Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Kesi namba 458 ya mwaka 2016 (Jamhuri dhidi ya Mkurugenzi wa Jamii Forums na Mwanahisa wa Jamii Media) imeendelea leo, 21 SEPT 2020 asubuhi mbele ya Hakimu Huruma Shaidi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar.
Kutoka Kushoto: Wakili Benedict Inshabakaki, Mwanahisa wa Jamii Media Mike Mushi, Wakili Peter Kibatala, Mkurugenzi wa Jamii Forums Maxence Melo na Wakili Jeremia Mtobesya
Katika shtaka la kwanza, Mkurugenzi wa Jamii Forums anatuhumiwa kuendesha mtandao (JamiiForums.com) bila kujasajiliwa Tanzania kwa Kikoa cha do-TZ
Katika shtaka la pili la Shauri hili, Polisi ilimtaka Mkurugenzi wa Jamii Forums kutoa taarifa kuhusu Wanachama wawili wa Mtandao wa JamiiForums.com waliodaiwa kuandika kuhusu madai ya uhalifu uliokuwa ukiendelea katika Benki ya CRDB.
Taarifa zilizotakiwa ni IP-Address, barua pepe, Majina Halisi ya Wanachama hao. Pia ilitakiwa yaondolewe Mabandiko yote yanayohusu Uhalifu uliokuwa unafanywa na maafisa wa CRDB kitu ambacho Polisi wanadai Mkurugenzi huyo aligoma kuwapa.
Hakimu baada ya kusikiliza pande zote, amepanga kutoa hukumu Tarehe 30 Oktoba 2020. Leo Wakili wa Jamhuri alikuwepo Faraj Nguka na Upande wa Utetezi alikuwa Alphonce Nachipyangu.
Kujua kesi ilipotoka, soma: Kesi dhidi ya JamiiForums (namba 458): Maxence Melo na Mike Mushi wajitetea. Inasubiriwa hukumu
Kutoka Kushoto: Wakili Benedict Inshabakaki, Mwanahisa wa Jamii Media Mike Mushi, Wakili Peter Kibatala, Mkurugenzi wa Jamii Forums Maxence Melo na Wakili Jeremia Mtobesya
Katika shtaka la kwanza, Mkurugenzi wa Jamii Forums anatuhumiwa kuendesha mtandao (JamiiForums.com) bila kujasajiliwa Tanzania kwa Kikoa cha do-TZ
Katika shtaka la pili la Shauri hili, Polisi ilimtaka Mkurugenzi wa Jamii Forums kutoa taarifa kuhusu Wanachama wawili wa Mtandao wa JamiiForums.com waliodaiwa kuandika kuhusu madai ya uhalifu uliokuwa ukiendelea katika Benki ya CRDB.
Taarifa zilizotakiwa ni IP-Address, barua pepe, Majina Halisi ya Wanachama hao. Pia ilitakiwa yaondolewe Mabandiko yote yanayohusu Uhalifu uliokuwa unafanywa na maafisa wa CRDB kitu ambacho Polisi wanadai Mkurugenzi huyo aligoma kuwapa.
Hakimu baada ya kusikiliza pande zote, amepanga kutoa hukumu Tarehe 30 Oktoba 2020. Leo Wakili wa Jamhuri alikuwepo Faraj Nguka na Upande wa Utetezi alikuwa Alphonce Nachipyangu.
Kujua kesi ilipotoka, soma: Kesi dhidi ya JamiiForums (namba 458): Maxence Melo na Mike Mushi wajitetea. Inasubiriwa hukumu