Kipigo cha mbwa koko Sumbawanga

Kipigo cha mbwa koko Sumbawanga

mapesa yamejaa

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2021
Posts
1,412
Reaction score
3,419
Mzee mmoja aliyejulikana kwa jina moja la Manase amepokea kipigo kutoka kundi la vijana wamachinga hapa mjini Sumbawanga. Nikiwa nimetulia zangu hapa kwenye biashara zangu za madafu, mita kama 100 mbele yangu nikaona kundi linamkimbiza huyo mzee aliyevalia nguo za CCM huku akipigwa mawe na fimbo na wengine wanamrushia chupa za soda. Huruma ilinijia ikabidi niende kuamua huo ugomvi.

Cha kushangaza sababu niliyoambiwa ya kumpiga huyo mzee Manase ni kusifia awamu ya sita. Ana tabia ya kuwa akifika kwa wa machinga anaanza kuwaambia mama anaupiga mwingi mara oooh sasa hivi Nchi inalamba asali then anamalizia kwa kuwauliza au ninyi mnasenaje? Sasa vijana wanasema wamekuwa wakikereka sana na tabia yake huyo mzee.

Mimi nimeshangwazwa sana na tukio hili.yaani ndo tumefika huku kweli?. Pole sana Mzee Manase naamini unaendelea vizuri huko hosipitali.

Wasifiaji mjitathimini.
 
Mtanzania yeyote anayekataa kuwa mama haupigi mwingi huyo ni mwehu. Hivi hatuoni mabadiliko yanayotekea ndani ya kipindi hiki kifupi?, Ishu ya mfumuko wa bei ni dunia nzima mimi nipo mpakani mwa Tanzania baadhi ya bidhaa Tanzania ni nafuu kuliko majirani ila ukweli nikuwa tulishazoea kufokewa tu.
 
Wapumbavu hao, polisi wakamate hao wajinga na kuwaadhibu kisawasawa

Wafuasi wa Magufuli ndio wanaopenda vurugu, ni cancer kwa hii nchi

Kipindi cha Magufuli walikuwa wakipiga hata kuua wafuasi na viongozi wa upinzani kisa tu kumkosoa kiongozi wao ambaye walikuwa wakimuona kama mungu

Leo hii mungu wao kafa, Samia ana mtazamo tofauti, wanashindwa kuvumilia wanapiga tena wafuasi wa chama chao
Huu upumbavu hauwezi kuvumiliwa, hawa vibaka ni wa kupiga kisawasawa hadi wajifunze kuwa siasa sio mabavu na vurugu bali ni hoja

CCM kazi kwenu huu wenda wazimu mliufuga nyie
 

Attachments

  • IMG_20220405_210521.jpg
    IMG_20220405_210521.jpg
    37.9 KB · Views: 9
Back
Top Bottom