Kipimo cha HIV rapid test kipo accurate kwa kiasi gani?

Quezon

Member
Joined
Mar 21, 2014
Posts
42
Reaction score
18
Baada ya kufanya ngono isiyo salama kwa miezi takribani isiyopungua sita huko nyuma, mwili ulianza kutokuwa katika hali yake ya kawaida, nimekuwa na homa za mara kwa mara miezi yote hyo, kichwa kuuma, fatigue na mbaya....(simu ilizima charge sikuweza kumaliza thread yangu) ...zaidi kuna vipele vinavyowasha sana vingi vingi maeneo ya tumbo, bega, shingo na hata kiuno nikidhani mkanda wa jeshi(herpes zoster)... lakini cha kunishangaza hasa mpaka kuuliza accuracy ha hicho kipimo, ni siku ya jana nilienda pima HIV na kupewa majibu kuwa ni NEGATIIVE!!!!!!!!!!!!!!
 
Weka namba tuanze kutuma rambirambi zetu.

R.I.P in advance.
 
Hahaha. Pole mwaya. Nenda kwa washauri nasaha, utafanyiwa rapid test na baada ya hapo ikihitajika utafanyiwa Kipimo kingine (Elisa)
 
Hahaha nenda kapime!! Wakati mwingine mawazo yanaweza yakafanya mwili ureact kulingana na unavojindanganya kichwani...
Mtu anayejua kua ana UKIMWI ana proba ya kufa haraka sana kuliko mwenye nao lakini hajui sababu alivotwist mind yake...
Mfano, kuna wagonjwa wengine hospitalini hua wanapewa vidonge wakiambiwa watumie watapona, ila ukweli vile vidonge ni sukari tu ya kawaida uliyoizoea, sema wanakua na yale mawazo na mwili unareact hivo.. Hii nliisoma kwenye kwenye psychology! ni kitu ambacho ts real.. Kwa nini ufanye rapid test huku unajua kabisa ukikuta uko safi bado moyo wako utakua unasitasita kama ambavo huamini hicho kipimo hadi ukaja hapa kuuliza...

Home zisikutishe! nenda kapime ujipange vzr... ukishapima ukajikuta uko safi kwanza utakua makini nxt time..
Tumia condom au acha kabisa
 
Awe mkini au atumie kondomu,,hvi kweli kondom ina uhakika kukinga virusi?,mfano tunaweza kukuambia vaa kondomu fanya uzinzi na huyu mwanamke mwenye ukimwi,utakubali?
 
...zaidi kuna vipele vinavyowasha sana vingi vingi
maeneo ya tumbo, bega, shingo na hata kiuno
nikidhani mkanda wa jeshi(herpes zoster)... lakini
cha kunishangaza hasa mpaka kuuliza accuracy
ha hicho kipimo, ni siku ya jana nilienda pima HIV
na kupewa majibu kuwa ni NEGATIIVE!!!!!!!!!!!!!!
 

Kapime kile kipimo cha mwisho kinaitwa yugoti sijui kama nimepatiaaaa
 
Kapime kile kipimo cha mwisho kinaitwa yugoti sijui kama nimepatiaaaa

Inaitwa Un-gold, kama determine ni negative hana haja ya kupima hicho otherwise asubiri miezi tena 3 arudie.....mkanda wa jeshi unaweza pata hata kama hauna HIV,IDS japo ni mara chache sana
 
Hahaha!!! unanikumbusha miaka ya hapo nyuma condom ilipasuka nikiwa kwenye shughuli, jameni ilinitia hofu sana. Nilikua naogopa kwenda kupimwa, na kila nikipata homa ama mafua nilikua najiambia basi ndio hiyo ngoma inataka kuanza. Upele kidogo tu ulikua unanitia wazimu.
Yaani kwa kifupi nataka kusema, vyema uende upimwe vizuri na kuhakikisha halafu utatulia kimawazo.
Hatimaye niliamua kupimwa na nikabaki kucheka nikikumbuka nilivyohangaika wakati kumbe niko negative.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…