Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 9,189
- 16,128
- Thread starter
-
- #101
sura ya 13. Imam Malcom X
Niliacha kazi kwenye kampuni ya Ford. Ilikuwa wazi kwangu kuwa Bwana Muhammad anahitaji wahubiri wa kutangaza mafundisho yake na kuanzisha Mahekalu mengine kwa watu weusi milioni ishirini na mbili waliokuwa wameshikwa akili na “kulala” kwenye majiji ya Marekani.
Uamuzi wangu ulikuja mara moja bila kusita. Mara zote nimekuwa ni mwanaharakati, na pengine hilo ndilo lililonifanya nichukue hatua haraka kuliko Maimam wengine. Lakini kila Imam, kwa muda wake na kwa nafasi yake alifikia hitimisho kuwa ilikuwa imeandikwa awe mwanafunzi wa bwana Muhammad, na maisha yake yote yalikuwa ni maandalizi kwa ajili ya suala hilo.
Uislamu unafundisha kuwa kila kinachotokea kimeandikwa.
Kwa miezi kadhaa aliyokuwa akinifundisha, Bwana Muhammad alinikaribisha kumtembelea nyumbani kwake Chicago mara nyingi niwezavyo.
Hata gerezani sikuwahi kusoma na kujifunza kwa makini kama nilivyojifunza chini ya bwana Muhammad. Nilizama kujifunza taratibu za ibada; mafundisho yake juu ya wanawake na wanaume; taratibu za kiuongozi; maana halisi na maana zingine, na matumizi ya Biblia na Quran.
Kila usiku nilienda kulala nikiwa nimeshangazwa zaidi. Kama si Allah basi ni nani mwingine angeweza kuweka hekima ile ndani ya mwanakondoo mnyenyekevu yule kutoka Georgia aliyeishia darasa la nne. Neno “mwanakondoo” nililitoa kwenye unabii unaopatikana kwenye kitabu cha Ufunuo ambako kuna kondoo wa mfano aliyekuwa na upanga wenye makali kuwili mdomoni mwake. Upanga wenye makali kuwili wa bwana Muhammad ulikuwa ni mafundisho yake, ulikata mbele na nyima ili kuiweka huru akili ya mtu mweusi kutoka kushikwa na mzungu.
Nilimhusudu bwana Muhammad kwa maana halisi ya neno la Kilatin nilalomanisha kuhusudu—yaani “Adorare.” Linamaanisha zaidi ya kuhusudu. Linamaanisha kumsujudu kwangu kulikuwa kukuu sana kiasi kwamba ndiye alikuwa mtu pekee niliyewahi kumuogopa—si kuogopa kama kule kumuogopa mtu mwenye bunduki, bali kuogopa kama vile kumuogopa mtu mwenye nguvu za jua.
Baada ya bwana Muhammad kuona kuwa nimeiva alinituma Boston. Ndugu Lloyd X aliishi huko. Aliwakaribisha watu waliopendezwa na mafundisho yake ya Kiislamu kuja kunisikiliza sebuleni kwake.
Nitanukuu niliyosema pale na sehemu nyingine nilizoenda kuhubiri. Maana nakumbuka mambo niliyohubiri mara kwa mara. Nakumbuka siku zile nilipenda sana kuanza na mfano juu ya bwana Muhammad.
“Mungu amempa bwana Muhammad ukweli mkali,” niliwaambia. “Ni kama upanga wenye makali kuwili. Unakukata na kukusababishia maumivu makali, lakini kama unaweza kuukubali ukweli, utakuponya na kukuokoa kutoka katika kifo.”
Baada ya utangulizi huo sikupoteza muda, mara moja nilianza kuwafungua macho juu ya shetani mweupe. ‘Najua hamtambui ukubwa wa madhira ya uhalifu wa mzungu mkristo . . .
