Kitabu ''Juhudi na Changamoto,'' Sheikh Ponda na Suala la Elimu

Kitabu ''Juhudi na Changamoto,'' Sheikh Ponda na Suala la Elimu

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
KITABU "JUHUDI NA CHANGAMOTO" SHEIKH PONDA NA SUALA LA ELIMU

Siku moja Sheikh Ponda kanipigia simu akaniambia kuwa wamefungua shule na ananialika hapo shuleni nizungumze na wanafunzi.

Mimi sikuwa na taarifa ya haya kumbe shule imefunguliwa muda mrefu.

Hapo shuleni kuna msikiti mkubwa naingia msikitini naukuta msikiti umejaa wanafunzi.

Vijana wa kiume wamekaa mbele na dada zao wakiwa katika hijab wamejipanga nyuma.

Mbele nawaona waalimu wao wamejipanga kulia na kushoto kwangu.

Katikati ya umma huu kasimama mpiga video.
Najisemea kimoyomoyo kumbe hii shughuli kubwa.

Aliponipa mwaliko Sheikh Ponda aliniambia nizungumze na wanafunzi niwafunze historia ya kweli ya Tanganyika nikiweka msisitizo katika juhudi za Waislam wa wakati ule katika elimu na vikwazo walivyowekewa na wakoloni na kisha serikali iliyokuja kushika madaraka baada ya wakoloni kuondolewa na nchi kuwa mikononi kwetu wenyewe wananchi..

Sheikh Ponda akanisisitizia kuwa kuna propaganda kubwa inaenezwa kuwa Waislam hawathamini elimu na ndiyo maana wako nyuma.

Wanatangaza kuwa Waislam hatupendi shule tunapeleka watoto madrasa na haya wanayasema kinywa kipana na kwa kebehi.

"Ndugu yangu njoo usafishe bongo za vijana wetu hawa wajue ukweli kwani huu ukweli utawapa nguvu ya wao kujitambua na hii italinda heshima yao na heshima yetu sisi wazazi wao."

Nimesimama pale msikiti mbele ya kibla nawaangalia wanafunzi waliokuwa mbele yangu nahisi kuna kitu kimepanda kwenye koromero na machozi kama yanataka kunitoka.

Namkumbuka Mufti Sheikh Hassan bin Ameir na juhudi zake chini ya Daawat Islamiyya za kuwahamasisha Waislam kujenga shule wakati wa ukoloni na hata baada ya ukoloni kuondoka Tanganyika.

Na ni juhudi hizi ndizo zilizomfanya afukuzwe Tanganyika arejeshwe kwao Zanzibar.

Huyu Sheikh Ponda huyu...

Msikiti uko kimya kabisa.
Nilishatambulishwa.

Hadhira inanisubiri mimi nianze kuzungumza.

Fikra za Sheikh Hassan bin Ameir na Ponda na ule umma uliokusanyika pale ndiyo ulionitoa pale nikiwa kama nimeduwaa.

Akili imerejea mahali pake.

Nasoma dua ya Nabii Mussa kimoyomoyo kisha nafungua kinywa kuzungumza.

Naanza kwa kueleza kuwa Waislam ndiyo jamii ya kwanza Pwani ya Afrika ya Mashariki kujua kusoma na kuandika kupitia madrasa.

Uislam uliingia Pwani ya Afrika ya Mashariki pamoja na elimu.
Waislam wakawa ndiyo watu wa kwanza kujua Kusoma, Kuandika na Hisabati.

Kipindi cha maswali na majibu hakika kilinifurahisha.
Somo lilikuwa limeeleweka.

Vijana wanauliza imekuwaje wanafundisha historia isiyo ya kweli?

Sheikh Ponda sasa kuwa ana shule anasomesha ikawa yale aliyokuwa anayasikia kuwa kuna mfumo uliojengwa wa kuwahujumu Waislam katika elimu sasa yakawa yanamkabili usoni moja kwa moja.

Changamoto hii ndiyo ikawa inafungua sura ya kwanza ya kitabu.
Kweli imedhihiri.

1661876942692.png
 
Mzee Mohamed Said, Binafsi ninaheshimu sana mchango wako wa kitaaluma hasa kwenye utunzi wa vitabu, na hususani vinavyohusu historia ya Tanganyika!

