Kitchen Parties zinasaidia Kuimarisha Ndoa na Mapenzi au ni tatizo...

Hebu fafanua kwa lugha nyepesi hii kauli nielewe

ha hahaaaa CPU!!! hayo maneno nilisikia tu kwenye kitchen party fulani sikuambiwa mimi!! usi panic bure!!!
 
For me i wish kungekuwa na harusi tu NO SEND OFF, NO KITCHEN PARTY huo ni mtazamo wangu
 

Unajua, usipende kuwa dictator katika maisha ya ndoa yajayo au ambayo unayo, utabaki unanyooshewa vidole bila sababu za msingi. Huwezi in any how kumkataza mtarajiwa wako eti asifanyiwe kitchen party!!! Labda uniambie umevuta mwanamke ukakaa naye for sometime then unataka kuhalalisha kwa njia ya ndoa. Lakini kama binti unamuoa akiwa bado kwa wazazi wake, huwezi narudia tena kumkataza asifanyiwe kitchen party.KP kwa kawaida inaendeshwa kulingana na wanafamilia wanavyotaka na walivyo kwa asili yao.
MC au mtoa mada siku zote anaambiwa shughuli hii ni ya watu gani! kama mcharuko basi mwanzo mwisho shughuli itakuwa ya kimcharuko, kama ya kidini basi mwanzo mwisho sherehe itaendeshwa kidini, hakuna kitu kinacholazimishwa pale iwapo wahusika hawakitaki. Na ukweli ni kwamba KP siku hizi inakaribia kufuta send-off, na ukilinganisha hata ukifanya comparison ya zawadi alizopata binti kwenye send-off na KP utagundua kp ndo kapata zawadi nyingi, na za maana kuliko kwenye send-off japo na wanaume walishiriki. Kiukweli kp siku hizi lengo kubwa sio matusi, bali ni kupata vyombo hasa vya jikoni kwa binti, na mafundisho ya hapa na pale ingawa ya ndani hayafundishwi hadharani
Ushauri wangu wa bure kwako ni kwamba, wewe ukichagua binti mstaarabu basi tegemea kp atakayofanyiwa itakuwa ya kiistaarabu, ila ukichagua mswahili na mcharuko basi tegemea kp kuwa ya aina hiyo, lakini si wewe kuwapangia wazazi eti wasimfanyie kp binti yao!!!!!!!! utakosa mchumba kaka
 
pEARL YOU HAVE A POINT kwa familia nyingi, KP ni just another party, socialization and bla bla! Ni sehemu ya mama kuonyesha socail network zake, anajulikana kiasi gani na zawadi alizokusanya kwa binti!

Coming to think of maadili, labda kuna vitu vichache vinaweza kupatikana hapo kwenye KP, lakini nyingi ni kumwaga radhi na kumwambia mwanamke jinsi ya kumhudumia.kumfurahisha mumewe. On the other hand, mwanaume haelezwi jinsi ya kuishi, kumtunza na kumfurahisha mkewe (kumbukeni thread yangu ya nyuma). Mwisho wa siku, kitchen party ni ya zawadi!
 


Haa!aine??nikose mchumba kwa ajili ya KP??Sidhani!!
Kuna swali sijibiwi...wanaume wanafuata nini kwenye KP??
Na kwanini KP nyingi zimebadilisha maana??na kwanini ziendelee kuitwa KP??
Kwanini wasiseme tunaenda kwenye mdundiko tu..??
Halafu inshu ya kusema eti kwenye KP anapata zawadi nyingi kushinda kwenye send-off is HolyCrap!!Imagine mke wangu hafanyi Kp bali anafanya Send-off tu,kwanza atakuwa amebalance bajeti, isitoshe wale ambao waliandaa zawadi za kp watazileta kwenye SO..kwahiyo percel zitakuwa maradufu!! u get the point??

Hii kitu si udikteta, bali ni ninyi wenyewe akina mama kuichakachua hii kitu KPs..u get that??
 
Hii sio kitchen party, ni kufundishana uhuni....
 
si kweli kitchen party sinasaidia sana kuimarisha ndoa
 
Kama mwanaume naona KP iko poa tu, tena itakusaidia kujua aina ya familia unayo kwenda kuoa Watu wenye staha na maadili yao wataalikana na watu wanaoendana nao. usitegemee familia iliyopinda ikawa na kp iliyonyooka, lazima wachukuane wenye mitazamo inayoendana na kuweka mipaka.
 
KP haiimarishi wala kuvunja ndoa. Ni kitu ambacho kimekuja karibuni wakati ndoa zilikuwepo miaka nenda rudi.
 