‘Hata katika Biblia hakuna uhalifu kama huo! Mungu kwa hasira aliwaua kwa moto waliofanya uhalifu mdogo kuliko huu. Watu weusi milioni mia moja! Mababu wako na wangu! Waliuawa na mzungu huyu ili tu kutufikisha hapa watu milioni kumi na tano na kutufanya watumwa. Njiani aliua watu milioni mia moja. Natamani ningeweza kuwaonyesha sakafu ya bahari ilivyokuwa wakati huo. Miili ya watu weusi, damu, na mifupa iliyovunjwa kwa mateke na marungu. Miili ya wanawake wajawazito waliotupwa baharini baada ya kuwa wagonjwa sana. Wakitupwa baharini kwenye papa, papa waliojifunza kuwa kufuata meli za watumwa ni njia rahisi ya kujipatia chakula.
“Kitendo cha wazungu kubaka wanawake weusi kilianza mle mle melini! Shetani mwenye macho ya bluu hakusubiri awafikishe kwanza! Binadamu aliyestaarabika hajawahi kushuhudia uchafu na mauaji na namna ile ”
Kuzungumzia ubaya wa utumwa hakujawahi shindwa kuwagusa watu weusi. Inashangaza sana kuona watu wengi
weusi wamekubali mzungu awapotoshe kiasi cha wengine kudhani kuwa enzi za utumwa zilikuwa enzi za starehe! Mara baada ya kuwachochea kwa habari za utumwa nilianza kuwazungumzia wao wenyewe.
‘Nataka mtakapo chumbani hapa muone hili kila mnapoonana na shetani wa kizungu. Ndiyo, ni shetani. Nataka muanze kumchunguza kwenye maeneo yake ambayo hataki nyinyi muwepo. Mchunguzeni anapokuwa anajifunua waziwazi.
“Kila mara unapomuona mzungu, fikiria kuhusu shetani unayemuona! Fikiria kuwa ni kupitia damu na jasho la babu zako watumwa ndiyo alijenga Milki hii ambayo leo hii ndiyo nchi tajiri kuliko zote duniani-dunia inayomchukia kutokana na uovu na tama yake.
Kila mkutano, wale waliofika mkutano uliopita walirudi wakiwa na rafiki zao. Hakuna hata mmoja wao aliyewahi kushuhudia mzungu akivuliwa kinyago alichojivika. Kila baada ya mkutano niliuliza, “kila anayeamini aliyosikia asimame.” Sikumbuki kuona mtu ambaye hakusimama. Na hata siku za Jumapili usiku niliposema, “Nani anataka kuwamfuasi wa Mtukufu Elijah Muhammad?” walisimama hata wale ambao niliona wazi hawako tayari.
Baada ya kama miezi mitatu tulikuwa na watu wa kutosha kuweza kufungua Hekalu dogo. Nakumbuka furaha tuliyokuwa nayo tulipokodi viti vya kukunjwa kwa ajili ya Hekalu letu. Nilijawa na furaha sana siku niliyomjulisha bwana Muhammad anuani ya Hekalu letu.
Ni wakati tulipopata Msikiti huu mdogo ndipo dada yangu Ella alianza kuja kunisikiliza. Alikaa na kustaajabu kama vile haamini nilikuwa ni mimi kweli. Ella hakuwahi kuinuka hata pale niliposema wale wanaoamini waliyosikia wasimame. Lakini alichangia tulipopitisha mchango wa sadaka. Lakini suala la Ella halikunihangaisha, wala sikuwahi kufikiria kumsilimisha, nilimfahamu ni kichwa ngumu na anayechukua tahadhari sana kabla ya kujiunga na chochote. Sikutegemea mtu yeyote amsilimishe Ella zaidi ya Allah mwenyewe.
Nilifunga mikutano kama nilivyofundishwa na bwana Muhammad: “Kwa jina la Allah, mlezi na mwenye rehema. Sifa zote zimuendee Allah, Bwana wa ulimwengu mzima. Bwana mwenye rehema wa siku za hukumu ambazo tunaishi. Ni wewe pekee tunayekutumikia. Hakuna Mungu ila wewe, na Mtukufu Elijah Muhammad ni mtumishi na mtume wako.” Niliamini kuwa Elijah Muhammad alitumwa kwetu na Allah mwenyewe.
Niliinua mkono kuwaashiria kuwa wanaweza kwenda: “Usimfanyie mtu yeyote vile usivyopenda wewe wenyewe kutendewa. Tafuta amani na kamwe usiwe mwenye kuonea— lakini kama mtu akikushambulia, hatufundishi umgeuzie shavu jingine. Allah awabariki mfanikiwe katika yote mfanyayo.”
