Kipindi cha kubeba mimba baada ya operation

Maysally

Member
Joined
Dec 6, 2013
Posts
54
Reaction score
21
Habari wana jf!naomba kuuliza mwaka jana nilijifungua kwa operesheni nikakosa mtoto ilikuwa jan 17 sasa nimetimiza mwaka nina hamu ya mtoto sana kwani sina.lakini sitaki kuzaa kawaida nataka operesheni je muda gani muafaka?naombeni ushauri
 
Pole Maysarah mwambie mzee afanye kweli au msubiri dr MziziMkavu akupe maelezo kidogo muhimu
 
Last edited by a moderator:
1. Ni salama kwa sasa kwako kubeba mimba. So go ahead and make that beautiful baby.

2. Kuzaa kwa operation ni hatari zaidi kwako kuliko kuzaa kwa njia ya kawaida. Iwapo hakuna sababu ya kitaalamu ni vema ukazaa kwa njia ya kawaida.

3. Kwenye ujauzito kuna tabia ya historia kujirudia. Kama kuna tatizo lolote ulilolipata mara ya kwanza pata ushauri toka kwa daktari jinsi ya kuepuka lisijirudie tena.

Kila la heri...
 

Maelezo mazuri ZeMarcopolo ila point na.2 sio sahihi . Kuna usemi tunatumia once caesarean section then next delivery must be at hospital, hii ni kutokana na hatari iliyopo wakati wa kujifungua kwani tayari mji wa kizaza (uterus) una kovu litokanalo na operation ya kwanza. Hivyo inategemeana na sababu ya operation ya kwanza ilikuwa nn maana nyingine km njia ndogo (contracted pelvis) lazima atajifungua kwa c/s tena. Hivyo nenda hospital kajadiliane na dokta wako na ni nzuri kama mtaenda na mumeo/mwenza wako.
 

Sawasawa. Unachosema ni sahihi na ndio maana nikaandika "Iwapo hakuna sababu ya kitaalamu ni vema ukazaa kwa njia ya kawaida."
 

ataweza vipi kuzaa kawaida na anaweak scar( 17 jan 2013) mkuu?
 
Habari wana jf!naomba kuuliza mwaka jana nilijifungua kwa operesheni nikakosa mtoto ilikuwa jan 17 sasa nimetimiza mwaka nina hamu ya mtoto sana kwani sina.lakini sitaki kuzaa kawaida nataka operesheni je muda gani muafaka?naombeni ushauri

Unaweza kubeba ujauzito dada yangu , ila usisubirie mpaka uchungu ukushike ndiyo uende hospitali kwa kovu lako la kizazi bado ni dhaifu halitaweza kuhimili mikikimikiki ya uchungu wa ujauzito.........

wazo lako la kutaka kuza kwa operesheni ni zuri kama utapata mimba mapema iwezekanavyo,,,,,,,,,,,

ukipata ujauzito jadiliana na daktari wako na mpange mipango yako ya kujifungua mapema........

pole sana kwa kupoteza mtoto.
 
Nashukuru sana mliotumia fursa kunishauri.nimekuwa na wasi wasi kuzaa kawaida kwani hata njia ilikuwa haifunguki kipindi hicho mpaka nikafanyiwa caesar!nashukuru xana na pia kuanzia sasa nipo tayari kwa mimba.mana ndo kwanza nna mwaka kwnye ndoa.
 
Nashukuru sana mliotumia fursa kunishauri.nimekuwa na wasi wasi kuzaa kawaida kwani hata njia ilikuwa haifunguki kipindi hicho mpaka nikafanyiwa caesar!nashukuru xana na pia kuanzia sasa nipo tayari kwa mimba.mana ndo kwanza nna mwaka kwnye ndoa.

Kazana kumlisha mmeo vitu vyenye protein amwage mbegu imara.
 
Hivi watu, mnaochangia hapa ni madaktari au ni waganga Wa kienyeji? Acheni na madaktari wamsaidie huyu mama.
 
Naomba kuuliza.

Mwanamke ambaye amejifungua kwa C-section mtoto kwa kwanza anaweza kuzaa kawaida mtoto wa pili after 2 years?
 

Hapa naona unampotosha mama wa watu!

Jaribu kusoma tabia za uterine muscle kwa undani.

Theory ya weak scar ilivyokuwa inachukuliwa miaka ya zamani na ukweli uliogunduliwa kwenye new findings ni tofauti kabisa.

By the way, what is the definition of a weak scar? Can you diagnose weak scar kwa mgonjwa ambaye hujamuona???
 
Naomba kuuliza.

Mwanamke ambaye amejifungua kwa C-section mtoto kwa kwanza anaweza kuzaa kawaida mtoto wa pili after 2 years?

Yes ni salama zaidi kuzaa kwa njia ya kawaida iwapo lile tatizo lililosababisha afanyiwe SC hapo awali halipo.
 
Kama alijifungua kwa operation mwaka mmoja uliopita itambidi asubiri miaka angalau nitatu iti aweza kujifungua kwa njia ya kawaida, otherwise kizazi kinaweza kuchanika
 
Pamoja na ushauri wa wadau. Mchango wangu ni kama ifuatavyo. Kwanza ni lazima ujue sababu kwa nn ulifanyiwa c/s, je kulikuwa na complications zozote kama uterine tear, na kwann mtoto alikufa( pole). Lkn pia ni muhimu sana km nilivyosema awali nenda kwa obstetricians ww na mwenza wako mkapate ushauri zaidi juu ya hili maana sababu km cephalopelvic disproportion(cpd) uwiano wa kichwa cha mtoto na njia kutoendana, contracted pelvis, km una diabetes husababisha big baby hivyo kuicontrol kipindi chote cha ujauzito. Hivyo hata kama mtaamua kuzaa lzma mjadiliane na dokta wako juu ya delivery modality.Na kuzingatia sana kuhudhuria clinic kwa ajili ya vipimo km ultrasound kuangalia mji wa uzazi ulivyo, placenta imejiattach vp(to rule out kitu kinaitwa placenta praevia-kujiattach chini karibu na shingo ya kizazi,placenta inccreta (kujishikiza ktk misuli ya uterus sababu ya kovu la kwanza,nk). My take jadiliana na daktari wako kwanza tafadhari pamoja na ushauri wa wadau. Asante
 
Ukweli kama unataka kuzaa kawaida baada ya c/s (trial of labour) lazima uwe chini ya mikono salama ya madaktari na hospitali yenye vifaa kwa ajili ya dharura hasa hasa kuchanika kwa uterus husababisha kutoka damu nyingi (PPH) ni hatari sana hii kitu!
 
Kama alijifungua kwa operation mwaka mmoja uliopita itambidi asubiri miaka angalau nitatu iti aweza kujifungua kwa njia ya kawaida, otherwise kizazi kinaweza kuchanika

Hii umejifunza wapi? Aliyekufundisha hivyo amekudanganya au hana taarifa sahihi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…