DALALI MKUU
JF-Expert Member
- May 7, 2022
- 2,011
- 4,705
TAMKO LA VIJANA WA ROMBO WAISHIO DAR ES SALAAM (VIWARO-DAR)
Umoja wa vijana wa Rombo waishio Dar es salaam, Ni chama Huru cha vijana waliotokea wilayani rombo Mkoani Kilimanjaro ambao wanaishi Dar es salaam. Umoja wetu kwa sasa una Jumla ya wanachama 4886
Chama hiki kilianzishwa Rasmi mwaka 2020 Kikiwa na lengo kuu la Kusaidiana na kushirikishana katika fursa mbalimbali zinazopatikana ndani ya Jiji la Dar es Salaam
Katika kikao chetu cha kawaida ambacho kimefanyika Jana, Pamoja na mambo Mengine tulijadili taarifa ya Mbunge wa Jimbo lA Rombo, Adolf Mkenda (CCM) Kuhusishwa na Tukio la ukiukaji wa haki za binadamu na matumizi mabaya ya Nafasi yake kwa yeye binafsi na taasisi anazoziongoza Kushirikiana na Jeshi la Polisi kumkamata Mwanaharakai na mchambuzi wa masuala ya Kijamii, Godlisten Malisa.
Tulijadili ka kina na taarifa hiyo kwa sababu Imegusa Jimbo letu, lakini inamhusisha kijana mwenzetu
Baada ya kuijadili kwa Kina Tumegundua kuwa Mbunge wa Jimbo la Rombo amekuwa akitumia nafasi yake ya Ubunge, lakini pia uwaziri kutesa,kudhalilisha na kuminya haki za watu wengi hasa wale wanaomkosoa, Na suala hili halijaanza tu kwa Malisa pale pia kuna matukio mengi likiwemo pia Tukio la kumlinda mfanyakazi wake Lucas tarimo aliyekuwa anatuhumiwa kumchoma kisu,Betrice.
Kufuatia Jambo hilo sisi kwa umoja wetu tunamtaka Mbunge ajitokeze Hadharani maara moja kutolea ufafanuzi wa taarifa hizo na uhsuika wake katika kesi hizo ambazo hata taarifa za uchunguzi kutoka Jeshi la Polisi Mkoani Kilimanjaro, zinzsema kwamba yeye pia alitoa amri kwamba Malisa asipewe Dhamana.
Pia kwa umoja wetu tumekubaliana kwa pamoja Kumsusisa Shughuli yoyote ya Mbunge Mkenda, kumkataa kwa vitendo kwa kuwashwishi pia hata wazazi wetu huko Wilayani Rombo kutompa ushirikiano Mbunge adolfu mkenda kutokana na vitendo vyake viovu vya matumizi mabaya ya madaraka
Hivi karibuni mbunge tulikutana nae Pale Msimbazi center na kutuhadaa kwa kutupa miradi hewa inayotekelezwa kule wilayani Rombo, kwa lengo la kujinufasha yeye binafsi kisiasa, Alitumia vibaya mkutano wetu wa wakazi wa Rombo kupenyeza ajenda zake binafsi za kisiasa.
Kwa hali ya kawaida tu haiwezekani Mbunge aalike madiwani, mkuu wa wilaya waje Dar es salaam kutukalisha msimbazi center et kuja kutueleza Kazi zilizofanywa na Rais kwa Kipindi cha miaka mitatu hii ni dharau ya hali ya Juu sana, wakati wazazi wetu klule Rombo wanateseka anataka kutuhadaa sisi kwa sahani ya ubwabwa.
Pamoja na mambo mengine tunaomba Chama cha Mapinduzi kutompa nafasi tena Ya kupepereusha bendera ya chama chake pale Rombo, lakini wananchi wa Rombo kumkataa na kutompa ushirikaino wa hali yoyote hadi pale atakapojitokeza hadharani na Kuomba Radhi wananchi wa Rombo.
Mwisho Chama chetu kinawaasa vijana war ROMBO na vyama vingine vya Rombo kukataa kutumiwa kisiasa na Mbunge Adolf Mkenda.
