Kitabu cha maisha ya mwanadamu

Kitabu cha maisha ya mwanadamu

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Utangulizi
Maisha ya mwanadamu, yana sehemu kuu tatu:-
  • Kuzaliwa
  • Kuishi
  • Kufa
Sura 1: Kuzaliwa​
  • Mtu anazaliwa pale panapokuwa na uhusiano wa kimapenzi, kati ya mwanaume na mwanamke.​
  • Na uhusiano huo uleta ujauzito na baada ya miezi 9 mtoto uzaliwa.​
  • Na tukio hili hutokea mara moja​
Sura 2: Kuishi​
  • Mtoto akishazaliwa, upitia malezi mbalimbali, pamoja na kupata elimu stahiki, itakayomuwezesha kuishi katika jamii.​
  • Kutofautiana kwa malezi, na elimu; kutoka kwa familia moja kwenda nyingine; kunasabisha kuwa na watu wenye tabia na mitazamo tofauti.​
  • Mitazamo hasi:-
    • Ujambazi​
    • Uhuni​
    • Uzurumaji/utapeli​
    • Unafiki/uongo​
    • Ubinafsi​
    • Uchawi​
    • Ushoga​
    • Chuki​
    • Ujilimbikiziaji wa mali​
    • Tamaa n.k​
  • Mitazamo chanya:-
    • Ustaarabu​
    • Kujali wengine​
    • Unyenyekevu​
    • Kupenda wengine wafanikiwe n.k​
  • Ni kipindi ambacho binadamu ataishi kwa furaha, pia ni kipindi ambacho ataishi kwa huzuni.​
  • Ni kipindi ambacho, watu uishi huku wakidharauliana; na mwingine kujiona bora zaidi kuliko mwingine; ni 'full' kukanyagana.​
  • Kutokana na viungo kuchoka, ulaji wa vyakula, umri mkubwa, magonjwa nyemelezi n.k; binadamu uanza kudhoofika.​
Sura 3: Kufa​
  • Hii ni hatua ya mwisho, inayofunga kitabu cha binadamu, na kubaki kuwa historia kwa waliobaki.​
  • Na hii utokea mara moja tu.​
  • Kama alitenda mema atakumbukwa kwa mema, na kama hakutenda mema atakumbukwa kwa aliyoyafanya.​
  • Mali zote alizozitafuta, ataziacha; na mwili tu ndio utakao-ifadhiwa.​
Mwisho

Nilichojifunza katika hiki kitabu, wote tulio hai leo; tupo kwenye sura 2, na wengi huwa tunajisahau kuwa hatutafika sura 3.

Ukijua sura 3 lazima ufike, itakusaidia kuishi vizuri katika sura 2; haya mambo ya kukanyagana katika sura ya 2 yatapungua.

Swali: Sura 2 kwako ikoje?​
 
Back
Top Bottom