Kipa Gani wa Simba mkali zaidi kuliko wote tangu -labu ilipoanzishwa?

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
Simba imekuwa na makipa wengi sana, lakini sijui yupi ni mkali zaidi kwa uhodari wa kudaka?
Kina Mambosasa tumezisikia sana sifa zao, Idd Pazi, Mwameja, Kaseja, etc.
Nia na dhamira yangu ni kufanya jamii ya Watanzania ianze kuwathamini na kuwaenzi wachezaji wake.
 
hata mimi kwa umri wangu duniani kipa bora niliyemuona simba ni mohamedi mwameja ingawa kuna wengine wanapinga hebu wale kaka na dada zetu pia si vibaya wakitumwagia wasifu wa wale wa kale ka kina mambosasa na mahadhi
 
inasemekana athumani mambosasa ndiye
aliyekuwa kipa bora kuliko wote nchini toka
wakati huo hadi sasa. wenye data za
kuongeza ama kupunguza hayo tunaomba
msaada tutani. pichani mambosasa akifanya
vitu vyake siku ya yanga na simba uwanja
wa nyamagana, mwanza, mwaka 1974
(samahani sio 1994) mbele ya kitwana
manara popat wa yanga huku beki mkali
shaaban baraza wa simba sc akihakikisha
hakuna linaloharibika.
 
Iddi Pazi alikuwa bora lakini hakuna kama Omar Mahadhi bin Jabir
 
Reactions: Mbu
Omar mahadhi Bin Jabir ndio kipa pekee wa Tanzania aliyeichezea timu ya wachezaji nyota wa Afrika nzima enzi hizo. Walikwenda wawili, yeye na Maulid Dilunga wa Yanga. Hao wachezaji ingekuwa sasa, wangeweza kuichezea timu yoyote ya ligi kuu za Ulaya na wangekuwa nyota.
 
Athumani mambosasa ingawa alikua na sifa ya udokozi!
 
nakuunga mkono huyo kipa mahiri kushinda woote waliopata kuwepo msimbazi
 
Omar Mahadh. Ila wangenigundua nikiwa dogo mngekuwa mnanitaja leo hii
 
Wekeni clip zao hapa tuone wengine hatukuwepo kipindi hicho.
 
Hakuna kama Mambosasa lakini jamaa alikuwa anapenda pochi sana hivyo ilikuwa rahisi kumnunua, alikuwa ana tamaa ya ajabu. Ila siku alizokuwa akiamua kufanya vitu vyake basi ilikuwa unafurahi na roho yako. RIP AM.
 
Wekeni clip zao hapa tuone wengine hatukuwepo kipindi hicho.


...Omar Mahadhi 'Bin Jabir' ni huyo wa pili kulia!...mnyama mkali miaka hiyo, mnamuona Moh'd Bakari 'Tall', Abdallah 'King' Kibaden, Abdallah Mwinyimkuu, Adam Sabu, Abubakar Salum 'Bruce Lee,' etc...
 
Reactions: BAK
Omar mahadhi bin Jabir....Sijui kama ipo mtandaoni,ila angalia mechi ya simba na Vita.Niliiona kwenye kideo a long time ago,lazima kuna taasisi inayo hiyo video.
 
Wewe unajua soka. Omar Mahadh Bin Jabir atabaki kuwa top goalkeeper in the history of soccer ya Tanzania
 
tangu -labu ilipoanzishwa?
Hii survey sio ya kiufundi. Kuna mtu hapa amewahi kuwaona wote "tangu klabu ianzishwe?"

Mimi sijawahi, nimeanza na era ya Moses Mkandawile na kuendelea, hivyo siwezi na sitakiwi ku comment kuhusu kina Mambosasa na Mahadhi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…