Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 9,189
- 16,128
Kitabu hiki kizuri sana. Kina mengi ya kujifunza yenye msaada hata leo.
Kimetungwa na S. J. Ntiro
Kuchapwa 1953.
Unaweza kukisoma ndani ya maktaba app. TuPM Kuungwa.
Juzi juzi mtaalamu mmoja wa mambo ya Afrika aliandika:
"Bila mikusanyo mingi ya hakika ya mambo ya zamani tuyaonayo katika historia, na bila kufahamu vema hali ya nchi yetu ilivyokuwa hapo kale, basi hatutakuwa na nguvu za kuendelea mbele nasi tutapata hasara tu, maana tutakosa kuwa na usawa na ufungamano."
Afrika ya Mashariki ni nchi isiyo na vitabu vingi vya historia. Wareno waliandika mambo kadha wa kadha ya wakati waliotawala, lakini hayapatikani wala hayasomeki ila kwa shida. Kiswahili peke yake kilikuwa na maandishi yake kabla ya mwanzo wa kazi ya Dr. Krapf 1844, nayo yalitaja hasa mashindano ya Waarabu waliopigania dola zao na enzi zao pwanipwani.
Lakini kuna sehemu nyingine za maarifa ya historia ambayo ni bora sana, lakini hayo hayajajulikana na wataalamu wengi bado ila wachache tu. Maarifa hayo ni desturi na masimulizi ambayo mpaka sasa yana nguvu katika maisha ya Afrika ya Mashariki. Mfuatano wa vitabu unaoitwa DESTURI NA MASIMULIZI KATIKA AFRIKA YA MASHARIKI utawaonyesha Waafrika na waandishi njia ya kuvumbua mambo hayo kama Wazungu wachache tu wawezavyo, ili kuandika habari za baadhi ya desturi ambazo wamezizoea, na kuhifadhi masimulizi ya kale ambayo yamepitishwa kwa midomo. Kama tujuavyo siku hizi wazee hawawasimulii vijana kama ilivyokuwa desturi katika siku za zamani.
Vile vile, pamoja na mfuatano huu wa vitabu vyenye maarifa ya maisha ya makabila, kuna mwingine ambao unatolewa siku hizi mfano wa huo. Vitabu vyake vina habari za maono ya wasafiri wa zamani waliokuja huku Afrika ya Mashariki, na mambo yaliyowapata.
Mifuatano miwili hiyo ya vitabu inakusudiwa kuwapa vijana wa Kiafrika na watu wa mataifa mengine nafasi kubwa ya kujifunza historia ya nchi hii pamoja na masimulizi na desturi.
Kimetungwa na S. J. Ntiro
Kuchapwa 1953.
Unaweza kukisoma ndani ya maktaba app. TuPM Kuungwa.
DIBAJI YA WATOAJI KITABU
Juzi juzi mtaalamu mmoja wa mambo ya Afrika aliandika:
"Bila mikusanyo mingi ya hakika ya mambo ya zamani tuyaonayo katika historia, na bila kufahamu vema hali ya nchi yetu ilivyokuwa hapo kale, basi hatutakuwa na nguvu za kuendelea mbele nasi tutapata hasara tu, maana tutakosa kuwa na usawa na ufungamano."
Afrika ya Mashariki ni nchi isiyo na vitabu vingi vya historia. Wareno waliandika mambo kadha wa kadha ya wakati waliotawala, lakini hayapatikani wala hayasomeki ila kwa shida. Kiswahili peke yake kilikuwa na maandishi yake kabla ya mwanzo wa kazi ya Dr. Krapf 1844, nayo yalitaja hasa mashindano ya Waarabu waliopigania dola zao na enzi zao pwanipwani.
Lakini kuna sehemu nyingine za maarifa ya historia ambayo ni bora sana, lakini hayo hayajajulikana na wataalamu wengi bado ila wachache tu. Maarifa hayo ni desturi na masimulizi ambayo mpaka sasa yana nguvu katika maisha ya Afrika ya Mashariki. Mfuatano wa vitabu unaoitwa DESTURI NA MASIMULIZI KATIKA AFRIKA YA MASHARIKI utawaonyesha Waafrika na waandishi njia ya kuvumbua mambo hayo kama Wazungu wachache tu wawezavyo, ili kuandika habari za baadhi ya desturi ambazo wamezizoea, na kuhifadhi masimulizi ya kale ambayo yamepitishwa kwa midomo. Kama tujuavyo siku hizi wazee hawawasimulii vijana kama ilivyokuwa desturi katika siku za zamani.
Vile vile, pamoja na mfuatano huu wa vitabu vyenye maarifa ya maisha ya makabila, kuna mwingine ambao unatolewa siku hizi mfano wa huo. Vitabu vyake vina habari za maono ya wasafiri wa zamani waliokuja huku Afrika ya Mashariki, na mambo yaliyowapata.
Mifuatano miwili hiyo ya vitabu inakusudiwa kuwapa vijana wa Kiafrika na watu wa mataifa mengine nafasi kubwa ya kujifunza historia ya nchi hii pamoja na masimulizi na desturi.