Kiswahili ndio Lugha ya Mama/Kwanza Tanzania!

Kiswahili ndio Lugha ya Mama/Kwanza Tanzania!

Kijakazi

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2007
Posts
7,093
Reaction score
10,469
Watu wengi sana utawasikia wanakwambia mimi sijui lugha ya mama ni Kisukuma, sijui Kichaga mara mimi sijui Kihehe woote ni Waongo!

Lugha ya mama Tanzania ni Kiswahili nikimaanisha kwamba Lugha ambayo Mtanzania wa kawaida anaiweza kuiongea na kuiandika kuliko Lugha nyingine yoyote ile, nasema hivi kwa maana zaidi ya 70% ya Watz (Vijana) hata waliozaliwa vijijini ingawaje wanaongea lugha mbili lkn ukiwauliza lugha ambayo wanaweza kuiongea kwa umakini na umahiri mkubwa kati ya Kiswahili na kilugha kingine watakwambia ni Kiswahili lkn ukimuuliza wewe Lugha yako ya kwanza ni ipi atakwambia ni kihehe au Kisumbwa! Hivyo wengi hawaelwei maana ya lugha ya mama ni nini!

Huu ni utafiti uliofanywa na niliofanya pia nilikuwa kwa mfano KLM vijijini huko nakutana na vijana wengi ambao hata hawajawahi kufika Moshi mjini hicho kinachoitwa Kichaga wanakiongea lkn kinawapa shida na ni lazima achanganye na Kiswahili, na ukimuuliza achague Lugha ambayo anaweza kujielezea kwa umakini kabisa hatochagua Hicho kinachoitwa Kichaga bali atachagua Kiswahili!

Na Mikoa yote ni hivyo hivyo, Nilikuwa Usukumani huko Bariadi vijana wote mpaka miaka 25 ingawaje wanaweza kuongea hicho kinachoitwa kisukuma lkn kuna mahali wanakwama na wanaingiza Kiswahili, na ukimwambia achague Lugha ya kukuelezea kitu basi atachagua Kiswahili na wengi humu mtapinga hili nikiwaambia mnielezee kitu kwa Ufasaha mtachagua kwa Kiswahili

Hivyo Lugha Mama ya Tanzani Ni Kiswahili!
 
Sema lugha mama ya hao uliokutana nao, nina watu kijijni hawawezi kuongea sentensi nzima kwa Kiswahili. Labda sikuelewi naomba unieleweshe nini maana ya lugha mama kijakazi wa II
 
Last edited by a moderator:
Sema lugha mama ya hao uliokutana nao, nina watu kijijni hawawezi kuongea sentensi nzima kwa Kiswahili. Labda sikuelewi naomba unieleweshe nini maana ya lugha mama kijakazi wa II


Nimetaja namba kwamba zaidi ya asilimia 70%!

 
Labda ungesema walozaliwa mjin lakini asilimia kubwa ya watu wa kijijini kiswahili kinawashinda sana na mtu hawezi kuchagua kujieleza kwa kiswahili kama ulivosema wengi wao hupenda kujieleza kwa lugha zao, kijijin hata mtoto wa miaka miwil anajua lugha ya kabila lake kuliko kiswahili sidhan kama huo uchunguzi wako umeufanyia vijijini na uliyoandika hayana ukweli.
 
Labda ungesema walozaliwa mjin lakini asilimia kubwa ya watu wa kijijini kiswahili kinawashinda sana na mtu hawezi kuchagua kujieleza kwa kiswahili kama ulivosema wengi wao hupenda kujieleza kwa lugha zao, kijijin hata mtoto wa miaka miwil anajua lugha ya kabila lake kuliko kiswahili sidhan kama huo uchunguzi wako umeufanyia vijijini na uliyoandika hayana ukweli.


Ndio ukweli wenyewe, na sababu kubwa ya kwanza ni Dini, kama wakristo wengi mafundisho ya komunio na kipaimara yanafanywa kwa Kiswahili TZ nzima, pili sasa hivi kuna shule za chekechea mpaka vijijini na Lugha ya shule ni kiswahili hivyo nimefika nakwambia Bariadi ndani ndani kabisa na nikakuta watoto wa Miaka 4-5 wanacheza kwa kutumia Kiswahili nikavutiwa kufwatilia nikagundua ni shauri ya chekechea, nimekwenda pia mpaka Tukuyu na Kyela ndani kabisa hali ni hiyo hiyo, wazee ni sawa wengi Lugha ya Kiswahili inaweza ikawa kidogo tatizo lkn hata wao pia kama anakwenda Kanisani Padri anaendesha Misa kwa Kiswahili na anafanya mahubiri kwa Kiswahili hivyo hawezi kukwepa, lkn Vijana wote TZ nasema kusema zaidi ya 70% lugha ambayo wanaiweza kuongea na kuandika kwa ufasaha ni kiswahili hata kama ukiwaulitza watakwambia wanaongea lugha nyingine lkn ukianza kuongea naye utaona bila ya kutumia Kiswahili anakwama!
 
Inawezekana ila sina hakika na hayo usemayo kwamba wanaweza kuongea na kuandika kiswahili fasaha.
 
Back
Top Bottom