Kitendo cha mkuu wa mkoa kukamia timu kubwa ligi kuu kikemewe

wakimataifa.

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2015
Posts
1,625
Reaction score
558
Inasikitisha kusikia mkuu wa mkoa akizikamia timu kubwa kuhakikisha zinafungwa zikicheza na timu mkoa husika.
Hizi tabia ni za kusikitisha sana zote zipo nchini
Tabia hizo zipo sana hasa mikoa ya musoma,kagera,mwanza na mtwara.
Mbona hatusikii timu za mkoa wake zinazocheza na timu ndogo
Tunaomba vyombo vinavyohusika kukemea vitendo hivyo
 
Siku ya kesho ni shida kaitaba.


Halafu usimsingizie mkuu wa mkoa .yeye anataka timu ya mkoa wake ichukue ligi kuu.


Kagera wanafunga kila timu sio Simba tu
 
Kwani kuna ubaya?
Hakuna ubaya, anatakiwa ajiweke tu wazi ka Ali Api wa iringa na akina Jeri Muro.
Asije akajifanya anahamasisha ili apate public sentiment, afu baada ya mechi ya Simba anapotea haijali tena team.
 
Hv mkuu wa mkoa wa kagera mnamfahamu vzr au mnamsikia? Yule ni Brigeidia General Gaguti bonge moja la mkuu wa mkoa ila kwa vile hapati attention kubwa ya vyombo vya habari hamuwezi kuwa mnamjuwa. Wakati wa mechi ya play off kati ya kagera na stend united alinunua mechi yote mashabiki waingie bule. Kwahyo wanamikia Fc taratibu tafadhali kama tuliwafunga mechi zote mbili msimu uliopita tukiwa na kikosi dhaifu sijui safari kwa kikosi hiki tutawapiga ngapi hapo kesho?
 
Mimi ni simba lakini sioni tatizo hapo kwenye uhamasishaji wa mkuu wa mkoa wa Kagera ili mradi tu waamuzi wachezeshe kwa haki bila kuipendelea timu mwenyeji. Wangepatikana wakuu wa mikoa wengi wenye uhamasishaji kama huu soka lingekuwa sana kwani timu za mikoani zingekuwa zinapania kwa kujiandaa vizuri na hizi timu kubwa zingekuwa zinajiandaa vya kutosha ili kuepusha kuaibishwa. Tukiacha hizi timu kubwa zikawa zinaenda mikoani zikijua zinaenda tu kujichukulia pointi mpira wetu hautapiga hatua. Ni wakati sasa wa Simba kuonyesha thamani ya mabilioni ya usajili wao kulinganisha na usajili wa mamilioni kama sio wa malaki wa Kagera Sugar na sio muda wa kuanza kuangalia sijui mkuu wa mkoa kakamia mechi.
 
Yaani hilo ndo jambo la msingi haiwezekani unaacha timu ya eneo lako unaenda kuishabikia timu nyingine.
But, kwa mpira wa hapa bongo umeingiliwa na siasa za mpira wa Simba na Yanga hilo hakuna aliyepona.
Ndo mana wajuzi wa mambo tunasema kwa nia ile ile aliyonayo tuone pia uhamasishaji wa nguvu hata Yanga akienda kucheza pale kaitaba na Kagera sugar.
 
Tupo pamoja mkuu. Wakuu wa mikoa wahamasishe lakini wasiingilie mchakato wa mchezo uwanjani. Lakini hao Kagera wakiingiza siasa kwenye mpira kwamba wao wanakamia mechi moja tu ya Simba lakini ya Yanga hawakazi yatakuja kuwakuta yale yale ya Toto African kutamba kumfunga Simba huku wanashuka daraja.
 
Hakuna ubaya, anatakiwa ajiweke tu wazi ka Ali Api wa iringa na akina Jeri Muro.
Asije akajifanya anahamasisha ili apate public sentiment, afu baada ya mechi ya Simba anapotea haijali tena team.

Mbona hujamtaja rc wa Dar, mbumbumbu mna shida gani viongozi wakiwa upande wa Mikia mnakuwa kimya ila wakiwa upande wa pili mnaumia.... Shida ni nini?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…