Jambo moja liko wazi, wewe daima huwa unaitazama historia katika jicho la kidini, na huwa unaelezea ushiriki wa waislamu katika harakati za kupigania uhuru. Ni jambo jema, maana una uhuru na haki hiyo, hakuna sheria inakuzuia kuona mambo katika muktadha wa kidini.

Jambo moja ambalo mie hutatizika nalo, ni pale unapodai kuwa historia imepotoshwa kwa lengo la kutowatambua waislamu katika mchakato wa uhuru, huwa sioni mantiki ni kwa nini waislamu wasitambuliwe, kwani wakitambuliwa watafanyaje?

Pia historia inawataja wengi tu ambao ni waislamu, akina Bibi Titi, Mohamed, Rashid Kawawa, Fundikira na wengine wengi tu waislamu wanatambuliwa ushiriki wao kwenye historia ya ujenzi wa nchi yetu.

Mzee Mohamed Said, ni sawa wewe kujikita katika muktadha wa kidini unapoongelea historia, lakini sio sawa kusema kuwa historia imepotoshwa ili kuhujumu waislamu.

Nimesoma kitabu chako ISLAMIC MOVEMENT AND CHRIASTIANS HEGEMONY sijaona ushahidi wa kuwa waislamu ama wamepuuzwa au hawatambuliwi kwenye historia.

I think, It's about time you revisit your approach on this matter!
 
Elimu ipi Kwanza?

Elimu Duniani au Elimu Akhera??

Kumbuka BOKO HARAM. Elimu duniani Ni HARAM
 
K
Mzee Mohamed Said, Binafsi ninaheshimu sana mchango wako wa kitaaluma hasa kwenye utunzi wa vitabu, na hususani vinavyohusu historia ya Tanganyika!

Jambo moja liko wazi, wewe daima huwa unaitazama historia katika jicho la kidini, na huwa unaelezea ushiriki wa waislamu katika harakati za kupigania uhuru. Ni jambo jema, maana una uhuru na haki hiyo, hakuna sheria inakuzuia kuona mambo katika muktadha wa kidini.

Jambo moja ambalo mie hutatizika nalo, ni pale unapodai kuwa historia imepotoshwa kwa lengo la kutowatambua waislamu katika mchakato wa uhuru, huwa sioni mantiki ni kwa nini waislamu wasitambuliwe, kwani wakitambuliwa watafanyaje?

Pia historia inawataja wengi tu ambao ni waislamu, akina Bibi Titi, Mohamed, Rashid Kawawa, Fundikira na wengine wengi tu waislamu wanatambuliwa ushiriki wao kwenye historia ya ujenzi wa nchi yetu.

Mzee Mohamed Said, ni sawa wewe kujikita katika muktadha wa kidini unapoongelea historia, lakini sio sawa kusema kuwa historia imepotoshwa ili kuhujumu waislamu.

Nimesoma kitabu chako ISLAMIC MOVEMENT AND CHRIASTIANS HEGEMONY sijaona ushahidi wa kuwa waislamu ama wamepuuzwa au hawatambuliwi kwenye historia.

I think, It's about time you revisit your approach on this matter!

Elimu ipi Kwanza?

Elimu Duniani au Elimu Akhera??

Kumbuka BOKO HARAM. Elimu duniani Ni HARAM
Acha kusikiliza propaganda we chizi! Nani amekuambia elimu duniani ni haramu? Na nani amekua boko haramu ni waislamu? Ondoa taka taka kichwani mwako
 
Mufti Sheikh Hassan bin Ameir na juhudi zake chini ya Daawat Islamiyya za kuwahamasisha Waislam kujenga shule wakati wa ukoloni na hata baada ya ukoloni kuondoka Tanganyika.

Na ni juhudi hizi ndizo zilizomfanya afukuzwe Tanganyika arejeshwe kwao Zanzibar.
Kama alikuwa Mzanzibar na Wakati huo hakukua na Muungano, hauoni ilikuwa sahihi kumfurusha mhamiaji huyo aliyekuwa akifanya yasiyopaswa kufanywa na mlowezi wa kigeni?
 