Ukiacha siku ile niliyolala kwa Ella nilipokuwa naenda Detroit, nilikuwa sijatembelea mitaa ya Roxbury kwa miaka saba. Basi nikaenda kuonana tena na Shorty.
Nilipoonana na Shorty hakuwa kawaida. Habari zilikuwa zimemfikia kuwa nipo mjini na nimezama kwenye mambo fulani ya kidini. Hakuwa na hakika kama nimezama kweli au nilikuwa tu mhubiri –kuwadi mwingine kama wale wanaopatikana kwenye maeneo ya maghetto ya watu weusi. Wale wenye makanisa madogo kwenye fremu za maduka, makanisa ambayo waumini wake wakubwa ni wanawake wazee ambao hufanya kazi kwa bidii kuwafanya wachungaji wao vijana kuvaa kitanashati na kuendesha magari ya gharama. Mara moja nilimfanya Shorty aamini kuwa sikuwa na utani na Uislamu, lakini tuliongea maongezi ya mtaani na tukawa na wakati mzuri. Tulicheka hadi kutokwa na machozi tulipokumbuka jinsi Shorty alivyokuwa Jaji alipoendelea kuhesabu “Kosa la kwanza, miaka kumi. . . kosa la pili, miaka kumi. . . “ tuliongea jinsi ambavyo kuwa na wasichana wale wa kizungu kulitupatia miaka kumi wakati gerezani tumekutana na wafungwa wenye makosa mazito zaidi yetu lakini wakiwa na miaka michache zaidi yetu.
Shorty bado alikuwa na bendi yake ndogo na alikuwa anaendelea vizuri. Alikuwa anajivuna sana kwamba aliweza kusoma muziki akiwa gerezani. Nilimueleza kiasi kuhusu Uislamu na niliona kuwa hakuwa tayari kusikia habari zake. Akiwa gerezani alikuwa amesikia habari mbaya kuhusu dini yetu. Alinikatiza kwa kuingiza masihara kwenye mazungumzo. Alisema kuwa bado hajala nyama ya nguruwe wala kupata wanawake wa kizungu wa kutosha kuridhisha nafsi yake. Sifahamu kama sasa ameridhika, ninachojua ni kuwa sasa ameoa mwanamke wa kizungu. . . na amekuwa mnene kama nguruwe kwa sababu ya kula nguruwe.
Nilionana na John Hughes, mmiliki wa nyumba ya kamari na wengine niliowafahamu ambao bado waliishi Roxbury. Habari juu yangu ziliwafanya wote wasinichangamkie kama kawaida, lakini maneno yangu ya mtaani yalisaidia walau tukawa na maongezi. Wengi wao sikuwaeleza kuhusu Uislamu. Kwa jinsi nilivyoishi nao hapo zamani nilifahamu jinsi walivyochotwa akili.
Nilitumikia kwa muda mfupi sana kama Imam wa Hekalu Namba Kumi na Moja. Mara tu nilipoliweka sawa nikaliacha chini ya Imam Ulysses X, hiyo ilikuwa mwezi wa tatu mwaka 1954. Mtume alinihamishia huko Phildelphia.
Watu weusi wa Philadelphia waliikubali kweli kuhusu mzungu haraka kuliko wale wa Boston. Mwishoni mwa mwezi wa tano mwaka huo Hekalu Namba Kumi na Mbili la Philaelphia likawa limeanzishwa. Ilichukua chini ya miezi mitatu kulianzisha.
Mwezi uliofuata, kutokana na mafanikio yangu ya Boston na Philadelphia, bwana Muhammad aliniteua kuwa Imam wa Hekalu Namba Saba huko jijini New York.
Siwezi kuelezea hisia zangu zilivyokuwa. Maana ili mafundisho ya bwana Muhammad yamuamshe mtu mweusi wa Marekani, ilihitajika Uislamu ukue, ukue sana. Na hakuna sehemu nyingine ndani ya Marekani ambayo hilo liliwezekana zaidi ya wilaya tano za jiji la New York. Huko walikaa watu weusi zaidi ya milioni moja.
