Kipi bora kati ya kilimo na ufugaji?

Kipi bora kati ya kilimo na ufugaji?

Mrimi

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2011
Posts
1,691
Reaction score
640
Nimekaa hapa leo nikawa najiuliza ni kipi bora kati ya kilimo na ufugaji..nikawa nafikiria kufuga n'gombe wa kienyeji ambao kimsingi wana soko kubwa hapa nchini..changamoto kubwa kwa haraka haraka ni uendeshaji;hasa eneo la kutosha la kufugia na malisho..lakini pia majira ya kiangazi kunakuwa na shida sana ya malisho na hasa ukizingatia kwamba hawa jamaa wanachelewa sana kukua..kuhusiana na magonjwa sikuona kama ni changamoto kubwa sana..

Kuhusiana na ng'ombe wa kisasa nikawa nafikiria je,nifuge wa nyama au maziwa? Nikajaribu kuangalia soko la maziwa lipo japo ktk eneo ninaloishi bei ya maziwa si nzuri..kwa hiyo nikaona kama output ni ndogo relatively to input..ng'ombe wa nyama wa kisasa soko lipo..ila changamoto ni namna ya kupata mbegu bora na eneo na gharama za chakula..

Nikageukia kilimo,hasa cha mazao ya chakula..changamoto kubwa ni bei ya soko na mabadiliko ya hali ya hewa..hapa eneo la kulima halikuwa changamoto sana na hata gharama za uzalishaji sikuona kama ni tatizo sana kwa kuanzia..

Wazo langu la ufugaji lilikuwa nianze kwa kununua ndama 20 kwa kuanzia halafu nikomae nao hadi baada ya miaka 3 nione nitakuwa nimepata nini..then kama mazingira yakiruhusu niongeze tena wengine..

Baada ya kutafakari sana nikajikuta kama nimeishafeli hata kabla ya kuanza! Ndipo nikaona nipite mitaa hii nipate uzoefu kwa wengine..na ktk hili nahitaji kufahamu kama nitawekeza kwa mfano tsh 20mil..ktk aidha kilimo au ufugaji ng'ombe,je baada ya hiyo miaka 3 ni wapi penye unafuu na maslahi zaidi?
 
Lima mahindi na maharagwe.Fuga nguruwe na kuku

Mkuu sehemu ninayoishi hakuna soko zuri kwa vitu hivi..tena nguruwe ndio kabisaa..labda kuku wa kienyeji..
 
Kama unahitaji pesa ya haraka zaidi nakushauri ulime hasa yale mazao yenye demand kubwa kama maharagwe, mpunga, mahindi etc ila risk ni kubwa kwasababu ya matatizo ya hali ya hewa, magonjwa, kukosea kwenye timing etc.
Kama huna haraka ya pesa ya haraka na hupendi kutake risk kubwa chagua kufuga hasa ng'ombe wa maziwa, hela yako itarudi taratibu baada ya muda mrefu kidogo.
Ufugaji unahitaji mtaji mkubwa kidogo ila kilimo ukiwa na mtaji wa kudunduliza unafanikiwa.
 
Duuuh upo mkoa gani mkuu?

Mbeya,tukuyu.

Niliposema hakuna soko zuri naona kama umeshangaa kigogo..lakini kama ni kuuza tu mradi umeuza nawezasema soko lipo..lakini kibiashara,siyo..

 
Duuuh kumbe upo home kabisa,sasa hapo ndo safi kwa ufugaji wa nguruwe na soko kubwa liko dsm.tukuyu chakula cha mifugo ni kingi tena bei chee kabisa.fanya hiyo kazi kijana utaona mabadiliko.
 
jamani mifugo yote mnafuga mbona Panya hamuweki sasa ivi wateja ni wengi Aswa ndugu zetu wa Kichina ni wateja wazuri tu
 
Mbeya,tukuyu.

Niliposema hakuna soko zuri naona kama umeshangaa kigogo..lakini kama ni kuuza tu mradi umeuza nawezasema soko lipo..lakini kibiashara,siyo..

sogea usangu ukapige mpunga kwenye mashamba ya shirika. baada ya 3yrs utakuwa vizuri.
 
Mbeya,tukuyu.

Niliposema hakuna soko zuri naona kama umeshangaa kigogo..lakini kama ni kuuza tu mradi umeuza nawezasema soko lipo..lakini kibiashara,siyo..

Kwani lazima uuzie hapohapo? Mbona Japan wanatengeneza magari yanakuja kuuzwa Africa? Jiongeze mkuu.
 
sogea usangu ukapige mpunga kwenye mashamba ya shirika. baada ya 3yrs utakuwa vizuri.
Mkuu avatar yako imenifanya nitoe machozi kwa kicheko, daaah! Jf bana raha sana.
 
Back
Top Bottom