Kipindi cha FROM ME TO YOU.

Sikonge

JF-Expert Member
Joined
Jan 19, 2008
Posts
11,584
Reaction score
6,136
Miaka ileee, kulikuwa na kipindi cha From Me To You. Nimeona tujikumbushe na baadhi ya miziki iliyokuwa ikipigwa enzi hizo kwenye hiyo idhaa ya FM. Nakumbuka walioanza kuja na redio nzuri zenye kudaka FM (By the time ni akina technics, Sansui, JVC etc) basi ilikuwa unaifaidi hii miziki kama vile unatumia CD kwa leo.

Ila kwa kuanzia, nimeona niweke hawa akina mama wenye sauti zao. Mwanzo nilikuwa nafahamu wimbo wa "Stay in my corner by Patti Labelle" kuwa ndiyo wenye longest note. Yaani huyu mama anavuta sauti hadi unafikiri ni kifaa. Ila nimekuja kusikia kuwa kumbe kuna waliokuwa wakimzidi. Hebu wasikilize na wewe uamuwe ni yupi wamvulia kofia.

Nasikia huwa kuna ufundi wa kuimba na kupumua. Sijui kukoje huko.....

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=Bxh0_tD40A8[/ame]

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=H_jnASqj3xk&feature=related[/ame]


Kurudi kwenye kichwa cha habari, nianze kwa wimbo huu niupendao sana sana maana huyu mama Gladys na kisauti chake kama kinakwaruza kwa kweli huwa kinanimaliza sana sana.....

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=EE9KT_dU_R8[/ame]
 
Ngoja niongeza mingine miwili:

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=B0lpityVOiE[/ame]

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=PR6rX94bXJw[/ame]
 
Libeneke linaendelea:

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=t-JQQ1e35lQ[/ame]

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=tEUP8uVwvBw[/ame]
 
Da! Kumbe watu wa enzi zile tupo wengi tu! Sansui Disco...unanikumbusha mbali when life was simple, real and funtastic!
 
Da! Kumbe watu wa enzi zile tupo wengi tu! Sansui Disco...unanikumbusha mbali when life was simple, real and funtastic!

Enzi hizo mtu ndani akiwa na vitofali vimefungiwa kwenye kabati lenye mlango wa kioo na juu turn-table basi wewe unaishi high life....



Itakuwaje kipindi cha 'From me to you' bila huu wimbo hapa chini???

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=Wtte8ns0_2w[/ame]
 
Yep yep,

Nipo tena na nyingine mbili kutoka kwa Marehemu Marvin Gaye.

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=GVTN5o9Kgu8[/ame]

Huu mwingine niliambiwa tu kuwa miaka ya 75 hakuna party bila ya huu wimbo. Kipindi hicho hizi nyimbo kwangu zilikuwa NOT REACHABLE. Nimewawekea LIVE, ambao ukiangalia ni lini, unaona kabisa ni siku zake mwisho kabla hajatutoka.

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=s7eTOnNBwYU[/ame]


Kwa nyongeza natoa kibao cha Freddy Jacksons. Kwa vijana wapya, huyu jamaa hana uhusiano na familia ya akina Michael Jacksons. Kama humfahamu na unapenda Soul Musics basi poteza dakika kadhaa umfahamu huyu jamaa.... Wengine watafuata NEKISITI time.

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=DD4_BD2enEA[/ame]

[ame="http://www.youtube.com/watch?v=DD4_BD2enEA"][/ame]
 


Mkuu kumbe na wewe ni mjuzi namna hii. Yaani umenikumbusha zama zile bwana. Vitofali vifichwa kwenye kabati, basi una vi LP vyako kadhaa, aah, maisha yalikuwa raha tupu.

Ngoja nikukumbushe hii

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=tSNWeXGZMcU[/ame]
 
Unamkumbuka huyu dada na kibao chake hiki?

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=mMkyZAZNuHA&feature=related[/ame]

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=n205XdtNnYg&feature=PlayList&p=7318CDF8BDEA4BB0&index=0&playnext=1[/ame]
 
Da! Kumbe watu wa enzi zile tupo wengi tu! Sansui Disco...unanikumbusha mbali when life was simple, real and funtastic!

Debe za pale Sansui zilikuwa si za kawaida. Namkumbuka demu mmoja alikuwa moto wa kuotea mbali basi kila akiinuka kwenda kucheza mimi nilikuwa sichezi ili nimuangalie uchezaji wake maana alikuwa anajua sana kuziruka nyoka yaani alikuwa ni kiboko sana. Enzi zile maisha yalikuwa poa sana na Tanzania hatukuwa na mafisadi kama ilivyo leo hii.
 
MaxShimba you must be a good DJ of those days particularly 1988-90's Congratulations.

When will we celebrate as JF family? When the support is there i prefer you to be a Music director of that particular function.

Big up you reminded me something so special !!
 

Wakati ule nilikuwa pale Helenic Club na Chuo Kikuu, ilikuwa kazi sana. XTC nilikuwa naumiza every other weekend.
 
Maxshimba,
Huyo Colonel Abraham leo hii nina single yake lakini Vynil. Nilikuwa namhusudu sana sana. Maadamu umenipeleka huko, basi ngoja nikupe wapinzani wake enzi hizo....

