilo litakuwa ndo Buffer ne mpya ya kujilinda na aina yoyote ya mashambulizi kutoka Congo DRC.
Je, Raisi Tshisekedi anafikiria nini.?
Raisi Tshisekedi ameamuru kukusanya vijana zaidi ili wajiunge na jeshi la Congo DRC maana wanajeshi hawapo wenye ujuzi na mafunzo ya kutosha. Itachukua miezi mingi kuwapa mafunzo vijana hao wa kuokoteza. Hivyo kusema M23 wakiamua kuingia Kinshasa waweza kufanya hivyo ingawa itakuwa ni vita kamili ambayo itawahusisha nchi zote jirani.
Akiongea juzi kwenye runinga ya taifa raisi Tshisekedi alisema kuwepo katika ardhi ya Congo DRC kwa majeshi ya Rwanda kwapelekea kutokea kwa matukio yasotarajiwa katika eneo lote la Afrika Mashariki.
Nini maoni yako?