LUKAMA Siogye
Niliacha kazi kwenye kampuni ya Ford. Ilikuwa wazi kwangu kuwa Bwana Muhammad anahitaji wahubiri wa kutangaza mafundisho yake na kuanzisha Mahekalu mengine kwa watu weusi milioni ishirini na mbili waliokuwa wameshikwa akili na “kulala” kwenye majiji ya Marekani.
Uamuzi wangu ulikuja mara moja bila kusita. Mara zote nimekuwa ni mwanaharakati, na pengine hilo ndilo lililonifanya nichukue hatua haraka kuliko Maimam wengine. Lakini kila Imam, kwa muda wake na kwa nafasi yake alifikia hitimisho kuwa ilikuwa imeandikwa awe mwanafunzi wa bwana Muhammad, na maisha yake yote yalikuwa ni maandalizi kwa ajili ya suala hilo.
Uislamu unafundisha kuwa kila kinachotokea kimeandikwa.
Kwa miezi kadhaa aliyokuwa akinifundisha, Bwana Muhammad alinikaribisha kumtembelea nyumbani kwake Chicago mara nyingi niwezavyo.
Hata gerezani sikuwahi kusoma na kujifunza kwa makini kama nilivyojifunza chini ya bwana Muhammad. Nilizama kujifunza taratibu za ibada; mafundisho yake juu ya wanawake na wanaume; taratibu za kiuongozi; maana halisi na maana zingine, na matumizi ya Biblia na Quran.
Kila usiku nilienda kulala nikiwa nimeshangazwa zaidi. Kama si Allah basi ni nani mwingine angeweza kuweka hekima ile ndani ya mwanakondoo mnyenyekevu yule kutoka Georgia aliyeishia darasa la nne. Neno “mwanakondoo” nililitoa kwenye unabii unaopatikana kwenye kitabu cha Ufunuo ambako kuna kondoo wa mfano aliyekuwa na upanga wenye makali kuwili mdomoni mwake. Upanga wenye makali kuwili wa bwana Muhammad ulikuwa ni mafundisho yake, ulikata mbele na nyima ili kuiweka huru akili ya mtu mweusi kutoka kushikwa na mzungu.
Nilimhusudu bwana Muhammad kwa maana halisi ya neno la Kilatin nilalomanisha kuhusudu—yaani “Adorare.” Linamaanisha zaidi ya kuhusudu. Linamaanisha kumsujudu kwangu kulikuwa kukuu sana kiasi kwamba ndiye alikuwa mtu pekee niliyewahi kumuogopa—si kuogopa kama kule kumuogopa mtu mwenye bunduki, bali kuogopa kama vile kumuogopa mtu mwenye nguvu za jua.
Baada ya bwana Muhammad kuona kuwa nimeiva alinituma Boston. Ndugu Lloyd X aliishi huko. Aliwakaribisha watu waliopendezwa na mafundisho yake ya Kiislamu kuja kunisikiliza sebuleni kwake.
Nitanukuu niliyosema pale na sehemu nyingine nilizoenda kuhubiri. Maana nakumbuka mambo niliyohubiri mara kwa mara. Nakumbuka siku zile nilipenda sana kuanza na mfano juu ya bwana Muhammad.
“Mungu amempa bwana Muhammad ukweli mkali,” niliwaambia. “Ni kama upanga wenye makali kuwili. Unakukata na kukusababishia maumivu makali, lakini kama unaweza kuukubali ukweli, utakuponya na kukuokoa kutoka katika kifo.”
Baada ya utangulizi huo sikupoteza muda, mara moja nilianza kuwafungua macho juu ya shetani mweupe. ‘Najua hamtambui ukubwa wa madhira ya uhalifu wa mzungu mkristo . . .
‘Hata katika Biblia hakuna uhalifu kama huo! Mungu kwa hasira aliwaua kwa moto waliofanya uhalifu mdogo kuliko huu. Watu weusi milioni mia moja! Mababu wako na wangu! Waliuawa na mzungu huyu ili tu kutufikisha hapa watu milioni kumi na tano na kutufanya watumwa. Njiani aliua watu milioni mia moja. Natamani ningeweza kuwaonyesha sakafu ya bahari ilivyokuwa wakati huo. Miili ya watu weusi, damu, na mifupa iliyovunjwa kwa mateke na marungu. Miili ya wanawake wajawazito waliotupwa baharini baada ya kuwa wagonjwa sana. Wakitupwa baharini kwenye papa, papa waliojifunza kuwa kufuata meli za watumwa ni njia rahisi ya kujipatia chakula.