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=pbV94YodhRg[/ame]

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=DVe0o6lRgcY[/ame]

Miaka ya 80 mwishoni nakumbuka kulikuwa na caseti moja sijui DJ gani alirekodi na karibu Tz nzima walikuwa na copy hiyo. Ilikuwa wimbo wa SOS band huo juu unaanza na wakati unaishia unaanza kusikia "touch touch...." na hapo unafahamu Midas Touch linaingia hilo. Na mwisho inakuja Colonel Abrams - Speculation.

Nilikuwa na mshikaji wangu akiitwa David K. alikuwa akinikusanyia "vigongo" kutoka kwa Dj mmoja mkali hapo Dar na anakuja kurekodi home Ilala.
 
Nyie watu mnamkumbuka Jefrey Daniel wa SHALAMAR wakati kaletwa Soul Train? Ilikuwa ukienda studio za video za wahindi, kama hawana Soul Train, basi tena huchukui kitu. Hawa jamaa walifanya maholi yote yawe yanacheza kama hawa jamaa wanavyocheza hapa chini........ Jamani, nyingine ntaendelea kutuma taratibu. Muwe mnapitia hapa time to time...

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=6cajy5WSDd0[/ame]

Wimbo huu pia ulikuwa unaniuwa sana. Hawa ni vijana wa New Edition. Kwa vijana ni kuwa hili kundi baadaye alijiunga Johnny Gill.

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=MMreX-6n9XE&feature=fvw[/ame]

Hawa jamaa walianza watoto sana kama inavyoonyesha video hapa chini. Nafikiri walianza na kibao cha Candy Girl na sauti za kitoto sana. Wamekuwa na huyo producer wa aitaye Silas hadi wakawa wakubwa. Na jamaa akawa akisema "inafurahisha kukaa na hawa watoto na kushuhudia wakibadilika from BOYS TO MEN. Mmoja wao ndiye aliyewagundua na kuamua kuwaleta hawa jamaa wa BOYZ II MEN huko Motown na wakawa wamepewa nick name ya New Edition. Hapa chini, huyo mwenye mkufu mkubwa na kama sikosei umeandikwa BOBBY, ndiyo Bobby Brown ambaye alikuja akamuowa bibie Whitney Houston....... Du kweli youtube inatunza history. Vijana enzi hizo kufuga nywele nyuma wanasema "PUSH BACK" na Tshirt isiyo na mikono wanasema "CAR WARSH", na viatu vya Matairi twaita "kata mbuga".

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=pYgxifjHsb8&feature=fvst[/ame]
 
Mkuu, ninamkumbuka sana. Wakati ule Soul Train unachanganya kidogo na Robot, ahh, basi unaumiza ile mbaya.
 
Mkuu ngoja nikuumize roho, unamkumbua Mtume na ile juicy fruit? Nilikuwa natokwa machozi na huu mwimbo.

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=VPEx8Gsa0XA[/ame]
 
Point of No return nilikuwa naupenda sana sana. Huyo dada Gwen G. nilikuwa simfahamu ila baadaye nikaja nikagundua kumbe aliimba aliimba wimbo huu chini na Peter Tosh. Na sisi Tosh, Don Williams, Dolly Parton, Shalamar, Hot Chocolate, Cliff Richards, Jimmy Cliff ...... walikuwa ni watu wa lazima wawepo home

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=XOAxvIME0i0[/ame]

Hii ni yangu ya mwisho na baadaye narudi kwenye nyimbo za From me to you type.

Hawa jamaa walitamba sana na hiki kibao chao enzi za breakdance. Hii ilikuwa ni kipande cha film ya Electric boogalow (breakdance). Original band waweza kuiona kwenye YOUTUBE maana ipo wakiimba live.
Nakumbuka watoto wa Dar walikuwa wakiimba "Michael Jackson njoo, SITAKIII, kama hutaki nenda...."

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=8x5JqZNYpRQ[/ame]

Nasubiri zeny wandugu zangu. Bye bye....
 
Mkuu unakumbuka kila mtu alikuwa na push back?

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=jE7k--0o1kM&feature=related[/ame]
 
Mkuu ngoja nikuumize roho, unamkumbua Mtume na ile juicy fruit? Nilikuwa natokwa machozi na huu mwimbo.

http://www.youtube.com/watch?v=VPEx8Gsa0XA

Ehh bwana wee. Nilipata shida sana kuupata wimbo huu. Kaka yangu sijui alizitoa wapi hizi nyimbo. Basi niliposikia wimbo wa Juicy wa Notorius BIG, kwenye album ya READY TO DIE, nikakimilia mara moja. Beats zake wamekuja kuchukua watu wengi sasa. Kuna jeniffer Lopez na wengine wengi. List ni ndefu sana. Hebu angalia mwenyewe:

http://en.wikipedia.org/wiki/Juicy_Fruit_(song)

Max, nilimsahamu MKONGWE kabla sijamaliza. Ila atakuja tena katika slow wiki lijalo.
Kwa vijana, huyo Mzungu ni Michael Douglas, mume wake Catherine-Zeta Jones na wote watatu ni Wacheza film wa Hollywood.... Kathleen Turner na Danny Devito. Ila naona kuna kalufundi hapa maana mpiga saxophone kwenye Video Original ni Devito na si huyo jamaa anayeonekana akipiga hapa.

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=fm4UWfyrEmQ[/ame]
 
Hii nilikuwa na 12 inch yake, ahh wacha tu

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=gtdPMoX2iws[/ame]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…