KIDUNDULIMA
JF-Expert Member
- Aug 18, 2010
- 966
- 540
Kilavu ameyatoa majibu hayo wakati ajihojiwa jana TBC1 kuwa uchaguzi ni muhimu kwa rais, wabunge na madiwani. Hivyo suala la kusema kuwa mtu aliyeko nje ya kituo chake apige kura ya raisi halikubaliki na pia itakuwa ni vigumu kujua kudhibiti upigaji kura mara mbili eti watashindwa kujiua kama huyo mtu hajapiga kura kwenye kituo cha awali. kwa kweli mwaka huu wamedhamiria kuhakikisha wimbi la vijana ambalo limejiandikisha kwa wingi, ambalo hupenda mageuzi na ambalo huathiliwa na mfumo wa kubadili sehemu za kuishi kutokana na utafutaji halipigi kura.
wataalamu watusaidie ni kwa jinsi gani hili kundi lililohama hwa hiari au kuhamishwa kwa lazima baada ya kufungwa kwa maboresho ya daftari la wapiga kura linaweza kusaidiwa ili angalau liweze kupiga kura ya rais?
wataalamu watusaidie ni kwa jinsi gani hili kundi lililohama hwa hiari au kuhamishwa kwa lazima baada ya kufungwa kwa maboresho ya daftari la wapiga kura linaweza kusaidiwa ili angalau liweze kupiga kura ya rais?