Kama alikuwa Mzanzibar na Wakati huo hakukua na Muungano, hauoni ilikuwa sahihi kumfurusha mhamiaji huyo aliyekuwa akifanya yasiyopaswa kufanywa na mlowezi wa kigeni?
Kinyungu,
Naona umeghadhibika.
Nasoma maneno, ''kumfurusha,'' ''mlowezi.''

Nashangaa sana kuwa humjui Sheikh Hassan bin Ameir.

Sheikh Hassan bin Ameir alikuwa Mufti wa Tanganyika ingawa alikuwa Mzanzibar.

Sheikh Hassan bin Ameir mwaka wa 1950 alikuwa mjumbe katika TAA Political Subcommittee pamoja na Hamza Mwapachu, Abdul Sykes, Dr. Vedasto Kyaruzi, Steven Mhando, Sheikh Said Chamwenyewe na John Rupia.

Hii ndiyo kamati iliyokuwa inaweka mikakati ya kuunda TANU na Sheikh Hassan bin Ameir alikuwa mmoja wa wanachama wa mwanzo wa TANU.

Sheikh Hassan bin Ameir alikuwa akiuza kadi za TANU misikitini katika darsa zake.

Ingia hapa ujifunze historia ya uhuru wa Tanganyika fanya ''name srarch:''

mohamedsaidsalum.blogspot.com
 
Kwahiyo unataka watoto na jamii ya watanzania ijigawane kwa misingi ya dini na imani zao?

Ina maana maisha ya sasa ya kuishi kwa utulivu na mshikamano wewe unayaona si sahihi unataka yale ya kukimbizana, kugombana, kuwindana, kuuwana, kuchukiana kama yale ya Nigeria wanavyofanyiana wakristo na waislam?!


Mzee, kama umri umekutupa mkono hebu mrejee MUNGU wako kwa sala kisha simamia huko kwenye maisha yako baada ya haya maana ndio muhimu ila hili la kuwafitisha watoto wa kiafrika kwa itikadi za magharibi na za uarabuni ni kinyume na maadili ya jamii yetu ya kitanzania, kinyume na katiba ya nchi lakini pia ni kutukana heshima ya utu katika jamii yetu ambayo inaishi kwa upendo.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwahiyo unataka watoto na jamii ya watanzania ijigawane kwa misingi ya dini na imani zao?

Ina maana maisha ya sasa ya kuishi kwa utulivu na mshikamano wewe unayaona si sahihi unataka yale ya kukimbizana, kugombana, kuwindana, kuuwana, kuchukiana kama yale ya Nigeria wanavyofanyiana wakristo na waislam?!


Mzee, kama umri umekutupa mkono hebu mrejee MUNGU wako kwa sala kisha simamia huko kwenye maisha yako baada ya haya maana ndio muhimu ila hili la kuwafitisha watoto wa kiafrika kwa itikadi za magharibi na za uarabuni ni kinyume na maadili ya jamii yetu ya kitanzania, kinyume na katiba ya nchi lakini pia ni kutukana heshima ya utu katika jamii yetu ambayo inaishi kwa upendo.



Sent using Jamii Forums mobile app
Sam...
Nakuomba usome kitabu cha Sheikh Ponda uone yaliyomo ndani.
Hapo utakuwa uko katika hali nzuri sana ya kuelewa tatizo hili.

Unazungumza kutokana na mengi usiyoyajua.
 
Mzee Mohamed Said, Binafsi ninaheshimu sana mchango wako wa kitaaluma hasa kwenye utunzi wa vitabu, na hususani vinavyohusu historia ya Tanganyika!

Jambo moja liko wazi, wewe daima huwa unaitazama historia katika jicho la kidini, na huwa unaelezea ushiriki wa waislamu katika harakati za kupigania uhuru. Ni jambo jema, maana una uhuru na haki hiyo, hakuna sheria inakuzuia kuona mambo katika muktadha wa kidini.

Jambo moja ambalo mie hutatizika nalo, ni pale unapodai kuwa historia imepotoshwa kwa lengo la kutowatambua waislamu katika mchakato wa uhuru, huwa sioni mantiki ni kwa nini waislamu wasitambuliwe, kwani wakitambuliwa watafanyaje?