Amini usiamini KP za sasa hivi 99.9% ni kwa ajili ya kupokea vyombo tu na si vinginevyo.
UTAKUTA MSICHANA/MWANAMKE ANA WATOTO WADOGO KWA WAKUBWA eti anafanyiwa KP,
WANAISHI PAMOJA NA HUYO MWANAUME eti bado anafanyiwa KP,
ANAMIMBA TENA KUUBWA eti anafanyiwa KP,
ALIWAHI KUOLEWA NA KUACHIKA eti anafanyiwa KP,
ANAITWA NA MAMA AU BIBI eti anafanyiwa KP,
HAPO LENGO KUU LA HIYO KP NI KUKUSANYA VYOMBO TU NA SI VINGINEVYO.....
HATA KUKIWA NA LENGO LINGINE BADO SIAMINI KUWA SOMO LA SIKU MOJA LINAWEZA KUJENGA TABIA,
TENA ETI TABIA NJEMA KATIKA NDOA.

NIJUAVYO MIMI NI RAHISI ZAIDI KUTOA ELIMU YA MAOVU NA IKAELEWEKA KIRAHISI ZAIDI NA KWA MUDA MFUPI,
KULIKO ELIMU YA MAMBO MEMA AMBAYO HUCHUKUA MUDA MREFU/ UVUMILIVU KATIKA KUELEWEKA NA KUJIJENGA.

PIA KP HAIHUSIKI KUIJENGA NDOA WALA KUIVUNJA.
WANAOJENGA NA KUVUNJA NDOA NI WANANDOA WENYEWE.

Nawaomba WANA JF wenzangu siku yangu ya KP nawaomba mfike bila kukosa eti eeh ila SIYO MIKONO MITUPU....lol
 
Hii mada ni nzuri sana............Carmel na Pearl michango yenu imekaa kirealistic zaidi kuliko wengi tunavyotizama............ aksanteni na mbarikiwe wote mliochangia humu.
KP inategemea inafanywa na watu wa familia gani na kivipi otherwise si KP zote ni ovu na si zote hufanyika kwa siku moja kuna ambazo zinakwenda ndani ya wiki nzima ambapo binti anapewa mafunzo ndani si adharani na wamama waliosafi na ndoa zao na kisha siku ya mwisho ndo sherehe ambapo hupatiwa na zawadi.
 
Ati lengo ni 'kupata zawadi tu'!....kama ni hivyo nadhani tuna matatizo makubwa sana vichwani mwetu...sijui tumerogwa na nani! Hivi kweli unaandaa sherehe kwa gharama kubwa ili upate zawadi tu? Ni umasikini wa aina gani unatusumbua?
 

Hujanitaja??hahaaa...
 
Ni kweli utakosa mchumba kwa maana kwamba, kama ukipata mchumba then unampa masharti ya kutofanya kp, unadhani atakapoliwakilisha kwa wazazi wake responce itakuwaje? Imagine huyo akutolee nje just bcoz of that, ukapata mwingine the same si utapata tabu hata wewe mwenyewe tena itabidi urudishe nyuma maamuzi yako. Na mabinti wengi wa siku hizi wana-prefer kp zaidi kuliko send-off
1. Wanaume kimsingi hawatakiwi kwenye kp, isipokuwa wao wanakuja kikazi zaidi, kupiga picha za mnato na video.Ukweli ni kwamba hatuna wataalam wa masuala ya video wengi na picha za mnato, ndiyo maana inalazimu kuita wanaume lakini si kusudio.
2. Kubadilishwa maana kwa kp narudi pale pale, inategemea na wahusika wa tukio ni wa aina gani
3. Kwamba aseme tunaenda kwenye mdundiko! yenyewe initwa kitchen party ( sherehe/pati ya jikoni)sasa watasemaje wanaenda kwenye mdundiko? ebu kuwa realistic Sizinga bwana
 
Ati lengo ni 'kupata zawadi tu'!....kama ni hivyo nadhani tuna matatizo makubwa sana vichwani mwetu...sijui tumerogwa na nani! Hivi kweli unaandaa sherehe kwa gharama kubwa ili upate zawadi tu? Ni umasikini wa aina gani unatusumbua?
SMU
Hapana hili si lengo zima la KP ingawa maana halisi siku hizi imepotea lakini kwa kuanza ilikuwa ni sehemu ya kumfunda mwali namna ya kuishi na mume pamoja na kuitunza familia mpya anayokwendaianzisha. Ni sehemu ya mwendelezo wa unyago kwa kina binti ambapo ni kama level nyingine ya juu baada ya unyago. Lakini siku zilivyozidi kwenda ikageuka kuwa sherehe ya kumpongeza binti kwa kumpata mwenzi wake au kumletea mama/mzazi wa kike heshima nyumbani (na ndio maana wahusika wakuu huwa ni wanawake zamani ilikuwa wamama watu wazima kisha na wasichana wakaanza kualikwa kukidhi sehemu ya marafiki wa binti)

Ila siku zinavyozidi kwenda ndio maana halisi ya KP inavyozidi kupotea.......... kwa sasa hivi nyingi hazina tofauti na send offs.
 
Reactions: SMU
Aksante Aine
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…