Kisutu: Mahakama yamhukumu Mfanyabiashara Herbinder Seth Kulipa fidia ya Tsh. 26.9 bilioni

Miaka 6 waliyokaa ndani wangezalisha zaidi ya hizo,huku wakichangia uchumi,kutoa ajira na kodi.
 
DPP Sylvester Mwakitalu leo amemuachia huru mfanyabiashara Herbinder Seth baada ya kukiri makosa na kulipa faini.

Mzee Ruge bado amekomaa, tusubiri tuone nini kinaendelea.

Source: Darmpya Blog
Jela si Kuzuri Mkuu hata Yeye 'atakaza' ila 'ataachia' Siku si nyingi. Anajaribu tu Kujitutumua na Kujidhira ila najua Familia pamoja na Mwandamizi Mmoja ( sasa ni Mstaafu ) Serikali ' watampoza ' kwa Ushauri na Kuridhia hatimaye nae Kuachiwa Huru hivi kwa Dhamana kama ' Swahiba ' wake huyu.
 
Mkuu umeisoma vizuri hiyo Habari kweli? Mahakama imemhukumu kulipa fidia bilioni 26 na kifungo cha nje cha mwaka mmoja bila kufanya jinai yoyote
 
Harbinder Seth kulipa fidia ya Sh26.9 bilioni baada ya kupatikana na hatia ya kujipatia Sh309 bilioni kwa njia ya udanganyifu.
Madness, amepata Billion 309 anatakiwa kulipa 26.9?
 
Niulize tu kwa ukihiyo wangu sijui hukumu/kesi za makosa ya uhujumu uchumi zinaendeshwa kwenye mahakama hizi za kawaida na sio mahakama kuu? halafu hii faini mbona kama Ze comedy vile, yaani ni sawa na huku Uswazi nifanye kosa la faini ya shilingi 300,000 na ushee halafu ukipelekwa kwenye mahakama za kata unaambiwa bwashee tunakuachia kwa sasa lipa kwanza faini ya shilingi 2,000/= hizo zingine utamalizia baadae. Kama sio maigizo ni nini basi ....
 
Japo si mtaalam wa sheria huyo baniani kishakiri kosa,anaanzaje sasa kushtaki kwa kitu ambacho alikubali aliiba!
 
Am sure alijaribu kipindi cha Magufuli pia kujinunulia uhuru.

Ila hii approach itumaanishie nini maskini? Kwamba inawezekana tukafungwa kisa hatuna pesa? Mtu akikiri makosa anatakiwa atumikie adhabu iliyopo kisheria au alipe pesa atoke?
Ndugu yangu miaka 4yrs Jela tena jela ya Tanzania ni sawa sawa na miaka 40yrs especially kwa MTU kama yule Seth. Hata rudia tena ujanja ujanja itakuwa kapata darasa la kutosha.
 
Na kalipa 200m baadae utasikia katorokea Canada, tunarudi enzi za awamu ya Kilimo kwanza.
Bila kusahau Big Results Now (BRN) na Tanzania Beyond Tomorrow (TBT),
Tulipoambiwa flat screen zipo Chamwino na Magogoni ila remote control ipo Chalinze hatukuamini
 
Samia = Magufuli

Mtaelewa tu nyie vivutio vya utalii
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imemhukumu, mmiliki wa kampuni ya kufua umeme ya IPTL, Harbinder Seth kulipa fidia ya Sh26.9 bilioni baada ya kupatikana na hatia ya kujipatia Sh309 bilioni kwa njia ya udanganyifu.
YAANI KAPIGA BIL 309 FAINI SH BIL29, HIVI HAWA WANASHERIA WAKIITWA MAJINA YA OVYO WATABISHA,
 
Ushahidi wote wa kinyaraka unaipa haki serikali na ni wazi pesa zimeibiwa na Serikali imepoteza.
Ila maelekezo ya kisheria ya mwanasheria mkuu wa Serikali na hukumu ya Jaji wa mahakama kuu inawabeba kina Harbinger Singh na Ruge mwenzake.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…