Pia historia inawataja wengi tu ambao ni waislamu, akina Bibi Titi, Mohamed, Rashid Kawawa, Fundikira na wengine wengi tu waislamu wanatambuliwa ushiriki wao kwenye historia ya ujenzi wa nchi yetu.

Mzee Mohamed Said, ni sawa wewe kujikita katika muktadha wa kidini unapoongelea historia, lakini sio sawa kusema kuwa historia imepotoshwa ili kuhujumu waislamu.

Nimesoma kitabu chako ISLAMIC MOVEMENT AND CHRIASTIANS HEGEMONY sijaona ushahidi wa kuwa waislamu ama wamepuuzwa au hawatambuliwi kwenye historia.

I think, It's about time you revisit your approach on this matter!
Mjuni...
Nasikitika kukuambia kuwa huijui histotia ya Waislam wa Tanganyika.
Kwa ajili hii unashindwa kuelewa ukweli.

Soma historia hii kwanza.
 
Kwahiyo unataka watoto na jamii ya watanzania ijigawane kwa misingi ya dini na imani zao?

Ina maana maisha ya sasa ya kuishi kwa utulivu na mshikamano wewe unayaona si sahihi unataka yale ya kukimbizana, kugombana, kuwindana, kuuwana, kuchukiana kama yale ya Nigeria wanavyofanyiana wakristo na waislam?!


Mzee, kama umri umekutupa mkono hebu mrejee MUNGU wako kwa sala kisha simamia huko kwenye maisha yako baada ya haya maana ndio muhimu ila hili la kuwafitisha watoto wa kiafrika kwa itikadi za magharibi na za uarabuni ni kinyume na maadili ya jamii yetu ya kitanzania, kinyume na katiba ya nchi lakini pia ni kutukana heshima ya utu katika jamii yetu ambayo inaishi kwa upendo.



Sent using Jamii Forums mobile app
Uko sawa!

Haya mahubiri ya kuwajaza watoto propaganda za kwamba waislamu sijui wameonewa, sijui historia imepotoshwa ili kuwakandamiza waislamu na mambo kama hayo ni kueneza chuki tu na ubaguzi.

Kwani uislamu hauwezi kusimama bila mafundisho ya chuki, ubaguzi na visasi?
 
Kwahiyo unataka watoto na jamii ya watanzania ijigawane kwa misingi ya dini na imani zao?

Ina maana maisha ya sasa ya kuishi kwa utulivu na mshikamano wewe unayaona si sahihi unataka yale ya kukimbizana, kugombana, kuwindana, kuuwana, kuchukiana kama yale ya Nigeria wanavyofanyiana wakristo na waislam?!


Mzee, kama umri umekutupa mkono hebu mrejee MUNGU wako kwa sala kisha simamia huko kwenye maisha yako baada ya haya maana ndio muhimu ila hili la kuwafitisha watoto wa kiafrika kwa itikadi za magharibi na za uarabuni ni kinyume na maadili ya jamii yetu ya kitanzania, kinyume na katiba ya nchi lakini pia ni kutukana heshima ya utu katika jamii yetu ambayo inaishi kwa upendo.
Sam...
Hili si suala la umri wangu.
Nimesimama kupigania haki niko kijana sana.

Wala haya wewe si wa kujibu.
Wanaotakiwa kuwajibu Waislam wako kimya.

Na si kama wako kimya hawasikii.
Wako kimya wanatambua tatizo na unyeti wa suala hili.

Mimi niko hapa kwa jina langu halisi sijajificha kwa kuwa nasema kweli.
 
Uko sawa!

Haya mahubiri ya kuwajaza watoto propaganda za kwamba waislamu sijui wameonewa, sijui historia imepotoshwa ili kuwakandamiza waislamu na mambo kama hayo ni kueneza chuki tu na ubaguzi.

Kwani uislamu hauwezi kusimama bila mafundisho ya chuki, ubaguzi na visasi?
Mjuni...
Kutahadharisha dhulma ndiyo chuki, ubaguzi na visasi?

Ikiwa haya yapo kwenye jamii nini kifanyike?
 
