Mhaya
JF-Expert Member
- Aug 20, 2023
- 1,831
- 5,489
Katika kisa cha kushangaza nimekutana nacho baada ya kuona Post instagram inayosema wazazi wamshtaki Mwalimu wa madrasa kwa kosa la kuwachapa watoto viboko jambo lililopelekea mwalimu huyo kukamatwa na polisi.
Katika kusoma kwangu comment nikakutana na maoni ya mtu mmoja yanasema kuwa Mtume Muhammad mwenyewe alibanwa mbavu kwa kushindwa kutamka maneno ya quran (kiarabu), sembuse hao watoto!
Hii comment ikanifanya niingie chimbo, kufatilia ni kwa nini mtume alipata kipigo kikali kwa kushindwa tu kusoma au kutamka maneno.
Katika sure ya Sahih al-Bukhari, imeelezwa kwamba alipojidhihirisha Malaika Jibril kwa mara ya kwanza kwa Mtume Muhammad katika Pango la Hira, alimuamuru "Soma" (au "Soma kwa sauti"). Mtume Muhammad, akiwa hana elimu ya kusoma, alijibu kuwa hawezi kusoma. Malaika Jibril kisha alimtia mikononi mwake kwa nguvu na kumbana na kurudia amri ya "Soma" mara tatu, kila mara akimshinikiza Mtume kwa nguvu zaidi. Mtume alielezea kuwa alijisikia kana kwamba anashinikizwa na kubanwa kwa nguvu kubwa hadi alihisi kama anakaribia kuzimia kwa kukosa pumzi.
Katika kusoma kwangu comment nikakutana na maoni ya mtu mmoja yanasema kuwa Mtume Muhammad mwenyewe alibanwa mbavu kwa kushindwa kutamka maneno ya quran (kiarabu), sembuse hao watoto!
Hii comment ikanifanya niingie chimbo, kufatilia ni kwa nini mtume alipata kipigo kikali kwa kushindwa tu kusoma au kutamka maneno.
Katika sure ya Sahih al-Bukhari, imeelezwa kwamba alipojidhihirisha Malaika Jibril kwa mara ya kwanza kwa Mtume Muhammad katika Pango la Hira, alimuamuru "Soma" (au "Soma kwa sauti"). Mtume Muhammad, akiwa hana elimu ya kusoma, alijibu kuwa hawezi kusoma. Malaika Jibril kisha alimtia mikononi mwake kwa nguvu na kumbana na kurudia amri ya "Soma" mara tatu, kila mara akimshinikiza Mtume kwa nguvu zaidi. Mtume alielezea kuwa alijisikia kana kwamba anashinikizwa na kubanwa kwa nguvu kubwa hadi alihisi kama anakaribia kuzimia kwa kukosa pumzi.