Kisulisuli charudi Jambiani

Kisulisuli charudi Jambiani

Jaji Mfawidhi

JF-Expert Member
Joined
Feb 20, 2016
Posts
15,835
Reaction score
23,776
Kisulisuli niache

Kisulisuli niache, Niache usinivute
Na sitaki nikufiche, Baadae unisute
Hao watu ni vicheche, Usinifanye nijute
*Kisulisuli niache* ,*Hao nawajua Mimi*

Walishindwa kujitunza, Kuheshimu miili yao
Ujana ukawaponza, Na wakakosa upeo
Sasa wamekuwa funza, Watafutao makao
*Kisulisuli niache*, *Hao nawajua mie*

Heri kumuoa punda, Abebe mizigo yangu
Kuliko kuoa ganda, Walilotupa wenzangu
Hakuna atayependa, Eti chetu kiwe changu
*Kisulisuli niache*, *Hao nawajua mie*

Kisulisuli wakumbushe, Ndoa sio makalio
Wala wasijibebishe, Na kutaka wenye vyeo
Wambie wasitutishe, Janja haijaanza leo
*Kisulisuli niache*, *Hao nawajua mie*

Wakiwa makanisani, Kama kuku chini ya mbawa
Wanaporudi nyumbani, Zaidi ya popobawa
Kuoa hatutamani, Punguzeni kuwa chawa
*Kisulisuli niache*, *Hao nawajua mie*

Kufunga ndoa hiyari, Moyo unaporidhia
Kama hatuko tayari, Mtaishia kulia
Mlijiona sukari, Cheki mnavyojutia
*Kisulisuli niache*, *Hao nawajua mie*

Ukiwa msichana, Maringo ni kama yote
Majibu yaso maana, Wanaume si chochote
Kutwa kushauriana, Eti ndoa si lolote
Wakishajaa laana, Wanaangaika kote
*Kisulisuli niache*, *Hao nawajua mie*

Wanaongoza kuroga, Kwa limbwata tuwe bwege
Kutufanya maboga, Kama kuku watufuge
Kisha wakapige soga, Kwa madawa watutege
Hawana hata uoga, Hao ndio vivuruge
*Kisulisuli niache*, *Hao nawajua mie*

Wasumbua wachungaji, Wazazi na viongozi
Eti haki wazihitaji, Miili ikiwa wazi
Heshima ndo mtaji, Na ndoa ni kama vazi
*Kisulisuli niache*, *Hao nawajua mie*

Mlioko kwenye ndoa, Msijione kama keki
Mkaanza kusumbua, Waume kutudhihaki
Na kaeni mkijua, Mfupa si mshikaki
*Kisulisuli niache*, *Hao nawajua mie*

Najua si kupenda kwenu, Ila ndo mjitambue
Tunzeni miili yenu, Someni mjiinue
Lindeni kilicho chenu, Hatua mjipigie
Msiishi kwa fununu, Badae mtusumbue
*Kisulisuli niache*, *Hao nawajua mie*


*Ujumbe*

Kisulisuli si dawa ya ndoa, bali tuwafundishe vijana maadili,kuwasisitiza kuwajibika na kuwaandaa kwaajili ya ndoa, Kisha tuwakumbe kuwa ndoa si rahisi kama wanavyofikiria.
 
Kisulisuli niache*

Kisulisuli niache
Niache usinivute
Na sitaki nikufiche
Baadae unisute
Hao watu ni vicheche
Usinifanye nijute
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua Mimi*


Walishindwa kujitunza
Kuheshim mili yao
Ujana ukawaponza
Na wakakosa upeo
Sasa wamekua funza
Watafutao makao
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*

Heri kumuoa punda
Abebe mizigo yangu
Kuliko kuoa ganda
Walilotupa wenzangu
Hakuna atayependa
Eti chetu kiwe changu
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*


Kisulisuli wakumbushe
Ndoa sio makalio
Wala wasijibebishe
Na kutaka wenye vyeo
Wambie wasitutishe
Janja haijaanza Leo
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*

Wakiwa makanisani
Kama kuku chini ya mbawa
Wanaporudi nyumbani
Zaidi ya popobawa
Kuoa hatutamani
Punguzeni kuwa chawa
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*