Ukifa wafia dini wenzio pengine watakupongeza au kukupuuza..ila jua unachokitengeneza na kukipandikiza sio asili ya watanzania.

Mimi nitaendelea kukupuuza daima..mana wewe sio mtanzania bali ni mamruki...uliyekuja kwa lengo la kutengeneza utengano na chuki dhidi ya watanzania.

#MaendeleoHayanaChama

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Hee! Kuna watu Wana pewa mamilioni burebure?
Mbona sijawahi kusikia watu humu wanalalamika
 
Mjuni...
Kutahadharisha dhulma ndiyo chuki, ubaguzi na visas?

Ikiwa haya yapo kwenye jamii nini kifanyike?
Mzee wetu Mzee Mohamed Said, unapomweleza mtu kwamba umedhulumiwa sana, unategemea reaction yake itakuwa ni nini kama sio kuwachukia wanaodhaniwa wamemdhulumu, unapowaambia hayo watoto wadogo wa shule, hauzalishi kizazi chenye chuki dhidi ya watu wengine?

Nini kifanyike?

Kwani katika uislamu hakuna kusamehe mtu aliekukosea?
Kama ni kweli waislamu walionewa huko nyuma labda kwa sababu ya mifumo ya kikoloni, kwa nini msisamehe na kusahau, na watoto wafundishe upendo dhidi ya watu wengine?

Wakristo wanafundishwa kumpenda hata adui yako, kwenye uislamu hakuna?
 
Mzee wetu Mzee Mohamed Said, unapomweleza mtu kwamba umedhulumiwa sana, unategemea reaction yake itakuwa ni nini kama sio kuwachukia wanaodhaniwa wamemdhulumu, unapowaambia hayo watoto wadogo wa shule, hauzalishi kizazi chenye chuki dhidi ya watu wengine?

Nini kifanyike?

Kwani katika uislamu hakuna kusamehe mtu aliekukosea?
Kama ni kweli waislamu walionewa huko nyuma labda kwa sababu ya mifumo ya kikoloni, kwa nini msisamehe na kusahau, na watoto wafundishe upendo dhidi ya watu wengine?

Wakristo wanafundishwa kumpenda hata adui yako, kwenye uislamu hakuna?
Mujuni,
Cha kufanya kiko mikononi kwa wale ambao tumewakabidhi madaraka ya utawala.
Hili tatizo linafahamika.

Serikali ndiyo ina uwezo wa kuondoa dhulma katika jamii.
 
Hee! Kuna watu Wana pewa mamilioni burebure?
Mbona sijawahi kusikia watu humu wanalalamika
Sirm,
Mwaka wa 1993 serikali ya Tanzania ilitilia sahihi mkataba na makanisa, mkataba uliokuja kujulikana kama ''Memorandum of Understanding.''

Haya ni makubaliano ambayo serikali iliidhinisha elimu, huduma za jamii na afya ziendeshwe na Christian Council of Tanzania (CCT), Tanzania Episcopal Conference (TEC) kwa kushirikiana na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mkataba huu ulitayarishwa kwa siri na Dr. Costa Mahalu, wa Kitivo cha Sheria Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam na ukatiwa sahihi na Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Edward Lowassa.

Mkataba huu ulitiwa sahihi bila ya kuwashirikisha au kuwafahamisha Waislam.

Ili makubaliano haya yaweze kutekelezeka, serikali ilibidi ifanye marekebisho kifungu 30 cha Education Act No. 25, 1978.
 
Ukifa wafia dini wenzio pengine watakupongeza au kukupuuza..ila jua unachokitengeneza na kukipandikiza sio asili ya watanzania.

Mimi nitaendelea kukupuuza daima..mana wewe sio mtanzania bali ni mamruki...uliyekuja kwa lengo la kutengeneza utengano na chuki dhidi ya watanzania.

#MaendeleoHayanaChama

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Jiwe...
''Mamluki,'' si ''Mamruki.''
 
Aga khan ni wakristo ?


Mbona wanatoa huduma za afya !


Nakusubiria hapa uniambie kama ni wakristo pekee wanaotoa huduma za afya na kama sio wao tu ni kwanini ulalamike
 
Back
Top Bottom