Chukwu emeka
JF-Expert Member
- Jan 12, 2018
- 24,314
- 38,919
Copy & Paste
*Kisulisuli niache*
Kisulisuli niache
Niache usinivute
Na sitaki nikufiche
Baadae unisute
Hao watu ni vicheche
Usinifanye nijute
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua Mimi*
Walishindwa kujitunza
Kuheshim mili yao
Ujana ukawaponza
Na wakakosa upeo
Sasa wamekua funza
Watafutao makao
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*
Heri kumuoa punda
Abebe mizigo yangu
Kuliko kuoa ganda
Walilotupa wenzangu
Hakuna atayependa
Eti chetu kiwe changu
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*
Kisulisuli wakumbushe
Ndoa sio makalio
Wala wasijibebishe
Na kutaka wenye vyeo
Wambie wasitutishe
Janja haijaanza Leo
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*
Wakiwa makanisani
Kama kuku chini ya mbawa
Wanaporudi nyumbani
Zaidi ya popobawa
Kuoa hatutamani
Punguzeni kuwa chawa
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*
Kufunga ndoa hiyari
Moyo unaporidhia
Kama hatuko tayari
Mtaishia kulia
Mlijiona sukari
Cheki mnavyojutia
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*
Ukiwa msichana
Maringo ni Kama yote
Majibu yaso maana
Wanaume si chochote
Kutwa kushauliana
Eti ndoa si lolote
Wakishajaa laana
Wanaangaika kote
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*
Wanaongoza kuroga
Kwa limbwata tuwe bwege
Kutufanya maboga
Kama kuku watufuge
Kisha wakapige soga
Kwa madawa watutege
Hawana hata uoga
Hao ndio vivuruge
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*
Wasumbua wachungaji
Wazazi na viongozi
Eti haki wazihitaji
Miili ikiwa wazi
Heshima ndo mtaji
Na ndoa ni Kama vazi
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*
Mlioko kwenye ndoa
Sijione kama keki
Mkaanza kusumbua
Waume kutudhihaki
Na kaeni mkijua
Mfupa si mshikaki
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*
Najua si kupenda kwenu
Ila ndo mjitambue
Tunzeni miili yenu
Someni mjiinue
Lindeni kilicho chenu
Hatua mjipigie
Msiishi kwa fununu
Badae mtusumbue
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*
*Ujumbe*
Kisulisuli si dawa ya ndoa, bali tuwafundishe vijana maadili,kuwasisitiza kuwajibika na kuwaandaa kwaajili ya ndoa, Kisha tuwakumbe kuwa ndoa si rahisi Kama wanavyofikilia.
*Kisulisuli niache*
Kisulisuli niache
Niache usinivute
Na sitaki nikufiche
Baadae unisute
Hao watu ni vicheche
Usinifanye nijute
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua Mimi*
Walishindwa kujitunza
Kuheshim mili yao
Ujana ukawaponza
Na wakakosa upeo
Sasa wamekua funza
Watafutao makao
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*
Heri kumuoa punda
Abebe mizigo yangu
Kuliko kuoa ganda
Walilotupa wenzangu
Hakuna atayependa
Eti chetu kiwe changu
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*
Kisulisuli wakumbushe
Ndoa sio makalio
Wala wasijibebishe
Na kutaka wenye vyeo
Wambie wasitutishe
Janja haijaanza Leo
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*
Wakiwa makanisani
Kama kuku chini ya mbawa
Wanaporudi nyumbani
Zaidi ya popobawa
Kuoa hatutamani
Punguzeni kuwa chawa
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*
Kufunga ndoa hiyari
Moyo unaporidhia
Kama hatuko tayari
Mtaishia kulia
Mlijiona sukari
Cheki mnavyojutia
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*
Ukiwa msichana
Maringo ni Kama yote
Majibu yaso maana
Wanaume si chochote
Kutwa kushauliana
Eti ndoa si lolote
Wakishajaa laana
Wanaangaika kote
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*
Wanaongoza kuroga
Kwa limbwata tuwe bwege
Kutufanya maboga
Kama kuku watufuge
Kisha wakapige soga
Kwa madawa watutege
Hawana hata uoga
Hao ndio vivuruge
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*
Wasumbua wachungaji
Wazazi na viongozi
Eti haki wazihitaji
Miili ikiwa wazi
Heshima ndo mtaji
Na ndoa ni Kama vazi
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*
Mlioko kwenye ndoa
Sijione kama keki
Mkaanza kusumbua
Waume kutudhihaki
Na kaeni mkijua
Mfupa si mshikaki
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*
Najua si kupenda kwenu
Ila ndo mjitambue
Tunzeni miili yenu
Someni mjiinue
Lindeni kilicho chenu
Hatua mjipigie
Msiishi kwa fununu
Badae mtusumbue
*Kisulisuli niache*
*Hao nawajua mie*
*Ujumbe*
Kisulisuli si dawa ya ndoa, bali tuwafundishe vijana maadili,kuwasisitiza kuwajibika na kuwaandaa kwaajili ya ndoa, Kisha tuwakumbe kuwa ndoa si rahisi Kama wanavyofikilia.