Kufunga ndoa hiyari
Moyo unaporidhia
Kama hatuko tayari
Mtaishia kulia
Mlijiona sukari
Cheki mnavyojutia
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*

Ukiwa msichana
Maringo ni Kama yote
Majibu yaso maana
Wanaume si chochote
Kutwa kushauliana
Eti ndoa si lolote
Wakishajaa laana
Wanaangaika kote
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*

Wanaongoza kuroga
Kwa limbwata tuwe bwege
Kutufanya maboga
Kama kuku watufuge
Kisha wakapige soga
Kwa madawa watutege
Hawana hata uoga
Hao ndio vivuruge
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*

Wasumbua wachungaji
Wazazi na viongozi
Eti haki wazihitaji
Miili ikiwa wazi
Heshima ndo mtaji
Na ndoa ni Kama vazi
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*

Mlioko kwenye ndoa
Sijione kama keki
Mkaanza kusumbua
Waume kutudhihaki
Na kaeni mkijua
Mfupa si mshikaki
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*



Najua si kupenda kwenu
Ila ndo mjitambue
Tunzeni miili yenu
Someni mjiinue
Lindeni kilicho chenu
Hatua mjipigie
Msiishi kwa fununu
Badae mtusumbue
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*

*Ujumbe*
Kisulisuli si dawa ya ndoa, bali tuwafundishe vijana maadili,kuwasisitiza kuwajibika na kuwaandaa kwaajili ya ndoa, Kisha tuwakumbe kuwa ndoa si rahisi Kama wanavyofikilia.
Asante sana
 
Kisulisuli niache*

Kisulisuli niache
Niache usinivute
Na sitaki nikufiche
Baadae unisute
Hao watu ni vicheche
Usinifanye nijute
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua Mimi*


Walishindwa kujitunza
Kuheshim mili yao
Ujana ukawaponza
Na wakakosa upeo
Sasa wamekua funza
Watafutao makao
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*

Heri kumuoa punda
Abebe mizigo yangu
Kuliko kuoa ganda
Walilotupa wenzangu
Hakuna atayependa
Eti chetu kiwe changu
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*


Kisulisuli wakumbushe
Ndoa sio makalio
Wala wasijibebishe
Na kutaka wenye vyeo
Wambie wasitutishe
Janja haijaanza Leo
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*

Wakiwa makanisani
Kama kuku chini ya mbawa
Wanaporudi nyumbani
Zaidi ya popobawa
Kuoa hatutamani
Punguzeni kuwa chawa
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*

Kufunga ndoa hiyari
Moyo unaporidhia
Kama hatuko tayari
Mtaishia kulia
Mlijiona sukari
Cheki mnavyojutia
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*

Ukiwa msichana
Maringo ni Kama yote
Majibu yaso maana
Wanaume si chochote
Kutwa kushauliana
Eti ndoa si lolote
Wakishajaa laana
Wanaangaika kote
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*

Wanaongoza kuroga
Kwa limbwata tuwe bwege
Kutufanya maboga
Kama kuku watufuge
Kisha wakapige soga
Kwa madawa watutege
Hawana hata uoga
Hao ndio vivuruge
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*

Wasumbua wachungaji
Wazazi na viongozi
Eti haki wazihitaji
Miili ikiwa wazi
Heshima ndo mtaji
Na ndoa ni Kama vazi
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*

Mlioko kwenye ndoa
Sijione kama keki
Mkaanza kusumbua
Waume kutudhihaki
Na kaeni mkijua
Mfupa si mshikaki
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*



Najua si kupenda kwenu
Ila ndo mjitambue
Tunzeni miili yenu
Someni mjiinue
Lindeni kilicho chenu
Hatua mjipigie
Msiishi kwa fununu
Badae mtusumbue
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*

*Ujumbe*
Kisulisuli si dawa ya ndoa, bali tuwafundishe vijana maadili,kuwasisitiza kuwajibika na kuwaandaa kwaajili ya ndoa, Kisha tuwakumbe kuwa ndoa si rahisi Kama wanavyofikilia.
sawa mzee umetisha ,umeona utembee kwwnye chaki
 
Wanadhani NDOA ni rahisi kiasi hicho!!
 
Back
Top Bottom