HAKI KWA WOTE
JF-Expert Member
- Nov 30, 2022
- 1,108
- 1,132
Habari wadau,
Kumetokea sitofahamu hivi karibuni kati ya wakusanya madeni na waendesha minada ya CRDB BANK kitengo cha kukukusanya madeni baada ya CRDB benki kutoa kazi kwa madalali hao kisha kuingilia kati mchakato huo kwa kuwasiliana moja kwa moja na wadaiwa na kuwaomba rushwa ili kusitisha zoezi husika.
Hii imekuwa ni kawaida ya maofisa hao walioko CRDB makao makuu kitengo cha kurejesha mikopo kupokea rushwa na kusitisha uuzwaji wa mali za wadaiwa bila kufuata taratibu na kuwataka madalali nao walipwe na wanunuzi au mwenye mali kinyume na mikataba ya kazi.
Nashauri vyombo husika vilimulike hili kwani rushwa imetawala CRDB kitengo cha urejeshaji mikopo na kusababisha mikopo isilipwe kwa wakati kwa kukwamisha madalali kufanya kazi zao kwa kutolipwa 10% za madalali ambazo huzichukua wao kutoka kwenye fedha za mnada na kuwaelekeza madalali wakalipwe na wadaiwa au wanunuzi wa dhamana husika.
Kumetokea sitofahamu hivi karibuni kati ya wakusanya madeni na waendesha minada ya CRDB BANK kitengo cha kukukusanya madeni baada ya CRDB benki kutoa kazi kwa madalali hao kisha kuingilia kati mchakato huo kwa kuwasiliana moja kwa moja na wadaiwa na kuwaomba rushwa ili kusitisha zoezi husika.
Hii imekuwa ni kawaida ya maofisa hao walioko CRDB makao makuu kitengo cha kurejesha mikopo kupokea rushwa na kusitisha uuzwaji wa mali za wadaiwa bila kufuata taratibu na kuwataka madalali nao walipwe na wanunuzi au mwenye mali kinyume na mikataba ya kazi.
Nashauri vyombo husika vilimulike hili kwani rushwa imetawala CRDB kitengo cha urejeshaji mikopo na kusababisha mikopo isilipwe kwa wakati kwa kukwamisha madalali kufanya kazi zao kwa kutolipwa 10% za madalali ambazo huzichukua wao kutoka kwenye fedha za mnada na kuwaelekeza madalali wakalipwe na wadaiwa au wanunuzi wa dhamana husika.