KISUTU: Kesi namba 456(Jamhuri v JamiiForums), Hakimu ashindwa kutoa uamuzi mdogo kutokana na tatizo la kisheria

KISUTU: Kesi namba 456(Jamhuri v JamiiForums), Hakimu ashindwa kutoa uamuzi mdogo kutokana na tatizo la kisheria

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Kesi namba 456 (Jamhuri v Maxence Melo na mwenzake Micke William) ambapo kampuni ya OilCom iliandikwa katika mtandao wa JamiiForums ikidaiwa kukwepa kodi na kuchakachua mafuta bandarini Dar (iliyopo chini ya Hakimu Thomas Simba) imetajwa tena leo Aprili 09, 2018

Upande wa Jamhuri leo umefika na shahidi wao mwingine ambaye ni Afisa Msimamizi wa mauzo ya rejareja wa OilCom, Usama Mohammed

Hata hivyo, shauri hili limeahirishwa mpaka tarehe Mei 03, 2018 baada ya Hakimu Simba kusema anahitaji muda kutatua tatizo dogo la kisheria alilikumbana nalo wakati anasoma jalada ya shauri hilo

Ikumbukwe Hakimu Simba anasubiriwa kutoa uamuzi mdogo juu ya ushahidi uliochapishwa na kutolewa na upande wa Jamhuri

Ushahidi huo ulipingwa na Mawakili wa Utetezi wakisema ushahidi huo hauwezi kutumika kwa kuwa kuna taratibu za kufuata ili ushahidi wa kuchapishwa uweze kutumika.

Kwa kujua kesi hii ilipotokea rejea hapa; Kesi namba 456(Jamhuri v JamiiForums) yaahirishwa. Hakimu hajamaliza kuandika uamuzi mdogo(ruling)
 
Haki Huinua Taifa Bali Dhambi Ni Aibu Kwa Watu Wote
 
Hivi nikikoment against max mello & wenzake ntapigwa ban??
 
Hivi nikikoment against max mello & wenzake ntapigwa ban??
Hakuna kitu kama hicho ...wao wanapigania mahakamani uhuru wa maoni kwa hiyo hawawezi kukukandamiza wewe kwa kutoa maoni yako...litakuwa jambo la kushangaza sana...
 
Hakuna kitu kama hicho ...wao wanapigania mahakamani uhuru wa maoni kwa hiyo hawawezi kukukandamiza wewe kwa kutoa maoni yako...litakuwa jambo la kushangaza sana...
Ahsante kwa uelewesho mkuu

Ntakoment dhidi yao siku nyingine
 
Kama vipi si wamalize tu hiyo kesi yanini kung'ang'ania ishu isiyo na kichwa wala miguu??

Jamiiforum imewakosea nini?
 
Back
Top Bottom