Kipi bora kati ya miembe ya kisasa na mitiki?

Kwanza nakupongeza mkuu kwa mawazo mazuri maana umechagua kilimo kizuri cha miti.
Miti ni faida.. Kukushauri kutokana na maelezo hapo juu, cha kwanza kama umebainisha vema kilimo cha aina mbili zote yani, kuanzia mtaji, mahali ama mazingira ya kustawi, uendelezaji na utunzaji. Meona chochote kati ya miembe na mitiki, kitakulipa. So option niwewe kuona wapi factors hizo hapo juu, nilizotaja zitakuwa strong ama kwa miembe au mitiki.
Then ukianza ni miembe basi faida utakayopata ndani ya muda huo ulokadiria ama kwa vipindi kadhaa vya mavuno, itakusaidia kupata fedha ama mtaji wa kuwekeza kwa mitiki, kwa kununua ardhi heka zingine kadhaa na kuendelea na kilimo cha mitiki. Pia ukianza na mitiki ikianza kustawi, vema kama ulivyosema hapo juu kwamba unaweza kupata mkopo kutoka benki kwa kutumia miti kama amana, then utaweza kopa kwa ajili ya shamba la miembe ambayo itakupa faida kwa muda mfupi ikiwa mitiki unaendelea kusubiri hivyo pia faida kutoka miembe utalipa benki taratibu. Baada ya miaka 20 kula faida ya miti.
 

Mawazo chanya,nami nazichanga nipate ardhi kwanza.
 
Dah ni kweli mkuu kichange ili usiwarithishe watoto umaskini km tuliorithishwa baba zao
 
Mkuu hili swali lako mbona sijalielewa?una maana kuna specie ya mtiki ambayo ni white?
 
Maembe kwanza then mitiki. ..maembe utavuna kila mwaka ila mitiki Sina uhakika
 
Mku nakushauri lima maembe kwani MItiki sio chini ya Miaka na tano mpaka ushirini japo mitiki ina fedha zaidi tatizo muda
 
Mie ningekuwa ni wewe ningeshauri maembe tu kwa kweli.utaendelea kuyavuna kwa miaka na miaka,



Labda kwa vile sifahamu vizuri kuhusu mitiki,
Hata mimi ningekushauri unge deal na miembe ingawa sijui soko linakuaje,ila itakuwa inalipa tu..
 
Nimelipenda swali lako na kwa upande wangu naona kwanza inatakiwa kuangalia mazingira au eneo unalotaka kuwekeza kwa faida nikimaanisha kama eneo unalotaka kuwekeza ni zuri kwa maembe basi panda maembe vivyo hivyo kwa mitiki.

Pili ni muhimu kupata kufahamu zaidi juu ya changamoto zinazoweza kujitokeza utakapo anza uwekeza. Hili lazima liangaliwe kwa pande zote yaani kuanzia shambani, sokoni na pia kwa wadau kama serikari na watu binafsi juu ya mipango endelevu na sera za mazao husika.

Otherwise nakushauri kukutana na wakulima wengine kupitia online platform kama ya MitiBiashara
Miti Biashara ambayo inamajadiliano mengi juu ya kilimo cha Miti.
 

Attachments

  • favicon.png
    5.8 KB · Views: 68
Shukrani sana mkuu kwa ushauri wako mzuri.
 
Hata mimi ningekushauri unge deal na miembe ingawa sijui soko linakuaje,ila itakuwa inalipa tu..
Asante sana nitalifanyia kazi mkuu najaribu nifanye division ya eneo nikate eneo dogo nipande miembe kwa ajili ya kutafutia nguvu ya kuhudumia hii mitiki maana miembe ni muda mfupi inaanza kuzalisha tofauti na mitiki ambayo inakaa muda mrefu
 
Ushauri mzuri
 
Kilimo cha mitiki kinakubali Kigoma wilayani Kakonko?
 
Mkaritusi ni mti wa mbao wenye faida ya haraka kulikn mtiki kwani ndani ya miaka 2.5 unaweza kuanza kuvuna. Watafute wakala wa misitu ujifunze kuusu hii miti. Tafuta tifori kwenye website.
Safi hii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…