Kipimo cha malaria kimenipa wasiwasi

chardboy77

Member
Joined
Aug 5, 2013
Posts
53
Reaction score
5
Aisee wataalamu wa afya habari za saa hizi.

Nimeenda zahanati kupima malaria leo lakini wamenitoboa mara nne damu inakataa kurun kwenye hicho kipimo hadi ikabidi nikapime kwenye kipimo cha zamani cha microscope. Naombeni msaada wa kitaalamu kama inawezekana tatizo lipo kwenye damu yangu au ni vipi.
 

wasiwasi wako ni majibu ulopata baada ya kupima au ni kwa mashine kukataa kupima damu yako, je mashine ilivyo kataa daktari alisema shida ni nini, sisi tutakushauri vipi wakati hatujui mashine ilivyokataa ilitoa error gani. Kisha bado hujatuambia aina ya mashine iliyotumika.
 
Mkuu kipimo cha mRDT cha kupima Malaria kina mapungufu mengi.


Huenda buffer iliyotmika imekwisha muda wake au kipimo hicho ni kibovu kutoka kiwandani.


Kipimo cha Giemsa stain kitabaki kuwa kipimo bora kwa kupimia Malaria.

Ondoa shaka mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…