HILI ni wazo langu kwa fikira zangu dogo.
Labda niliweke katika swali. Je JamiiForums ina watu wenye mapenzi na Kiswahili kiasi cha kutosha kujitolea muda wao kuanzisha kitu kitakachoitwa KISWAHILI DEVELOPMENT COMMUNITY FORUM?
Je Forum hiyo inaweza kuwa na makundi mbalimbali ya watu hususan kulingana na hapa chini:
. Wana Istilahi za Kemia
. Wana Istilahi za Fizikia
. Wana Istilahi za Jiografia
. Wana Istilahi za Historia
. Wana Istilahi za Commerce
. Wana Istilahi za Book-keeping
. Wana Istilahi za Introduction to Computers
. Wana Istilahi wa Programming
. na kadhalika na kadhalika.
Je, makundi haya yanaweza kujitolea kuanzisha uundwaji istilahi katika fani yao mtandaoni kwa kutumia nadharia ya Open Source. Katika kila fani watu watachangia tafsiri ya maneno ya Kiingereza kwa Kiswahili kwa lengo la kuhakikisha kuwa kila somo lina tafsiri ya msamiati wake wote kwa Kiswahili?
IKUMBUKWE KWAMBA TAYARI MCROSOFT wana hazina ya maneno laki 7 yaliyokwishatafsiriwa kwa Kiswahili.
Baada ya kuundwa kwa Istilahi, je, sisi wenye uchungu na lugha yaetu ya Kiswahili tunaweza kuanzisha Kiswahilipedia?
Katika kiswahilipedia wakuu wa forum katika fani mbalimbali watawagawia wanachama wetu sura za kuandika katika kila somo. Sura hizo zitasomwa na kushahishwa na wengine bila kuharibiwa kwa mada asilia.
Baada ya miaka miwili tu hivi hatutakuwa na elimu zote zinazofundishwa Tanzania hivi sasa kwa Kiswahili?
Wale wanaodhania kwamba ni WANASIASA AU SERIKALI ndiyo inayoweza kutuhamisha toka kutawaliwa na kulemazwa na Kiingereza cha kubabaisha wanakosea. Ni sisi wenyewe. Na tumshukuru Muumba kwa teknolojia hii ya habari na mawasiliano ambayo leo inaweza kuigeuza kazi ya kuwa na vitabu vya kiswahili katika kila somo kuwa rahisi kama vile mchezo. Tuanze. Na wakati ni huu. Maprofesa, madokta na walimu wa Kiswahili. Wakina Ikbal Shaaban Robert Karibuni, Mobhare Matinyi na na David Fisadi Marekani na kina Katunzi India na China ilipeni jamii mlichopewa bure!
Asilimia 95 ya Watanzania hawawezi kuelimika kwa Kiingereza wanataka masomo na mafunzo kwa Kiswahili. Je, hii kazi ikifanyika si tuna soko kubwa tu la masomo ya Kiswahili kwenye mtandano. Twendeni hatua moja mbele ya forum za k ujiburudisha na blogi za kukashifiana tuanze kuaandaa vitabu mtandaoni kwa ulainiiiiiiini!!!!!
Na ninaiomba UFALME WA NORWAY uliochangia kwa kiasi kikubwa kuwepo kwa Microsoft Office na Windows XP/Vista kwa Kiswahili wasisite kutoa msaada wao kwa KISWAHILI DEVELOPMENT COMMUNITY FORUM punde itakapoanzishwa.
Labda niliweke katika swali. Je JamiiForums ina watu wenye mapenzi na Kiswahili kiasi cha kutosha kujitolea muda wao kuanzisha kitu kitakachoitwa KISWAHILI DEVELOPMENT COMMUNITY FORUM?
Je Forum hiyo inaweza kuwa na makundi mbalimbali ya watu hususan kulingana na hapa chini:
. Wana Istilahi za Kemia
. Wana Istilahi za Fizikia
. Wana Istilahi za Jiografia
. Wana Istilahi za Historia
. Wana Istilahi za Commerce
. Wana Istilahi za Book-keeping
. Wana Istilahi za Introduction to Computers
. Wana Istilahi wa Programming
. na kadhalika na kadhalika.
Je, makundi haya yanaweza kujitolea kuanzisha uundwaji istilahi katika fani yao mtandaoni kwa kutumia nadharia ya Open Source. Katika kila fani watu watachangia tafsiri ya maneno ya Kiingereza kwa Kiswahili kwa lengo la kuhakikisha kuwa kila somo lina tafsiri ya msamiati wake wote kwa Kiswahili?
IKUMBUKWE KWAMBA TAYARI MCROSOFT wana hazina ya maneno laki 7 yaliyokwishatafsiriwa kwa Kiswahili.
Baada ya kuundwa kwa Istilahi, je, sisi wenye uchungu na lugha yaetu ya Kiswahili tunaweza kuanzisha Kiswahilipedia?
Katika kiswahilipedia wakuu wa forum katika fani mbalimbali watawagawia wanachama wetu sura za kuandika katika kila somo. Sura hizo zitasomwa na kushahishwa na wengine bila kuharibiwa kwa mada asilia.
Baada ya miaka miwili tu hivi hatutakuwa na elimu zote zinazofundishwa Tanzania hivi sasa kwa Kiswahili?
Wale wanaodhania kwamba ni WANASIASA AU SERIKALI ndiyo inayoweza kutuhamisha toka kutawaliwa na kulemazwa na Kiingereza cha kubabaisha wanakosea. Ni sisi wenyewe. Na tumshukuru Muumba kwa teknolojia hii ya habari na mawasiliano ambayo leo inaweza kuigeuza kazi ya kuwa na vitabu vya kiswahili katika kila somo kuwa rahisi kama vile mchezo. Tuanze. Na wakati ni huu. Maprofesa, madokta na walimu wa Kiswahili. Wakina Ikbal Shaaban Robert Karibuni, Mobhare Matinyi na na David Fisadi Marekani na kina Katunzi India na China ilipeni jamii mlichopewa bure!
Asilimia 95 ya Watanzania hawawezi kuelimika kwa Kiingereza wanataka masomo na mafunzo kwa Kiswahili. Je, hii kazi ikifanyika si tuna soko kubwa tu la masomo ya Kiswahili kwenye mtandano. Twendeni hatua moja mbele ya forum za k ujiburudisha na blogi za kukashifiana tuanze kuaandaa vitabu mtandaoni kwa ulainiiiiiiini!!!!!
Na ninaiomba UFALME WA NORWAY uliochangia kwa kiasi kikubwa kuwepo kwa Microsoft Office na Windows XP/Vista kwa Kiswahili wasisite kutoa msaada wao kwa KISWAHILI DEVELOPMENT COMMUNITY FORUM punde itakapoanzishwa.