Imtetolewa na Shangali John Mremi
Katibu mtendaji VIWARO-DAR
June 09,2024
Umoja wa vijana wa Rombo waishio Dar es salaam, Ni chama Huru cha vijana waliotokea wilayani rombo Mkoani Kilimanjaro ambao wanaishi Dar es salaam. Umoja wetu kwa sasa una Jumla ya wanachama 4886
Chama hiki kilianzishwa Rasmi mwaka 2020 Kikiwa na lengo kuu la Kusaidiana na kushirikishana katika fursa mbalimbali zinazopatikana ndani ya Jiji la Dar es Salaam
Katika kikao chetu cha kawaida ambacho kimefanyika Jana, Pamoja na mambo Mengine tulijadili taarifa ya Mbunge wa Jimbo lA Rombo, Adolf Mkenda (CCM) Kuhusishwa na Tukio la ukiukaji wa haki za binadamu na matumizi mabaya ya Nafasi yake kwa yeye binafsi na taasisi anazoziongoza Kushirikiana na Jeshi la Polisi kumkamata Mwanaharakai na mchambuzi wa masuala ya Kijamii, Godlisten Malisa.
Tulijadili ka kina na taarifa hiyo kwa sababu Imegusa Jimbo letu, lakini inamhusisha kijana mwenzetu
Baada ya kuijadili kwa Kina Tumegundua kuwa Mbunge wa Jimbo la Rombo amekuwa akitumia nafasi yake ya Ubunge, lakini pia uwaziri kutesa,kudhalilisha na kuminya haki za watu wengi hasa wale wanaomkosoa, Na suala hili halijaanza tu kwa Malisa pale pia kuna matukio mengi likiwemo pia Tukio la kumlinda mfanyakazi wake Lucas tarimo aliyekuwa anatuhumiwa kumchoma kisu,Betrice.
Kufuatia Jambo hilo sisi kwa umoja wetu tunamtaka Mbunge ajitokeze Hadharani maara moja kutolea ufafanuzi wa taarifa hizo na uhsuika wake katika kesi hizo ambazo hata taarifa za uchunguzi kutoka Jeshi la Polisi Mkoani Kilimanjaro, zinzsema kwamba yeye pia alitoa amri kwamba Malisa asipewe Dhamana.
Pia kwa umoja wetu tumekubaliana kwa pamoja Kumsusisa Shughuli yoyote ya Mbunge Mkenda, kumkataa kwa vitendo kwa kuwashwishi pia hata wazazi wetu huko Wilayani Rombo kutompa ushirikiano Mbunge adolfu mkenda kutokana na vitendo vyake viovu vya matumizi mabaya ya madaraka
Hivi karibuni mbunge tulikutana nae Pale Msimbazi center na kutuhadaa kwa kutupa miradi hewa inayotekelezwa kule wilayani Rombo, kwa lengo la kujinufasha yeye binafsi kisiasa, Alitumia vibaya mkutano wetu wa wakazi wa Rombo kupenyeza ajenda zake binafsi za kisiasa.
Kwa hali ya kawaida tu haiwezekani Mbunge aalike madiwani, mkuu wa wilaya waje Dar es salaam kutukalisha msimbazi center et kuja kutueleza Kazi zilizofanywa na Rais kwa Kipindi cha miaka mitatu hii ni dharau ya hali ya Juu sana, wakati wazazi wetu klule Rombo wanateseka anataka kutuhadaa sisi kwa sahani ya ubwabwa.
Pamoja na mambo mengine tunaomba Chama cha Mapinduzi kutompa nafasi tena Ya kupepereusha bendera ya chama chake pale Rombo, lakini wananchi wa Rombo kumkataa na kutompa ushirikaino wa hali yoyote hadi pale atakapojitokeza hadharani na Kuomba Radhi wananchi wa Rombo.
Mwisho Chama chetu kinawaasa vijana war ROMBO na vyama vingine vya Rombo kukataa kutumiwa kisiasa na Mbunge Adolf Mkenda.
Imtetolewa na Shangali John Mremi
Katibu mtendaji VIWARO-DAR
June 09,2024