kisarawe secondary junior seminary majanga tupu!

Isaack Newton

JF-Expert Member
Joined
Apr 15, 2013
Posts
594
Reaction score
291
wanafunzi wa shule tofauti za dsm zimechoka na tabia ya wanafunzi wa kisarawe secondary.Wanafunzi wa kisarawe wanazidi kuiba mabegi na nguo za wanafunzi walioenda kwenye easter conference ktk shule hiyo.Baadhi ya wanafunzi wameamua kurudi makwao kwa sababu hawana chochote zaidi ya nguo walizo vaa! inashangaza sana wasichana wa kisarawe kuwaibie wageni wao hadi nguo za ndani!!!
 
Hii utafikiri sio Shule ya Kidini, Walutheri wajitahidi sana.
 

Bwana Yesu asifiwe mtumishi uliyeleta mada hapa. Kwanza nikupe pole kama limekukumba na wewe. Wizi upo sehemu zote duniani na kilichotokea hapo Kisarawe kinatokea sehemu nyingine yeyote yenye mkusanyiko wa watu wanye lengo moja, lakini kumbuka kuwa wapo wenye malengo tofauti. Simply mmeenda kwa conference ya UKWATA usidhani wezi hawapo. Mwizi ni mwizi anaiba chochote na akikosa cha kuiba anakuachia kinyesi. Mlichotakiwa kufanya ni kuimarisha ulinzi tu. Dont trust anybody! Suspect everybody! Pili, zameni kwenye maombi kama imani zenu ziko sawa sawa, hivyo vitu mtafidiwa na Mungu kama mlienda kwa nia nzuri au Mungu anaweza kutenda kabisa vikarudi. Ila kama mna mambo yenu pia hapo kila mtu achunge mzigo wake maana si wanaukwata wote wana woga wa Kimungu kiasi cha kushindwa kuiba chochote. Waliorudi nyumbani (kuchukua nguo nyingine) nawashauri warudi tena kisarawe wakapate neno la Mungu na kushiriki vipaji, nguo kitu gani mbele ya neno la Mungu.Pole na nikutakie Pasaka njema.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…