“Kitendo cha wazungu kubaka wanawake weusi kilianza mle mle melini! Shetani mwenye macho ya bluu hakusubiri awafikishe kwanza! Binadamu aliyestaarabika hajawahi kushuhudia uchafu na mauaji na namna ile ”
Kuzungumzia ubaya wa utumwa hakujawahi shindwa kuwagusa watu weusi. Inashangaza sana kuona watu wengi
weusi wamekubali mzungu awapotoshe kiasi cha wengine kudhani kuwa enzi za utumwa zilikuwa enzi za starehe! Mara baada ya kuwachochea kwa habari za utumwa nilianza kuwazungumzia wao wenyewe.
‘Nataka mtakapo chumbani hapa muone hili kila mnapoonana na shetani wa kizungu. Ndiyo, ni shetani. Nataka muanze kumchunguza kwenye maeneo yake ambayo hataki nyinyi muwepo. Mchunguzeni anapokuwa anajifunua waziwazi.
“Kila mara unapomuona mzungu, fikiria kuhusu shetani unayemuona! Fikiria kuwa ni kupitia damu na jasho la babu zako watumwa ndiyo alijenga Milki hii ambayo leo hii ndiyo nchi tajiri kuliko zote duniani-dunia inayomchukia kutokana na uovu na tama yake.
Kila mkutano, wale waliofika mkutano uliopita walirudi wakiwa na rafiki zao. Hakuna hata mmoja wao aliyewahi kushuhudia mzungu akivuliwa kinyago alichojivika. Kila baada ya mkutano niliuliza, “kila anayeamini aliyosikia asimame.” Sikumbuki kuona mtu ambaye hakusimama. Na hata siku za Jumapili usiku niliposema, “Nani anataka kuwamfuasi wa Mtukufu Elijah Muhammad?” walisimama hata wale ambao niliona wazi hawako tayari.
Baada ya kama miezi mitatu tulikuwa na watu wa kutosha kuweza kufungua Hekalu dogo. Nakumbuka furaha tuliyokuwa nayo tulipokodi viti vya kukunjwa kwa ajili ya Hekalu letu. Nilijawa na furaha sana siku niliyomjulisha bwana Muhammad anuani ya Hekalu letu.
Ni wakati tulipopata Msikiti huu mdogo ndipo dada yangu Ella alianza kuja kunisikiliza. Alikaa na kustaajabu kama vile haamini nilikuwa ni mimi kweli. Ella hakuwahi kuinuka hata pale niliposema wale wanaoamini waliyosikia wasimame. Lakini alichangia tulipopitisha mchango wa sadaka. Lakini suala la Ella halikunihangaisha, wala sikuwahi kufikiria kumsilimisha, nilimfahamu ni kichwa ngumu na anayechukua tahadhari sana kabla ya kujiunga na chochote. Sikutegemea mtu yeyote amsilimishe Ella zaidi ya Allah mwenyewe.
Nilifunga mikutano kama nilivyofundishwa na bwana Muhammad: “Kwa jina la Allah, mlezi na mwenye rehema. Sifa zote zimuendee Allah, Bwana wa ulimwengu mzima. Bwana mwenye rehema wa siku za hukumu ambazo tunaishi. Ni wewe pekee tunayekutumikia. Hakuna Mungu ila wewe, na Mtukufu Elijah Muhammad ni mtumishi na mtume wako.” Niliamini kuwa Elijah Muhammad alitumwa kwetu na Allah mwenyewe.
Niliinua mkono kuwaashiria kuwa wanaweza kwenda: “Usimfanyie mtu yeyote vile usivyopenda wewe wenyewe kutendewa. Tafuta amani na kamwe usiwe mwenye kuonea— lakini kama mtu akikushambulia, hatufundishi umgeuzie shavu jingine. Allah awabariki mfanikiwe katika yote mfanyayo.”
