nilimuona mohammed ali mombasa karibi na blue room CBD alikua ywanywa maji ya barafu nje ya duka flani, jamaa anatembea tu pekeyake kama mtu wa kawaida bila wasi wasi
kuna wakati flani ma officer wa NIS walikua wanapenda kufwata fwata kwani kuna wakati mmoja alihoji hata wafwasi wa alshabaab waliojificha ndani ya pwani la kenya, alafu zile ripoti hua anavumbua serikali hua wanataka kujua kinanani(whistleblowers) hua ana leak infomation kwake .....
jamaa hana uoga kabisa! mpaka sikuhizi naona serikali imebidi haina budi kumwacha tu, wakimshika hawawezi mpeleka kotini manake kama mwanahabari ako na haki, wakimuua wanamfanya shahid(martyr) na wengine wengi zaidi wataamka kufwata nyayo zake , besides ako na wafwasi wengi sana kenya nzima, itakua ni hatari sana kwa nchi nzima , kunaeza kua na ka revolution sasa hivi... inabidi wamfwate fwate wakitafuta kamakosa kadogo ili walazimishe stetioni kama KTN imfute kazi, Lakini sikuhizi video zake pia huenda aljazeera mbali na KTN sasa hashikiki, hauliki, hafutiki... naona hata serikali ilichoka naye