Ukiacha siku ile niliyolala kwa Ella nilipokuwa naenda Detroit, nilikuwa sijatembelea mitaa ya Roxbury kwa miaka saba. Basi nikaenda kuonana tena na Shorty.
Nilipoonana na Shorty hakuwa kawaida. Habari zilikuwa zimemfikia kuwa nipo mjini na nimezama kwenye mambo fulani ya kidini. Hakuwa na hakika kama nimezama kweli au nilikuwa tu mhubiri –kuwadi mwingine kama wale wanaopatikana kwenye maeneo ya maghetto ya watu weusi. Wale wenye makanisa madogo kwenye fremu za maduka, makanisa ambayo waumini wake wakubwa ni wanawake wazee ambao hufanya kazi kwa bidii kuwafanya wachungaji wao vijana kuvaa kitanashati na kuendesha magari ya gharama. Mara moja nilimfanya Shorty aamini kuwa sikuwa na utani na Uislamu, lakini tuliongea maongezi ya mtaani na tukawa na wakati mzuri. Tulicheka hadi kutokwa na machozi tulipokumbuka jinsi Shorty alivyokuwa Jaji alipoendelea kuhesabu “Kosa la kwanza, miaka kumi. . . kosa la pili, miaka kumi. . . “ tuliongea jinsi ambavyo kuwa na wasichana wale wa kizungu kulitupatia miaka kumi wakati gerezani tumekutana na wafungwa wenye makosa mazito zaidi yetu lakini wakiwa na miaka michache zaidi yetu.
Shorty bado alikuwa na bendi yake ndogo na alikuwa anaendelea vizuri. Alikuwa anajivuna sana kwamba aliweza kusoma muziki akiwa gerezani. Nilimueleza kiasi kuhusu Uislamu na niliona kuwa hakuwa tayari kusikia habari zake. Akiwa gerezani alikuwa amesikia habari mbaya kuhusu dini yetu. Alinikatiza kwa kuingiza masihara kwenye mazungumzo. Alisema kuwa bado hajala nyama ya nguruwe wala kupata wanawake wa kizungu wa kutosha kuridhisha nafsi yake. Sifahamu kama sasa ameridhika, ninachojua ni kuwa sasa ameoa mwanamke wa kizungu. . . na amekuwa mnene kama nguruwe kwa sababu ya kula nguruwe.
Nilionana na John Hughes, mmiliki wa nyumba ya kamari na wengine niliowafahamu ambao bado waliishi Roxbury. Habari juu yangu ziliwafanya wote wasinichangamkie kama kawaida, lakini maneno yangu ya mtaani yalisaidia walau tukawa na maongezi. Wengi wao sikuwaeleza kuhusu Uislamu. Kwa jinsi nilivyoishi nao hapo zamani nilifahamu jinsi walivyochotwa akili.
Nilitumikia kwa muda mfupi sana kama Imam wa Hekalu Namba Kumi na Moja. Mara tu nilipoliweka sawa nikaliacha chini ya Imam Ulysses X, hiyo ilikuwa mwezi wa tatu mwaka 1954. Mtume alinihamishia huko Phildelphia.
Watu weusi wa Philadelphia waliikubali kweli kuhusu mzungu haraka kuliko wale wa Boston. Mwishoni mwa mwezi wa tano mwaka huo Hekalu Namba Kumi na Mbili la Philaelphia likawa limeanzishwa. Ilichukua chini ya miezi mitatu kulianzisha.
Mwezi uliofuata, kutokana na mafanikio yangu ya Boston na Philadelphia, bwana Muhammad aliniteua kuwa Imam wa Hekalu Namba Saba huko jijini New York.
Siwezi kuelezea hisia zangu zilivyokuwa. Maana ili mafundisho ya bwana Muhammad yamuamshe mtu mweusi wa Marekani, ilihitajika Uislamu ukue, ukue sana. Na hakuna sehemu nyingine ndani ya Marekani ambayo hilo liliwezekana zaidi ya wilaya tano za jiji la New York. Huko walikaa watu weusi zaidi ya milioni moja.
LUKAMA Siogye